Power G
JF-Expert Member
- Apr 20, 2011
- 3,886
- 1,193
Hali ya kisiasa ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) inatazamiwa kukumbwa na mtikisiko kutokana na kuwepo nia ya kumtaka Rais Jakaya Kikwete, ahojiwe bungeni.
Taarifa za ndani zilizolifikia NIPASHE Jumamosi zinaeleza kuwa, hatua hiyo inatarajiwa kufanikishwa kupitia mabadiliko ya kanuni yatakayoamuru Rais wa nchi kuhojiwa na Bunge kupitia maswali ya papo kwa hapo, badala ya Waziri Mkuu kama ilivyo sasa.
Wachunguzi wa mambo ya siasa wanaielezea hali hiyo kuwa huenda ikakumbwa na mtikisiko na malumbano ya kisheria kati ya makundi yanayounga mkono mfumo uliopo sasa na wale wanaomtaka Rais aulizwe maswali.
Hadi kufikia sasa, imebainika kuwa hoja hiyo inatarajiwa kuwasilishwa na Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Ritta Enespher Kabati.
Kabati amethibitisha azma hiyo lakini akapinga kwamba inatokana na shinikizo la kundi moja kati ya yanayopingana ndani ya CCM.
"Mimi sina haja ya kupata shinikizo lolote, nina akili na uwezo wangu, ninatambua kwamba ninawatumikia wananchi wa Iringa hasa wanawake," alisema katika mahojiano yake na NIPASHE Jumamosi.
Kabati alisema nia ya kuwasilisha hoja hiyo inatokana na uchunguzi aliowahi kuufanya kwa nyakati tofauti na kubaini kwamba asili ya kipindi cha maswali kwa Waziri Mkuu ni Bunge la Uingereza ambapo Waziri Mkuu ana mamlaka ya kuwa Mtendaji Mkuu wa serikali, tofauti na ilivyo hapa nchini.
"Ninavyouona mfumo huu, tunahitaji kufanya marekebisho ili badala ya Waziri Mkuu kuulizwa maswali ya papo kwa hapo, awe anakuja Rais wa nchi," alisema.
Kabati alisema mfumo uliopo sasa ambapo Waziri Mkuu anashindwa kutoa majawabu ya baadhi ya hoja za wabunge anazoulizwa, isipokuwa kuelekeza kwenye mamlaka ya Rais, kunatoa fursa ya kufanya mabadiliko hayo.
"Kama unavyolifuatilia Bunge kuna wakati Waziri Mkuu anatoa majawabu yasiyowaridhisha wabunge, inafikia wakati anaonekana anadanganya na hata kufikia hatua ya kudhalilishwa kama ilivyowahi kutokea wakati Godless Lema alipokuwa Mbunge wa Arusha Mjini.
Lema aliwahi kuliambia Bunge kuwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alilidanganya Bunge wakati akitoa majibu kuhusu mgogoro uliosababisha mauaji ya raia mjini Arusha, hali iliyosababisha kiti cha Spika kumpa siku saba kuthibitisha kabla ya kutolewa mwongozo.
Hadi kufikia sasa, gazeti hili halijapata kumbukumbu zinazoonyesha kuwa Spika wa Bunge, Anne Makinda ama wasaidizi wake walishatoa bungeni utetezi wa Lema kuhusu hoja hiyo.
"Kwa hiyo ninaona kwamba kama Rais atakuwa anakuja kujibu maswali kila Alhamis, itasaidia kupunguza mkanganyiko na wakati mwingine kumfanya aonekane anadanganya," Kabati alisema.
Source: Nipashe
My Take:- Iwapo huu utaratibu utaafikiwa, "DHAIFU" atakuwa na majibu ya kuwaridhisha wabunge kuliko "LIWALO NA LIWE"? Naona kama hawa wabunge wana hamu ya kupewa majibu ya uongo na ahadi hewa zisizotekelezeka.
Taarifa za ndani zilizolifikia NIPASHE Jumamosi zinaeleza kuwa, hatua hiyo inatarajiwa kufanikishwa kupitia mabadiliko ya kanuni yatakayoamuru Rais wa nchi kuhojiwa na Bunge kupitia maswali ya papo kwa hapo, badala ya Waziri Mkuu kama ilivyo sasa.
Wachunguzi wa mambo ya siasa wanaielezea hali hiyo kuwa huenda ikakumbwa na mtikisiko na malumbano ya kisheria kati ya makundi yanayounga mkono mfumo uliopo sasa na wale wanaomtaka Rais aulizwe maswali.
Hadi kufikia sasa, imebainika kuwa hoja hiyo inatarajiwa kuwasilishwa na Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Ritta Enespher Kabati.
Kabati amethibitisha azma hiyo lakini akapinga kwamba inatokana na shinikizo la kundi moja kati ya yanayopingana ndani ya CCM.
"Mimi sina haja ya kupata shinikizo lolote, nina akili na uwezo wangu, ninatambua kwamba ninawatumikia wananchi wa Iringa hasa wanawake," alisema katika mahojiano yake na NIPASHE Jumamosi.
Kabati alisema nia ya kuwasilisha hoja hiyo inatokana na uchunguzi aliowahi kuufanya kwa nyakati tofauti na kubaini kwamba asili ya kipindi cha maswali kwa Waziri Mkuu ni Bunge la Uingereza ambapo Waziri Mkuu ana mamlaka ya kuwa Mtendaji Mkuu wa serikali, tofauti na ilivyo hapa nchini.
"Ninavyouona mfumo huu, tunahitaji kufanya marekebisho ili badala ya Waziri Mkuu kuulizwa maswali ya papo kwa hapo, awe anakuja Rais wa nchi," alisema.
Kabati alisema mfumo uliopo sasa ambapo Waziri Mkuu anashindwa kutoa majawabu ya baadhi ya hoja za wabunge anazoulizwa, isipokuwa kuelekeza kwenye mamlaka ya Rais, kunatoa fursa ya kufanya mabadiliko hayo.
"Kama unavyolifuatilia Bunge kuna wakati Waziri Mkuu anatoa majawabu yasiyowaridhisha wabunge, inafikia wakati anaonekana anadanganya na hata kufikia hatua ya kudhalilishwa kama ilivyowahi kutokea wakati Godless Lema alipokuwa Mbunge wa Arusha Mjini.
Lema aliwahi kuliambia Bunge kuwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alilidanganya Bunge wakati akitoa majibu kuhusu mgogoro uliosababisha mauaji ya raia mjini Arusha, hali iliyosababisha kiti cha Spika kumpa siku saba kuthibitisha kabla ya kutolewa mwongozo.
Hadi kufikia sasa, gazeti hili halijapata kumbukumbu zinazoonyesha kuwa Spika wa Bunge, Anne Makinda ama wasaidizi wake walishatoa bungeni utetezi wa Lema kuhusu hoja hiyo.
"Kwa hiyo ninaona kwamba kama Rais atakuwa anakuja kujibu maswali kila Alhamis, itasaidia kupunguza mkanganyiko na wakati mwingine kumfanya aonekane anadanganya," Kabati alisema.
Source: Nipashe
My Take:- Iwapo huu utaratibu utaafikiwa, "DHAIFU" atakuwa na majibu ya kuwaridhisha wabunge kuliko "LIWALO NA LIWE"? Naona kama hawa wabunge wana hamu ya kupewa majibu ya uongo na ahadi hewa zisizotekelezeka.