Vyakula vya Ajabu kutoka kwa Jose Mla Vichwa

Vyakula vya Ajabu kutoka kwa Jose Mla Vichwa

Damaso

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2018
Posts
6,132
Reaction score
10,514
Kwa muda mrefu sasa, jina la Jose Mla Vichwa limekuwa gumzo mitaani, mitandaoni na hata meza za chai za ofisi nyingi hapa nchini. Ni mtu anayeonekana tofauti, mtu mwenye hamu ya kugusa, kuonja na kula vyakula ambavyo Watanzania wengi hawaitaji hata kuvisikia.
images (80).jpeg

Kicheche, kenge, panya, chatu – kwa Jose hivi ni kama nyama ya kawaida ya ng'ombe, mbuzi au kuku. Huu ni upande wake wa kipekee, ambao mara nyingi huacha mashabiki wake wakibaki na mshangao, huku wengine wakimuona kama mtu wa hatari anayejaribu kutikisa misingi ya utamaduni wa chakula cha Kitanzania na Kiafrika.
images (79).jpeg

Lakini je, safari hii Jose anaelekea mbali zaidi ya utamaduni na kuingia kwenye eneo hatarishi la maisha yake?
images (81).jpeg

Wataalamu wa afya wanabainisha wazi kuwa si kila mnyama anayekula nyama unaweza pia kumla wewe. Kuna wanyama wenye sumu kali sana, ambao ukijaribu kugeuza kitoweo, basi kitakuwa ndio tiketi yako ya moja kwa moja kwenda kaburini.
channels4_profile.jpg

Moja ya mifano hai ni samaki maarufu Pufferfish (Fugu), anayejulikana sana duniani. Ni chakula cha kifahari kinachohitaji mpishi mtaalamu mwenye leseni maalumu. Kosa dogo tu katika maandalizi yake, na nyama ya samaki huyu hugeuka sumu kali sana. Hata Jose mwenye tumbo la chuma asithubutu kupima hatari hii.
images (82).jpeg

Kisha kuna Blue-ringed Octopus, kapweza kadogo kwa umbo lakini kajamaa kana sumu kali inayoweza kuua mtu mzima ndani ya dakika chache. Wakati watanzania wengi tunafurahia mchuzi wa pweza, na ubora wake katika kuhimarisha nguvu za kiume, Kaka Jose asije akajikuta amechanganya bakuli na kachori zako utajikuta kwenye wakati mgumu sana.
images (83).jpeg

Hali ni hiyo hiyo kwa Cane Toad, chura mkubwa ambaye ngozi yake inatoa sumu ya aina ya bufotoxin. Wengine wamejaribu kumla na ugali maharage lakini matokeo yake mara nyingi ni vifo visivyotarajiwa.
images (86).jpeg

Kwa mtindo huu wa kula vyakula visivyo vya kawaida, Jose anachochea mjadala mpana kuhusu usalama wa chakula na utamaduni wa Tanzania. Je, tunaposhabikia upekee wake, tunasahau kuwa kuna mpaka kati ya kula chakula cha kienyeji na kula sumu kwa makusudi?
images (79).jpeg

Hata wageni ambao unawapatia mwaliko mara kadhaa, kuwa makini maana mgeni anaweza kutamani kuonja nyama ya Kuku Makucha, kumbe ana allergy, kinamlamba vizuri kabsa. Wakija wageni wako wape tahadhari mapema na kama inawezekana wape chakula cha kawaida. Sio kila mtu umpatie nyama ya Kuku Makucha.
images (83).jpeg

Ila yote kwa yote Kaka Jose, endelea kuwa mbunifu, lakini kumbuka: hamu isije ikawa adui wa maisha.
 
Kwa muda mrefu sasa, jina la Jose Mla Vichwa limekuwa gumzo mitaani, mitandaoni na hata meza za chai za ofisi nyingi hapa nchini. Ni mtu anayeonekana tofauti, mtu mwenye hamu ya kugusa, kuonja na kula vyakula ambavyo Watanzania wengi hawaitaji hata kuvisikia.
View attachment 3460369
Kicheche, kenge, panya, chatu – kwa Jose hivi ni kama nyama ya kawaida ya ng'ombe, mbuzi au kuku. Huu ni upande wake wa kipekee, ambao mara nyingi huacha mashabiki wake wakibaki na mshangao, huku wengine wakimuona kama mtu wa hatari anayejaribu kutikisa misingi ya utamaduni wa chakula cha Kitanzania na Kiafrika.
View attachment 3460370
Lakini je, safari hii Jose anaelekea mbali zaidi ya utamaduni na kuingia kwenye eneo hatarishi la maisha yake?
View attachment 3460374
Wataalamu wa afya wanabainisha wazi kuwa si kila mnyama anayekula nyama unaweza pia kumla wewe. Kuna wanyama wenye sumu kali sana, ambao ukijaribu kugeuza kitoweo, basi kitakuwa ndio tiketi yako ya moja kwa moja kwenda kaburini.
View attachment 3460371
Moja ya mifano hai ni samaki maarufu Pufferfish (Fugu), anayejulikana sana duniani. Ni chakula cha kifahari kinachohitaji mpishi mtaalamu mwenye leseni maalumu. Kosa dogo tu katika maandalizi yake, na nyama ya samaki huyu hugeuka sumu kali sana. Hata Jose mwenye tumbo la chuma asithubutu kupima hatari hii.
View attachment 3460378
Kisha kuna Blue-ringed Octopus, kapweza kadogo kwa umbo lakini kajamaa kana sumu kali inayoweza kuua mtu mzima ndani ya dakika chache. Wakati watanzania wengi tunafurahia mchuzi wa pweza, na ubora wake katika kuhimarisha nguvu za kiume, Kaka Jose asije akajikuta amechanganya bakuli na kachori zako utajikuta kwenye wakati mgumu sana.
View attachment 3460379
Hali ni hiyo hiyo kwa Cane Toad, chura mkubwa ambaye ngozi yake inatoa sumu ya aina ya bufotoxin. Wengine wamejaribu kumla na ugali maharage lakini matokeo yake mara nyingi ni vifo visivyotarajiwa.
View attachment 3460381
Kwa mtindo huu wa kula vyakula visivyo vya kawaida, Jose anachochea mjadala mpana kuhusu usalama wa chakula na utamaduni wa Tanzania. Je, tunaposhabikia upekee wake, tunasahau kuwa kuna mpaka kati ya kula chakula cha kienyeji na kula sumu kwa makusudi?
View attachment 3460370
Hata wageni ambao unawapatia mwaliko mara kadhaa, kuwa makini maana mgeni anaweza kutamani kuonja nyama ya Kuku Makucha, kumbe ana allergy, kinamlamba vizuri kabsa. Wakija wageni wako wape tahadhari mapema na kama inawezekana wape chakula cha kawaida. Sio kila mtu umpatie nyama ya Kuku Makucha.
View attachment 3460379
Ila yote kwa yote Kaka Jose, endelea kuwa mbunifu, lakini kumbuka: hamu isije ikawa adui wa maisha.
Nilisoma nae ifm.... aliwahi kuwa MR IFM ....enzi hizo pia kina sanchoka wapoo pale wanasoma diploma
Madem walikuwa wana mkubali sana jose mla vichwaaa sanaaa asee
 
Nilisoma nae ifm.... aliwahi kuwa MR IFM ....enzi hizo pia kina sanchoka wapoo pale wanasoma diploma
Madem walikuwa wana mkubali sana jose mla vichwaaa sanaaa asee
Licha ya yote hayo sijui IFM sijui madem walimkubali. Je umeshakula kiapo cha utii kwa Kipenzi chetu cha dhati Imam Hussain ibn Ali AS mwamba mkombozi wa waislamu aliyeuwawa kikatili kuutetea kuulinda na kuupigania uislamu dhidi ya dhulma ukandamizaji unyanyasaji na uonevu kwenye jamii?

Screenshot_2025-07-07-20-16-29-71_40deb401b9ffe8e1df2f1cc5ba480b12~2.jpg


kimsboy adriz
 
Back
Top Bottom