dosama
JF-Expert Member
- Dec 25, 2010
- 912
- 957
Na Deogratius Temba, Tanzania Daima
PENGINE tunaweza kupingana, kukosoana na kutokukubaliana kuwa tatizo au sababu ya vurugu za Zanzibar zilizotokea wiki iliyopita ni udini au chuki za kiimani zilizoasisiwa na viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakati wa uchaguzi Mkuu mwaka 2010. Tuna kila sababu ya kuendelea kuwalaumu na kuwalaani wanasiasa waliotufikisha hapa.
Hali ya hewa imechafuka wao wamekaa pembeni! Hata kama Muungano utavunjika ni kwa uzembe wao. Haya ni matunda ya kutumia udini kujinufaisha kisiasa, walifanikiwa kuwagawa Watanzania kimakundi, ili wawatawale kirahisi.
Hii ilikuwa ni mbinu ya chama tawala kulikuza suala hili, wakilitumia kama mbinu ya kuua au kudhoofisha upinzani baada ya ukabila kushindwa.
Sababu nyingine ya CCM na viongozi wake kupandikiza mbegu ya udini ni kutaka kuvunja nguvu ya upinzani, baada ya kuona CHADEMA inakuja kwa kasi hasa baada ya CCM kujeruhiwa vibaya kwenye uchaguzi 2010.
Tutakumbuka kuwa agenda hii ilitumika sana kuwa CHADEMA ni chama cha Wakristo na hata tumeona kwenye uchaguzi mdogo wa Jimbo la Igunga mambo yalivyofanyika baada ya CCM kufanikiwa kukipaka matope CUF kwamba ni chama cha Kiislamu. Kwa sera yao ya udini, sasa wameamua kuhamishia majeshi yao CHADEMA baada ya kufanikiwa kuisarambatisha CUF.
Udini unatumiwa na CCM kama kielelezo kwamba serikali inasemwa na kusimangwa sana kuhusu ufisadi kisa Rais ni Mwislamu, hata sasa hivi kuna watu wanazusha eti Mkulo (Mustafa) alihujumiwa kisa ni Mwislamu.
Kwa kuwa CCM wameshindwa kutimiza ahadi zao kama Maisha Bora kwa kila Mtanzania, wameamua kutumia udini kama sera ya kulinda uzembe,ufisadi na maovu yao! Kiongozi Mwislamu akishindwa kutekeleza wajibu wake akishughulikiwa wanasema ni kwa sababu ni Mwislamu.
Agenda ya Muungano imeingizwa kwenye suala hili la udini, kuwa umetawaliwa na mfumo wa Kikristo, na Tanzania Bara imejaa Wakristo, na wanaichafua Zanzibar, kwa hiyo ukiua Muungano Ukristo utakosa nguvu Zanzibar.
Haya ni matunda ya kukua kwa mbegu ya udini iliyopandwa na watawala wetu mwaka 2010. Niliandika katika gazeti hili katika safu hii Januari 29, mwaka huu, niliona mbali na kutabiri hili kutokea Zanzibar kwa sababu nilishaona jinsi CCM na viongozi wake wakuu walivyoutumia mtaji wa udini.
Serikali inafikiri kuwa kuwagawa Wakristo na Waislamu, ikapandikiza chuki itafanikiwa kuwatawala daima! Amani ni muhimu!
Nchi za Afrika ya Magharibi zina Waislamu tena wenye imani kali kuliko Tanzania, Afrika ya Kaskazini na hata Bara la Asia kumekuwa na machafuko na vuguvugu la kudai mabadiliko kwa muda mrefu, lakini hata siku moja hawajawahi kuchomeana makanisa au nyumba za ibada.
Wananchi wa huko hawakubali kugawanywa kwa itikadi za kidini kama hapa kwetu, wanaungana, wanajenga hoja wanaamua kudai mabadiliko na kuuwajibisha uongozi.
Kila Mtanzania anajiuliza Zanzibar hawataki Muungano au hawataki Makanisa? Je, tatizo la Muungano ni Ukristo? Je, Ukristo ukiondoka tatizo la Muungano litamalizika?
Viongozi wetu wanachochea, wanachekelea na wanafikiri wameshinda.Watanzania waachwe wajadili,waelimishane, wakemeane kama Watanzania bila kujaili dini na kama hawautaki Muungano waseme waziwazi.
My concern
CCM ni wadini wakuu katika nchi hii
PENGINE tunaweza kupingana, kukosoana na kutokukubaliana kuwa tatizo au sababu ya vurugu za Zanzibar zilizotokea wiki iliyopita ni udini au chuki za kiimani zilizoasisiwa na viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakati wa uchaguzi Mkuu mwaka 2010. Tuna kila sababu ya kuendelea kuwalaumu na kuwalaani wanasiasa waliotufikisha hapa.
Hali ya hewa imechafuka wao wamekaa pembeni! Hata kama Muungano utavunjika ni kwa uzembe wao. Haya ni matunda ya kutumia udini kujinufaisha kisiasa, walifanikiwa kuwagawa Watanzania kimakundi, ili wawatawale kirahisi.
Hii ilikuwa ni mbinu ya chama tawala kulikuza suala hili, wakilitumia kama mbinu ya kuua au kudhoofisha upinzani baada ya ukabila kushindwa.
Sababu nyingine ya CCM na viongozi wake kupandikiza mbegu ya udini ni kutaka kuvunja nguvu ya upinzani, baada ya kuona CHADEMA inakuja kwa kasi hasa baada ya CCM kujeruhiwa vibaya kwenye uchaguzi 2010.
Tutakumbuka kuwa agenda hii ilitumika sana kuwa CHADEMA ni chama cha Wakristo na hata tumeona kwenye uchaguzi mdogo wa Jimbo la Igunga mambo yalivyofanyika baada ya CCM kufanikiwa kukipaka matope CUF kwamba ni chama cha Kiislamu. Kwa sera yao ya udini, sasa wameamua kuhamishia majeshi yao CHADEMA baada ya kufanikiwa kuisarambatisha CUF.
Udini unatumiwa na CCM kama kielelezo kwamba serikali inasemwa na kusimangwa sana kuhusu ufisadi kisa Rais ni Mwislamu, hata sasa hivi kuna watu wanazusha eti Mkulo (Mustafa) alihujumiwa kisa ni Mwislamu.
Kwa kuwa CCM wameshindwa kutimiza ahadi zao kama Maisha Bora kwa kila Mtanzania, wameamua kutumia udini kama sera ya kulinda uzembe,ufisadi na maovu yao! Kiongozi Mwislamu akishindwa kutekeleza wajibu wake akishughulikiwa wanasema ni kwa sababu ni Mwislamu.
Agenda ya Muungano imeingizwa kwenye suala hili la udini, kuwa umetawaliwa na mfumo wa Kikristo, na Tanzania Bara imejaa Wakristo, na wanaichafua Zanzibar, kwa hiyo ukiua Muungano Ukristo utakosa nguvu Zanzibar.
Haya ni matunda ya kukua kwa mbegu ya udini iliyopandwa na watawala wetu mwaka 2010. Niliandika katika gazeti hili katika safu hii Januari 29, mwaka huu, niliona mbali na kutabiri hili kutokea Zanzibar kwa sababu nilishaona jinsi CCM na viongozi wake wakuu walivyoutumia mtaji wa udini.
Serikali inafikiri kuwa kuwagawa Wakristo na Waislamu, ikapandikiza chuki itafanikiwa kuwatawala daima! Amani ni muhimu!
Nchi za Afrika ya Magharibi zina Waislamu tena wenye imani kali kuliko Tanzania, Afrika ya Kaskazini na hata Bara la Asia kumekuwa na machafuko na vuguvugu la kudai mabadiliko kwa muda mrefu, lakini hata siku moja hawajawahi kuchomeana makanisa au nyumba za ibada.
Wananchi wa huko hawakubali kugawanywa kwa itikadi za kidini kama hapa kwetu, wanaungana, wanajenga hoja wanaamua kudai mabadiliko na kuuwajibisha uongozi.
Kila Mtanzania anajiuliza Zanzibar hawataki Muungano au hawataki Makanisa? Je, tatizo la Muungano ni Ukristo? Je, Ukristo ukiondoka tatizo la Muungano litamalizika?
Viongozi wetu wanachochea, wanachekelea na wanafikiri wameshinda.Watanzania waachwe wajadili,waelimishane, wakemeane kama Watanzania bila kujaili dini na kama hawautaki Muungano waseme waziwazi.
My concern
CCM ni wadini wakuu katika nchi hii