Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,437
- 5,235
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imewahakikishia viongozi wa vyama vya siasa kuwa kutakuwa na uwanja sawa kwa vyama vyote wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka huu kwa kuhakikisha kila chama kinafanya mikutano yake kwa mujibu wa ratiba.
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi na Vyama vya Siasa kuhusu uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025. Kikao hicho cha siku moja kilifanyika leo Julai 27, 2025 jijini Dodoma na kushirikisha vyama vyote vyenye usajili kamili.
Mwambegele akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi na Vyama vya Siasa kuhusu uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025. Kikao hicho cha siku moja kilifanyika leo Julai 27, 2025 jijini Dodoma na kushirikisha vyama vyote vyenye usajili kamili.
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani, Jacobs Mwambegele ameyasema hayo leo tarehe 27 Julai, 2025 wakati akifungua mkutano wa Tume na Viongozi wa Vyama vya Siasa jijini Dodoma.
"Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, inawahakikishia kuwepo kwa uwanja sawa kwa vyama vyote wakati wa kampeni kwa kuhakikisha kila chama kitafanya mikutano yake kwa mujibu wa ratiba itakayokuwa imepitishwa na Kamati ya Ratiba Ngazi ya Taifa inayoratibu ratiba ya kampeni ya wagombea wa Kiti cha Rais na Makamu wa Rais, kamati ya jimbo inayoratibu ratiba ya wagombea wa ubunge na kamati ya kata inayoratibu ratiba ya wagombea wa udiwani,” amesema Jaji Mwambegele
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani Jacobs Mwambegele akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi na Vyama vya Siasa kuhusu uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025. Kikao hicho cha siku moja kilifanyika leo Julai 27, 2025 jijini Dodoma na kushirikisha vyama vyote vyenye usajili kamili.
Mwambegele akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi na Vyama vya Siasa kuhusu uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025. Kikao hicho cha siku moja kilifanyika leo Julai 27, 2025 jijini Dodoma na kushirikisha vyama vyote vyenye usajili kamili.
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufani, Jacobs Mwambegele ameyasema hayo leo tarehe 27 Julai, 2025 wakati akifungua mkutano wa Tume na Viongozi wa Vyama vya Siasa jijini Dodoma.
"Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, inawahakikishia kuwepo kwa uwanja sawa kwa vyama vyote wakati wa kampeni kwa kuhakikisha kila chama kitafanya mikutano yake kwa mujibu wa ratiba itakayokuwa imepitishwa na Kamati ya Ratiba Ngazi ya Taifa inayoratibu ratiba ya kampeni ya wagombea wa Kiti cha Rais na Makamu wa Rais, kamati ya jimbo inayoratibu ratiba ya wagombea wa ubunge na kamati ya kata inayoratibu ratiba ya wagombea wa udiwani,” amesema Jaji Mwambegele