Waafrika walioishangaza dunia

MSEZA MKULU

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2011
Posts
3,768
Reaction score
5,635
Hawa ni baadhi ya waafrika/watuweusi waliobadili fikra zao na kuishanganza dunia.

1. Dr Phillip Emeaguali

Alizaliwa nigeria. Anajulikana duniani kama "Father of supercomputer" au "Father of internet" au "The Bill Gate of Africa". Akiwa na miaka 14 alisitisha shule kutokana na vita vya BIAFRA, baada ya vita alimalizia shule kwa kujisomea mwenyewe, alikuwa na uwezo wa kusolve complex mathematics kwa kutumia kichwa tu. Ameshinda nobel prize na tuzo lukuki huko marekani.

2: Dr. Isaiah M. Blankson

Huwezi kuizungumzia NASA Bila kumtaja Huyu MGHANA. Ni miongoni mwa SCIENTISTS waliobokea 12 wa nasa kati ya maengineer. Anajua Kirusi kwa sababu hata warusi humtumia mara mojamoja wanapohitaji ushauri wa kuitaalam.
Aliwahi kupewa tuzo ya heshima 2006 kutoka kwa raisi wa marekani na tuzo nyingine kibao. High speed Missles na ndege za kivita na vitu vingi vinavyokwenda mwezini. Anaanzisha idara za AERONAUTICS katika vyuo vya africa.

3.RACHID YAZAMI

Mmoroco, na baadae kupewa uraia wa Ufaransa. Alivumbua LITHIUM ION Battery. Betry hizi ndio tunatumia leo KWenye Simu, Computer, Camera, Na karibu vifaa vyote vya electronic. Na zinatumika dunia nzima.

4.Kwatsi Alibaruho

Mganda huyu, Ndio mtu mweusi wa kwanza kuwa Director NASA. Ni Fright Director wa NASA. Utajiuliza kafanya nini wakaachawa watu wote apewe cheo hicho mtu huyu katika taasisi yenye heshima yake duniani kote.

5.Prof. Dr. Francis A. S. Torya Matambalya
Huyu ni Msomi Kutoka TANZANIA Mji wa Musoma. Duniani ukizungumzia wasomi na watu maarufu wa Africa, anatambuliwa kama Msomi Nguli wa Mambo ya Biashara za Kimataifa. Na yupo kwenye list ya wanasansi, wasomi na wavumbuzi wakubwa africa.

6. Madam C J WALKER

Mwanamke MILLIONAIRE wa kwanza Marekani. Mjasiriamali na mvumbuzi wa mambo ya urembo. Ndie aliyevumbua shampoo, na vitu vingine vingi vya kuzifanya nywele mbovummbovu kuwa raini na nzuri. Na system zake nyingi za urembo, yupo katika kumbukumbu ya watu maarufu marekani.

7: Jan Ernst Matzeliger

Alivumbua mashine ya kutengeneza viatu. Mashine hiyo ilileta mapinduzi duniani katika soko viatu na mwenendo wake.

8. George Washington Carver

Mchango wake na uvumbuzi wake katika mambo ya kilimo yalipindua mwenendo wa kilimo dunia nzima. Aligundua na kudocument matumizi zaidi ya Mia moja ya karanga ambayo na mavumbuzi kibao katika sekta ya kilimo.

9. DR. ANSWAR HILONGA


2015 mtanzania huyu kijana alijishindia tuzo nchini afrika kusini iliyohusisha bara zima afrika kwa kuwa Best african Engineering Innovator. Alivumbua Kifaa maalum cha kiteknolojia kisicho na ghalama kinachoweza kuchuja maji yasiyosafi na kufaa kwa kunywa. Kama kifaa au uvumbuzi huu ukitumika utaokoa waafrica na watu wengi vijijini na magonjwa waliyo katika maji machafu na hata kuokoa vifo africa na duniani kwa ujumla.

10: Elijah McCoy (1843-1929)

Huyu mzee katika maisha yake alivumbua vitu zaidi ya 50. Kikubwa mabacho kilibadili taswira kabisa ya Industry ya treni duniani duniani kote, ni kifaa maalumu kilichoweza kuzuia msuguano wa vyuma engine ya katika treni (automatic lbricating cup).

11: Verone Mankou

Kijana wa Congo Brazaville aliyevumbua smartphone yake mwenyewe 2012 huku akipata msaada kutoka kwa serikali na mabenki kukamilisha mradi wake. Baadae ilienda kuwa assempled China na kuuzwa kwa zaidi ya $116. Inaitwa ELIKIA.

Unaweza kusema chochote cha kujenga au kumuongeza yoyote hata kama ni vijana wetu mtaani.
 
Kwanini wengi wao wamekimbilia huko Ulaya na Marekani na hawakubaki ili kuendeleza nchi zao au kushare hiyo knowledge yao na wazawa wa Nchini mwao?
 
this has inspired me a lot, i can see bado Ni mweupe hamna nilichokifanya, yani daah!
 
Aisee,Francis Matambalya yumo? Namkubali huyu mzee na Nimewahi kumfanyia kazi zake siku za nyuma, ni kichwa sana ila mjanjamjanja sana.
 
 
Hongera zao natamani apatikane mtanzania mwingine wa kuvumbua upimaji wa tezi dume kwa gharama nafuu na usihushishe mtindo kama wa kampeni hizi zInazoendelea.
 
Kwa nini hao wote wamekimbilia Marekani?..au je ni ule usemi wa kuwa Mwaflika bila Mzungu si chochote?... nami nilitegemea wabaki Africa kuliendeleza bara letu.. Labda kama walienda America kwa kuibwa..maana nasikia siku hizi mwafrika ukionekana tu una kipaji cha ajabu ajabu unabebwa na kwenda kufungiwa uwafanyie Assignment.
 
mleta mada hapo uliposema "waliobadili fikra zao" naomba ufafanuzi...

kwani waafrika fikra zetu zipoje mpaka tuzibadilishe ndo tuweze kufanya mambo makubwa na yenye michango ktk jamii zetu na dunia? Naomba jibu
 
Kwanini wengi wao wamekimbilia huko Ulaya na Marekani na hawakubaki ili kuendeleza nchi zao au kushare hiyo knowledge yao na wazawa wa Nchini mwao?

Kwa sababu hapa Africa hata uvumbue kitu gani hauwezi kuwa appreciated sana sana kama ni hapa Tanzania watakuuliza ww ni ccm au ukawa halafu wakupigwe zengwe. Si unaona Mbwana Sammata alivyowahishwa Lumumba kupiga picha na maccm. Africa ni shida
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…