yutong
JF-Expert Member
- Apr 15, 2011
- 1,601
- 338
katika kipindi hiki kigumu ambambo CCM imekuwa na wakati mgumu na hasa kutokana na mwenyekiti wa chama hicho kuwa na uwezo mdogo wa kukiongoza chama hicho lakini nashangaa sana kuona waasisi wa chama hicho kama vile Mzee Malechela, Mzee Mwinyi, Salim Ahmed Salim, Warioba, cleopa Msuya wapo kimya kabisa pamoja na CCM kuwa na wakati mgumu. Hii inanifanya mimi niamini kwamba ndani ya CCM kwenyewe wazee wengi hawajaridhishwa na utendaji wa JK ambaye sasa amewatenga wazee na kujifanya anawakumbatia vijana. Hii ndo maana wazee wameamua kukaa kimya na kumwachia zigo hili ambalo limemuelemea.
Katika kipindi chote kilichopita hatukuwahi kushuhudia CCM kuboronga kwa kiasi kikubwa namna hii. Hii pia inanipa wasiwasi kwamba mwenyekiti wachama hicho ameshindwa kukiongoza chama na serikali.
hebu tujiulize ndani ya CCM hakuna watu wenye uwezo zaidi ya JK? na kama wapo inamaana hawampi ushauri? na kama wanampa je inamaana anapuuzia? na kama haya yote yanatokea na wazee wenyebusara wako kimya hii inaleta taswira gani? Haya kazi inabaki kwetu sisi wananchi kuamua. Hebu toeni maoni yenu
Katika kipindi chote kilichopita hatukuwahi kushuhudia CCM kuboronga kwa kiasi kikubwa namna hii. Hii pia inanipa wasiwasi kwamba mwenyekiti wachama hicho ameshindwa kukiongoza chama na serikali.
hebu tujiulize ndani ya CCM hakuna watu wenye uwezo zaidi ya JK? na kama wapo inamaana hawampi ushauri? na kama wanampa je inamaana anapuuzia? na kama haya yote yanatokea na wazee wenyebusara wako kimya hii inaleta taswira gani? Haya kazi inabaki kwetu sisi wananchi kuamua. Hebu toeni maoni yenu