Wabunge wa CCM tupeni katiba nyingine

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
12,307
12,602
Tuko chini ya miguu yenu ndugu zetu na watanzania wenzetu wabunge kwa tiketi ya CCM

. Katiba hii ya 1977 haitufai watanzania wote bila kubagua chama, dini, kabila, jinsia wala kanda zetu tunakotoka. Iko siku Mungu pishia mbali watanzania tunawezakuja kumpata kiongozi ambaye ni dictator, mlevi, au fisadi na tusijue nini chakufanya. Katiba hii inategemea uadilifu na huruma ya kiongozi aliyeko madarakani kwa watanzania wenzake.

Wabunge wa CCM ndio wenye turufu ya taifa hili ama kuelekea kuzuri au kubaya kutokana na wingi wao bungeni. Kiongozi mbaya haangalii chama wala wanachama wa chama fulani, bali anaongozwa na maslahi yake na ya wale wanaomzunguuka tu.

Tunaomba chondechote tuibadilishe katiba hii muda utakapofika kwa kuliangalia taifa na vizazi vijavyo.
 
Back
Top Bottom