Yona F. Maro
R I P
- Nov 2, 2006
- 4,201
- 255
MWANDISHI wa Habari, ni mtu muhimu kwa taifa na jamii kwa ujumla,
kutokana na mchango wake mkubwa katika kuelimisha, kuasa, kuonya na
kuhabarisha matukio mbalimbali, yanayotokea katika dunia, lakini pia
huweza kuwa mchonganishi na mfitini, iwapo atashindwa kuzingatia
maadili ya kazi yake.
Hapa nchini, kumekuwa na habari nyingi zinazoandikiwa kwa lengo la
uvurugaji na uchochezi, kutoka jamii moja hadi nyingine, au kutokana
na dini moja hadi nyingine, hata chama kimoja na kingine hali
inayowafanya wasomaji wa habari hizo kudhani habari zilizoandikwa ni
kweli na kuanzisha uhasama bila ya sababu za msingi.
Magazeti mengi, waandishi wao wameshindwa kutumia busara na hekima na
kuzingatia maadili ya uandikaji wa habari, kwa kuripoti habari ambazo
kwa muonekano wa jamii, ni zenye kuchochea uhasama, ingawa waandishi
wenyewe hawalioni hili.
Vile vile, magazeti nayo kutokana na kujua uuzwaji wa gazeti siku hizi
ni ushindani, wamekuwa wakikubali kuripoti habari hata ambazo huwa
hawana uhakika nazo, ili mradi wanajua mapato kutokana na mauzo yake
kwa siku hiyo yatakuwa makubwa.
Tumeshuhudia magazeti yakiandika, kwa mfano habari za Mwenyekiti wa
IPP, katika hali ya kuonyesha chuki dhidi ya watanzania wenye Asili ya
Asia na kuwasomesha wasomaji, wasiojua chochote kuhusu sakala hilo au
hata kutokuwa na chochote katika watu hao wawili !
Mwandishi anatakiwa kuandika habari bila kushinikizwa, wala woga,
ilimradi habari iwe ya kweli na yenye uhakika, lakini kupotosha kitu
ambacho wengi wa wananchi walielewa ni nini kilichotokea, ilijenga
kudhalilisha taaluma hii, ambayo ina mchango mkubwa kwa jamii na taifa
kwa ujumla.
Baadhi ya waandishi wamekuwa wakiandika ndani ya habari zao, majina
kama, uchochezi , papa , Nyangumi , Fisadi na mengineyo ambayo
'kamusi' za akili zao ziliwatuma kutumia hivyo, lakini bila wao
wenyewe kujua wanajenga uadui na chuki kati ya wahusika na vyombo
hivyo, kwa vile mtu yeyote, apewapo sifa mbaya, hujisikia unyonge na
kujenga chuki.
Pia, waandishi wengine kwa kutaka kuuza magazeti yao, wamekuwa
wakitaka tusema sifa kwa kuzikuza habari, kuonekana jambo la ajabu kwa
kutafutia vichwa vya habari, wanavyohisi kusomeka na kukubalika kwa
haraka na mnunuzi wa habari, bila kujua wanakwenda kinyume.
Kwa kutambua waandishi wana wajibu mkubwa kwa jamii katika kutoa
habari na kuelimisha umma, hawana budi kuzingatia maadili na haki
zitakiwavyo katika kuandika habari, kwa kuzingatia kuwa, habari hizo
husomwa na watu mbalimbali, iwapo zitakuwa zenye malengo mabaya, ni
rahisi kuhamasisha watu wanaoitilafiana katika habari hizo, kuweza
kudhihiri chuki zao bayana.
Wengi watakubaliana nami kuwa, hata mgogoro wa Reginald Mengi na
Rostam pamoja na wengine umekuzwa sana na vyombo vya habari kwa
kuripoti maelezo toka pande zote zenye malumbano, zenye kejeli na
tuhuma nzito, jambo linalopelekea wawili wanaogombana kuendeleza chuki
na mfarakano baina yao.
Kutokana na kuidhalilisha fani hii, kwa kuandika habari kwa mtindo wa
bora linunuliwe, ndio maana jamii huwa wanaowagopa waandishi, kiasi
cha kuwaita 'wambeya' na 'wadaku', kwa nini? Kwa sababu, kwa sikiu za
hivi karibuni habari nyingi huwa hazina malengo yoyote, zaidi ya
kupandikiza chuki na kupotosha umma. Turejeshe hadhi ya taaluma kwa
kuandika habari za kweli, kamilifu na zisizo na upendeleo.
kutokana na mchango wake mkubwa katika kuelimisha, kuasa, kuonya na
kuhabarisha matukio mbalimbali, yanayotokea katika dunia, lakini pia
huweza kuwa mchonganishi na mfitini, iwapo atashindwa kuzingatia
maadili ya kazi yake.
Hapa nchini, kumekuwa na habari nyingi zinazoandikiwa kwa lengo la
uvurugaji na uchochezi, kutoka jamii moja hadi nyingine, au kutokana
na dini moja hadi nyingine, hata chama kimoja na kingine hali
inayowafanya wasomaji wa habari hizo kudhani habari zilizoandikwa ni
kweli na kuanzisha uhasama bila ya sababu za msingi.
Magazeti mengi, waandishi wao wameshindwa kutumia busara na hekima na
kuzingatia maadili ya uandikaji wa habari, kwa kuripoti habari ambazo
kwa muonekano wa jamii, ni zenye kuchochea uhasama, ingawa waandishi
wenyewe hawalioni hili.
Vile vile, magazeti nayo kutokana na kujua uuzwaji wa gazeti siku hizi
ni ushindani, wamekuwa wakikubali kuripoti habari hata ambazo huwa
hawana uhakika nazo, ili mradi wanajua mapato kutokana na mauzo yake
kwa siku hiyo yatakuwa makubwa.
Tumeshuhudia magazeti yakiandika, kwa mfano habari za Mwenyekiti wa
IPP, katika hali ya kuonyesha chuki dhidi ya watanzania wenye Asili ya
Asia na kuwasomesha wasomaji, wasiojua chochote kuhusu sakala hilo au
hata kutokuwa na chochote katika watu hao wawili !
Mwandishi anatakiwa kuandika habari bila kushinikizwa, wala woga,
ilimradi habari iwe ya kweli na yenye uhakika, lakini kupotosha kitu
ambacho wengi wa wananchi walielewa ni nini kilichotokea, ilijenga
kudhalilisha taaluma hii, ambayo ina mchango mkubwa kwa jamii na taifa
kwa ujumla.
Baadhi ya waandishi wamekuwa wakiandika ndani ya habari zao, majina
kama, uchochezi , papa , Nyangumi , Fisadi na mengineyo ambayo
'kamusi' za akili zao ziliwatuma kutumia hivyo, lakini bila wao
wenyewe kujua wanajenga uadui na chuki kati ya wahusika na vyombo
hivyo, kwa vile mtu yeyote, apewapo sifa mbaya, hujisikia unyonge na
kujenga chuki.
Pia, waandishi wengine kwa kutaka kuuza magazeti yao, wamekuwa
wakitaka tusema sifa kwa kuzikuza habari, kuonekana jambo la ajabu kwa
kutafutia vichwa vya habari, wanavyohisi kusomeka na kukubalika kwa
haraka na mnunuzi wa habari, bila kujua wanakwenda kinyume.
Kwa kutambua waandishi wana wajibu mkubwa kwa jamii katika kutoa
habari na kuelimisha umma, hawana budi kuzingatia maadili na haki
zitakiwavyo katika kuandika habari, kwa kuzingatia kuwa, habari hizo
husomwa na watu mbalimbali, iwapo zitakuwa zenye malengo mabaya, ni
rahisi kuhamasisha watu wanaoitilafiana katika habari hizo, kuweza
kudhihiri chuki zao bayana.
Wengi watakubaliana nami kuwa, hata mgogoro wa Reginald Mengi na
Rostam pamoja na wengine umekuzwa sana na vyombo vya habari kwa
kuripoti maelezo toka pande zote zenye malumbano, zenye kejeli na
tuhuma nzito, jambo linalopelekea wawili wanaogombana kuendeleza chuki
na mfarakano baina yao.
Kutokana na kuidhalilisha fani hii, kwa kuandika habari kwa mtindo wa
bora linunuliwe, ndio maana jamii huwa wanaowagopa waandishi, kiasi
cha kuwaita 'wambeya' na 'wadaku', kwa nini? Kwa sababu, kwa sikiu za
hivi karibuni habari nyingi huwa hazina malengo yoyote, zaidi ya
kupandikiza chuki na kupotosha umma. Turejeshe hadhi ya taaluma kwa
kuandika habari za kweli, kamilifu na zisizo na upendeleo.