Watu wasiojulikana, wamebomoa kaburi na kisha kumvua nguo marehemu na kuiba vitu kadhaa alivyozikwa navyo yakiwemo mabegi mawili, pamoja na Vito kadhaa vya thamani na kisha kutoweka huko Kibaha, mkoani Pwani.
Kwa mujibu wa watu wa karibu na eneo hilo, walisema kuwa baada ya mazishi hayo kufanyika, ndugu waliweka mlinzi maalum wa kulilinda kaburi hilo kwa muda wa wiki 3, na baada ya muda huo kwisha na kisha mlinzi huyo kuondoka, ndipo lilipotokea tukio hilo lililowaacha watu wengi kutoamini kilichotokea.
Chanzo: Kado Cool
Hiyo ushawahi kutokea miaka ya nyuma Ktk makaburi ya mwananyamala, kuna bahari mmoja alizikwa na dhahabu, usiku wahuni wakamfukua
Kuchukua dhahabu zile alizovaa
walivyo mzika na mabegi na vito walitegemea nini na kwa nini wamemzika na mabegi au huko aendako akabadili nguo au akafanye biashara mambo mengine hayahitaji akili za kuambiwa kabisa yaani
Makaburi ya kinondoni watu mpka leo wanaiba mishumaa na madhara ya mama, sasa wakiskia mtu kazikwa na vitu vya thamani unafikiri watakuacha, watakufukua tu masela
Kwa hapa ndipo napo ona Imani ya ndugu zangu waislam haina mbwembwe kwenye suala la mazishi sasa mtu mnamzika na vito vya thamani vya nini sasa? Hata ningekuwa ni mimi ningefukua tu maana nitakuwasina dhambi kwa sababu niliyemuibia hana kauli.
Walimzika na vitu vya thamani ili akavithainishaje huko kaburini? jamaa alikuwa anapenda anasa duniani na kaburini anajinaksi amfurahishe nani? wacha vichukuliwe kwa sababu ni mali ya dunia.
Safi sana vijana ni kawaida kabisa vito vya thamani kufukuliwa chini na nyie mmevitoa chini hongereni sana kama mngevichukua akiwa juu mngekuwa mmeiba...nawapongeza kwa kazi nzuri
Kweli haya mambo ni magumu sana..nakumbuka mwaka juzi kuna jamaa angu alifiwa na Mama ake pale kibaha mailmoja..siku ya kuzika walishusha na mabegi yake ya nguo..nikashangaa sana..baadae nikauliza imekuwaje..jamaa wakasema Maza wao alikuwa ni mshirikina na inasemekana hata bro wao wa kwanza alifariki kwenye mazingira ya kishirokina so kama familia wakaona isiwe kesi..kila kitu chake wakifukie..nikachoka..!!