Wa enzi hizo mnayakumbuka haya?

Wa enzi hizo mnayakumbuka haya?

Miwatamu

JF-Expert Member
Joined
Oct 2, 2012
Posts
1,450
Reaction score
490
Kwetu ss tuliobahatika kuwepo miaka ya 80 tulikutana na mambo mengi sana ambayo ukiyakumbuka kwa sasa unaishia kucheka.

Zama zile ukikutwa umenyoa denge lazima uwekwe ndani eti umenyoa mnyoo wa kipolisi!

Ukionekana na kitambaa chenye rangi za bendera ya taifa hiyo kesi ingefika hata ikulu!

Ukivaa cadet unaambiwa umevaa kitambaa cha polisi na lazima uvuliwe! Utakwendaje kwenu, haiwahusu.

Ukionekana umevaa shati lenye lebo au nyota ama V unaambiwa hivi ni vyeo vya askari!!!

Je, haya yangekuwepo leo c vjana wetu wangeishia lupango?! Ama kweli tumetoka mbali.
 
Ni kweli mkuu hata mm mambo yamekuwa yakiniumiza kichwa sana. Nashindwa kueleza dhana hi yo ni kwamba viongozi wetu hawajiamini au inakuwaje? Coz hata Leo baadhi ya sheria hizo bado zipo.
 
Miwatamu umesahau, ukiwa umebeba mfuko wa karatasi ambao unaonekana ndani una kitu mgambo anakukamata kutaka kujua umebeba nn na ukikutwa na sukari au mchele utawaeleza umeutoa wapi
 
Hii inaonyesha tumepigia hatua kimaendeleo hata kama ni kidogo lakini tofauti ipo
 
Mambo ya utandawazi yamesaidia watu wameelimika hizo zilikuwa sheria za kunyanyasana,ingawa viongozi engine uelewa mdogo
 
Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi ndie aliyeondoa mambo mengi ya unyanyasaji,aliporuhusu bidhaa kuuzwa madukani kutoka nje ya nchi,na za viwandani.
 
msisahau pia KODI YA KICHWA ambayo kabla ya kufutwa walikuwa wanalipa watu wzm wote, afu ikarekebishwa walipe wanaume tu!
 
msisahau pia KODI YA KICHWA ambayo kabla ya kufutwa walikuwa wanalipa watu wzm wote, afu ikarekebishwa walipe wanaume tu!

Watu walikuwa wanakimbia makazi yao kutokana na hiyo kodi,ulikuwa unyanyasaji hasa.
 
msisahau pia KODI YA KICHWA
ambayo kabla ya kufutwa walikuwa wanalipa watu wzm wote, afu
ikarekebishwa walipe wanaume tu!

Hiyo kodi mbona unaendelea kulipa hadi leo? Hivi sasa ulipa mwenyewe softly.
 
Na kukamatwa kwa kosa la uzembe na uzururaji[\b]
 
Hiyo kodi mbona unaendelea kulipa hadi leo? Hivi sasa ulipa mwenyewe softly.

Vipi kuhusu mchango wa mafuta ya mwenge? Nilishangaa sana kwamba kwa wakati huu vijijini wanalazimishwa kuchangia hii kitu. Yaani watendaji wamejipa mamlaka makubwa kiasi cha kuwacharaza bakora wale wanaokaidi hii michango ya mafuta ya mwenge!! Na sidhani kama wanapewa risiti. Na hata kama wanapewa risiti. Hii michango ipo ktk sheria za nchi hii kweli?!
 
nakumbuka enzi hizo rais akitembelea wilaya ama mkoa fulani,wanafunzi wa shule za msingi na sekondari tulikuwa tunajipanga barabarani kumwimbia nyimbo za kusifu CCM!Wafanyabiara walilazimishwa kufunga biashara zao kwa ajili ya kwenda kumpokea na kumsikiliza rais.
 
Wakati ule baiskeli inalipiwa kodi na risiti zinabandikwa pale kwenye dobo,lakini kodi zote zipo mpaka leo na zimeongezeka kwa 100% kila kitu sahvi komeunganishwa na kodi tena kubwakubwa
 
Halafu wakati huo ilikuwa sio rahisi kukuta mwanamke anakitambi. Ukikuta anatumbo kubwa basi huyo ana mimba lakini sasa hivi ni vigumu kutofautisha mwenye mimba na asiye na mimba. Yaani sasa hivi wanawake na hata wasichana wadogo ndio wanaongoza kwa kuwa na vitambi kuliko wanaume, sijui nini kimewakuta?
 
Halafu wakati huo ilikuwa sio rahisi kukuta mwanamke anakitambi. Ukikuta anatumbo kubwa basi huyo ana mimba lakini sasa hivi ni vigumu kutofautisha mwenye mimba na asiye na mimba. Yaani sasa hivi wanawake na hata wasichana wadogo ndio wanaongoza kwa kuwa na vitambi kuliko wanaume, sijui nini kimewakuta?

Chezea chipsi kuku wewe! Hapa factor kubwa ni vyakula wanavyokula siku hizi, vina mafuta mabaya kwa kiasi kikubwa kaka.
 
Nakumbuka zamani kuoa au kuolewa ilikuwa ni fashion tena ni heshima kubwa, ila siku hizi ni kuanua ngoma juani tu!
 
Halafu wakati huo ilikuwa sio rahisi kukuta mwanamke anakitambi. Ukikuta anatumbo kubwa basi huyo ana mimba lakini sasa hivi ni vigumu kutofautisha mwenye mimba na asiye na mimba. Yaani sasa hivi wanawake na hata wasichana wadogo ndio wanaongoza kwa kuwa na vitambi kuliko wanaume, sijui nini kimewakuta?

Ni kweli kabisa bwana, na pia siku hizo huwezi kumkuta mwanamke kavaa suruali. Mtaa mzima watamshangaa na kumwona malaya
 
Back
Top Bottom