EJM_
JF-Expert Member
- Jul 8, 2011
- 3,836
- 2,108
Siku za hivi karibuni kumekuwa na kile wanachokiita uhuru wa vyombo vya habari hapa nchini. Hali hii imepelekea kuanza kukosekana kwa maana halisi ya vyombo vya habari na jukumu lake kubwa kwa Taifa. Moja ya Radio ambazo mi huwa nasikiliza sana ni Clouds FM (Kwakuwa ndio radio pekee inayosikika vyema huku kwetu) lakini katika siku za hivi karibuni naanza kuhisi kama imeanza kukosa muelekeo hasa linapokuja suala la kutofungamana na upande wowote.
Mfano mmoja mzuri ni matukio mawili makubwa yaliyotokea siku za hivi karibuni;
Katika hili nahisi kuna umuhimu wa kuangaliwa vizuri kwa matumizi ya vyombo hivi vya habari, tumeshuhudia mara kadhaa sasa zikianza kutumwa messeji za kuwatukana hawa watangazaji. Hii ni picha ya namna gani chuki na uhasama unajengeka kutokana na yale wanayoyasema kupitia radio au vyombo vyao mbalimbali vya habari. Tukumbuke mauaji ya Rwanda, vyombo vya habari vilichangia kwa kiasi kikubwa sana, tusipoangalia na sisi tunaelekea huko.
Kama vyombo vya habari vifanye kazi zao na sio kuwa mashabiki kwani hii ni hatari kwa amani na maendeleo ya Taifa letu. Nikiona habari fulani kwenye Uhuru na Mzalendo au Tanzania Daima, TBC na zile zenye muelekeo huo sishangai sana kwasababu watu wote wanajua hivi ni vyombo vya propaganda lakini sio wale wanaojiita hawafungamani na upande wowote huku wakifanya tofauti.
Ni mtazamo wangu tu.............
Mfano mmoja mzuri ni matukio mawili makubwa yaliyotokea siku za hivi karibuni;
- Mgogoro wa gesi ya Mtwara; Mi nilifikiri kazi kubwa ya chombo cha habari ingekuwa kuziweka pamoja fikra za pande zote na kuwaleta wataalam mbalimbali wenye mawazo tofauti ili kujenga picha ya balanced news kuliko kufanya kampeni ya kipuuzi kama waliyokuwa wanaifanya Clouds FM. Sikuwahi kusikia hata siku moja hao Clouds wakiwauliza watu wa Mtwara ni hasa walikuwa wanakitaka, mwisho wakaanza kutangaza Mtwara hawataki gesi ije Dar es salaam, je ni kweli hawataki gesi ije Dar es salaam?
- Suala la Katiba; Mimi naamini kwamba ni kweli kila raia wa Tanzania ana uhuru wa kutoa maoni yake hasa kwenye suala muhimu kama la katiba, lakini ni lazima uangalie ni wapi unatoa hayo maoni yako, kwa namna gani unayatoa na kwa watu gani. Unapotoa maoni kwenye radio tena kwa kuwakashifu wanaotoa maoni tofauti na yako kama anavyofanya kaka yangu Kibonde mara nyingi sio tu kwamba nina wasiwasi kama maadili yanaruhusu bali pia yanatengeneza chuki zisizokuwa na msingi kwa wasikilizaji.
Katika hili nahisi kuna umuhimu wa kuangaliwa vizuri kwa matumizi ya vyombo hivi vya habari, tumeshuhudia mara kadhaa sasa zikianza kutumwa messeji za kuwatukana hawa watangazaji. Hii ni picha ya namna gani chuki na uhasama unajengeka kutokana na yale wanayoyasema kupitia radio au vyombo vyao mbalimbali vya habari. Tukumbuke mauaji ya Rwanda, vyombo vya habari vilichangia kwa kiasi kikubwa sana, tusipoangalia na sisi tunaelekea huko.
Kama vyombo vya habari vifanye kazi zao na sio kuwa mashabiki kwani hii ni hatari kwa amani na maendeleo ya Taifa letu. Nikiona habari fulani kwenye Uhuru na Mzalendo au Tanzania Daima, TBC na zile zenye muelekeo huo sishangai sana kwasababu watu wote wanajua hivi ni vyombo vya propaganda lakini sio wale wanaojiita hawafungamani na upande wowote huku wakifanya tofauti.
Ni mtazamo wangu tu.............