Waasisi wa neno uzalendo ni watawala

Waasisi wa neno uzalendo ni watawala

Cally30

Member
Joined
Mar 28, 2017
Posts
5
Reaction score
4
Kivuli cha neno UZALENDO kinaangazia zaidi watu masikini, huku kikiwapa watawala fursa ya kujineemesha.

Madaktari, Walimu na watumishi wengine wa umma na sekta binafsi mfano wakulima wakibebeshwa msalaba wa uzaledo.

Hakuna mtawala anayeshiriki ktk kuubeba msalaba UZALENDO. Fikra na AKILI zao zimelenga kutufanya tusitoke shimoni, tukose afya ya mwili na akili ili mambo yao yawe sawa.

NI Mbunge gani angepewa hata kama ni milioni 2 kwa mwezi angekaa pale!!.Tunapo hamasisha uzalendo kwa pamoja tujali maslahi ya kila nafsi.
 
Hii ukiitafakari unaweza kulia machozi, wanasiasa wemeitafsiri vibaya na kuwakandamiza wanyonge. I wish WaTZ wangeweka kipaumbele kwenye elimu kwanza ili wayafahamu hila hizi kwa wingi wao. Ila ndiyo hivyo tena...
 
Wanasiasa uchwara wanapenda kutumianeno uzalendo kama kichaka cha kuficha uovu wao.Hakika moto wa milele uwatafune na kizazi cha nne.
 
Kivuli cha neno UZALENDO kinaangazia zaidi watu masikini, huku kikiwapa watawala fursa ya kujineemesha.

Madaktari, Walimu na watumishi wengine wa umma na sekta binafsi mfano wakulima wakibebeshwa msalaba wa uzaledo.

Hakuna mtawala anayeshiriki ktk kuubeba msalaba UZALENDO. Fikra na AKILI zao zimelenga kutufanya tusitoke shimoni, tukose afya ya mwili na akili ili mambo yao yawe sawa.

NI Mbunge gani angepewa hata kama ni milioni 2 kwa mwezi angekaa pale!!.Tunapo hamasisha uzalendo kwa pamoja tujali maslahi ya kila nafsi.
Bora hata wewe ulifanikiwa kuliona hili mapema ndugu yangu. Mimi nilichelewa kulifahamu hili nikajikuta ninapoteza muda wangu mwiiiingi katika kivuli cha uzalendo kwa kudanganywa na wanasiasa.
 
Hakika, ifike wakati WaTZ waweke kipaumbele kwenye elimu kwanza badala ya kuweka kwenye mambo ya kipuuzi, ili wafahamu hila hizi kwa wingi wao. Ila ndiyo hivyo tena...
Wakiwapa elimu bora mtawasumbua ndio maana hawataki kuwapa.
 
Wanasiasa uchwara wanapenda kutumianeno uzalendo kama kichaka cha kuficha uovu wao.Hakika moto wa milele uwatafune na kizazi cha nne.
Mimi pia ni mhanga wa neno Uzalendo. Nilifikiri kuwa hii nchi pia ni yangu kumbe ina wenyewe.
 
Kama waazilishi ni watawala kwanini wao sio wazalendo au waadilifu?
Viongozi wa kisiasa wa ccm
Bunge
Ma jaji
 
Back
Top Bottom