Jumakidogo
R I P
- Jul 16, 2009
- 1,851
- 417
Mh Mnyika CHADEMA na Mh Ndugulile CCM walikuwa na hoja ya dharura leo katika kikao cha bunge, tena hoja ya msingi kwa mustakabari wa afya na uhai wa Watanzania kutokana na mgomo wa madaktari. Kwa vyovyote vile huu ndiyo ulikuwa wakati mwafaka wa bunge kujadili na kutafuta njia ya kutatua utata huu. Hata hivyo wabunge wetu wameonyesha kuwa suala hili halijawagusa kiasi cha kuona hakuna haja ya kuwaunga mkono wenzao. Kwa hili wabunge wetu hawajaonyesha uzalendo. Inaonyesha wanajali maslahi yao zaidi kuliko matatizo ya wananchi walio wengi. Kwa hili madaktari kuna haja ya kuendelea kukaza uzi na kuendelea na mgomo wenu mpaka pale watakapoamua kuwasikiliza.