Wissman
JF-Expert Member
- Dec 12, 2014
- 1,034
- 1,319
Katika hali ya kushangaza migomo mbalimbali huwa inaendeshwa na wanafunzi wa vyuo mbalimbali hapa nchini (kama ilivyo sasa) lakini kwa hali ya ajabu na kustaajabisha kwa miaka mingi hapajakuwa na mgomo wa wanafunzi wa chuo kikuu Mzumbe. Nini siri ya wasomi wa chuo hicho? Wanawezaje kukabiliana na changamoto ambazo wasomi wa vyuo vikuu vingine Tanzania wameshindwa kuvumilia? Wao wanawezaje kujikimu kama fedha hazijafika kwa vyuo vyote? Kama wana mbinu ni ipi? Ili vyuo vingine navyo viige?