Wabunge wa Upinzani Watoka Bungeni tena, ni baada ya kunyimwa nafasi ya Muongozo

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,717
55,819
Hali ya sintofahamu imeendelea ndani ya bunge, baada ya wabunge wote wa Upinzani kutoka ndani ya bunge, mara baada ya Wabunge kuanza kuchangia hotuba ya Rais.

Baada ya Maswali na Majibu, yalifuata matangazo, baada ya Matangazo, wabunge wakaanza kuomba muongozo lakini Naibu Spika Mhe. Tulia, hakuweza kuwapa nafasi ya Kuongea. Mtu akiomba Muongozo anasimama na kusema Mimi nikisimama mbunge inabidi ukae, Mbunge akikaa anamuita mchangiaji. Mbunge akiomba muongozo, naibu Spika anasimama tena na kusema nikisimama inabidi ukae.

Mwisho wa yote wabunge wa Upinzani wakaamua kutoka nje kwa kile wanachodai wamenyimwa nafasi ya kusikilizwa walipoomba muongozo ndani ya bunge.

Wabunge wa CCM, wanaendelea na kujadili Hotuba ya Rais.
bunge1.jpg


 
Natizama Star tv. Wabunge wa UKAWA wanatoka baada ya Kubenea kunyimwa nafasi ya kuomba ''muongozo''
Wanaulizwa ''mmesha-saini posho ?''.
Ni kituko kingine..kama jana.
 
Ghosryider,
Unaogopesha kweli kwa uchangiaji wako. Sasa, hicho ulichoona hao UKAWA wapo kimaslahi zaidi ni kipi? Kwani wajua kuwa huo "Muongozo" waliokuwa wakiomba ulihusu nini?? Jamani tuwe wenye busara kidogo tu, tuchangie ki-Great Thinkers zaidi
 
Vipi zitto ametoka?
nawapongeza ukawa kwa kutoka nje, waache mamburula wa lumumba waendelee kujadili hiyo hotuba ya rais wao
 
Back
Top Bottom