utaifa ulioporwa ni utaifa gani?
baada ya kuporwa huo utaifa wako ulioasisiwa na wakoloni waliotwala Tanganyika, unajutia uhuru wako uliokukirimu utaifa mpya?
wewe huna utaifa?
unayo passport?
umeishawahi kusafiri nje na kuchanganyikana na watu wa mataifa mengine ukakosa kutambuliwa?
utaifa uliopachikwa na wakoloni wako ndio bora kuliko utaifa tunaouchukua vifuani mwetu na ulioasisiswa na watanzania wenzako wanamapinduzi?
Tuambie umuhimu wa huu Muungano na tusipokuwa kuwa na huo Muungano tunapoteza nini?
Unaona Tanganyika ni ukoloni? au utawala ndio ulikuwa wa kikoloni? kwani Zanzibaar kabla ya mapinduzi ilikuwa inaitwaje? mbona baada ya mapinduzi na hata muungano zanzibar imebaki kuitwa zanzibar? mataifa mangapi yamebadili majina ya utaifa wao eti kwa kisingizio kama hicho kuwa hayo majina yameletwa na wakoloni?
Mbona mipaka ya tanganika iliwekwa na wakoloni lakini baada ya uhuru hatujaibadilisha? au wewe kinachokukera ni jina tanganyika? Wewe unajua jina Tanzania mwalimu alilitoa wapi na lina maana gani?
Kama Muungano umekuwa ndio chanzo cha Zanzibar kudidimia kiuchumi kwanini waung'anga'anie the same kwa watanganyika.
Tueleze sababu za msingi za kwanini tuendelee kuamini kwenye Muungano huu wa vitu. maana ki uhalisia muungano huu sio wa watu bali wa vitu.
naombeni wale wote ambao wanasema muungano uvunjike wataje hasara mbili 2. mimi nimeshataja faida ninazoziona
1: elimu - wazanzibari wanfaidaka ktk elimu ya juu wakija kusoma tanganyika wankopeshwa sawa na wanalip[a ada sawa kama watanganyika na watanganyika wakienda zanzibar hivyohivyo wanapata fursa hiyo.
2; kuna free trade btn zanzibar na tanganyika. mzanzibar hapati aina yyte ya kikwazo akitaka kufanya biashara tanganyika kwa sababu ya uzanzibar wake na mtanganyika hivyohivyo hapati vikwazo akitaka kufanya biashara zanzibar.
sasa nyinyi munaouona hauna faida tajeni hasara mbili mnazozipta kwa ajili ya huu muungano wetu.
MUNGU IBARIKI TANZANIA MUNGU UBARIKI MUUNGANO WETU.
utaifa ulioporwa ni utaifa gani?
baada ya kuporwa huo utaifa wako ulioasisiwa na wakoloni walioitawala Tanganyika, unajutia uhuru wako uliokukirimu utaifa mpya?
wewe huna utaifa?
unayo passport?
umeishawahi kusafiri nje na kuchanganyikana na watu wa mataifa mengine ukakosa kutambuliwa?
utaifa uliopachikwa na wakoloni wako ndio bora kuliko utaifa tunaouchukua vifuani mwetu na ulioasisiswa na watanzania wenzako wanamapinduzi?
je, mwalimu nyerere, karume na wanamapinduzi wengine walaaniwe kwa kuwa tu waliasisi utaifa mpya wenye heshima kwa mwafrika na usioakisi ubeberu wa magharibi uliozaa ukoloni wa mataifa ya kiafrika?
kwako utaifa wa kutuniukiwa na mkoloni ni bora kuliko utaifa wa kizalendo?
Sijui mawazo kama haya kwa mtu wa JF huanzia wapi?
Nini unachofaidi kwa kuitwa m-Tanzania? nini utapoteza kwa kuitwa m-Tanganyika? Ni matokeo ya kudanyanywa muda mrefu na hatimaye unang'aka kana kwamba umefikiria kwa makini.
Naona tunaendelea kuchanganya mambo tuuu! Mbona kulikuwa na Congo, Ikaja Zaire, ikarudi tena Congo! kipindi chote hicho nini kilileta neena au taabu kwa maisha ya mtu kama wewe!
Hivii, naweza kuruhusiwa kugombea uwakilishi au ubunge huko Zenji bila kikwazo?
KILL, KILL KIIILL wasiotaka uTANGANYIKA WAO waungane na SOMALI au SUDAN si mnapenda kuungana! Mnawaonea wa Zenj tu. Na ukoloni wenu enh!Hatuwezi kujuta, muungano sio lazima, viinchi vingapi vidogo kama karanga vina nguvu kuliko Tanzania na li muungano lake?
Swaziland, Lesotho, Botswana, wameungana na nani?
Hatujaenda Ulaya, viinchi kama Belgium, Luxembourg, Uswizi wameungana na nani?
Kill the Muungano!
mkuu uyasemayo ni ya kweli kabisa.
Kuna watu humu sijui wanafaidishwa nini na huu utawala wa sasa. wanavyoupigia chapuo.
lakini ipo siku tu haya yote yatafika mwisho Tanganyika itarudi, maendeleo tutayaona na hawa wapinzani wa sasa ndio watakuwa wa kwanza kupongeza.
Wazanzibar mnajua sana Kiswahili, labda utanielewa kwa hili: Inzi akikuzunguka zunguka usoni ndio kero. Mbu akikuuma, au nyoka, ni tatizo, anaweza kukuua. Muungano sio kero, ni matatizo. Kwa nini hatutumii Kiswahili fasaha kuelezea matatizo yetu?kila siku itakuwa tunatatua kero, wakati muungano wenyewe ndio kero.
Yaani umemaliza, ningekuwa na uwezo ningekupa nishani.
Ndio maana wengine tunasema to hell with the Muungano!
Najua wengi wenu mtahisi au mtaniona kama mropokaji lkn kamwe damu ya kitanzania na kamwe haitakuwa ya tanganyika wala ya kizanzibari. kwangu hupatwa na mfadhaiko nikimsikia mtu anajitambulisha yy ni mzanzibari au yy ni mtanganyika. uchezeeni muungano leo lkn kesho mutajuta. tunachotakiwa ni kuurekebisha mfumo wa muungano wa si kutengana haswa ktk wakati huu ambao tuhitaji kuujenga uchumi wetu. lkn mkiamua kamwe sitokuwa mtanganyika wala mzanzibari.
nakuunga mkono mkuu,
hata mimi nitabaki mtanzania daima.
Tanganyika siijui,
sikuzaliwa Tanganyika,
wakoloni ndio wanaoijua Tanganyika,
hii Tanganyika ilikuwa shamba la bibi kwa wakoloni,
ha wao wanjua kuwa hawatathubutu kuigeuza Tanzania koloni lao, haiwezekani
Tanzania ni huru na haijawahi kutawaliwa
Tanganyika na Zanzibar yote ni makoloni na hayajawahi kuwa huru
muungano ndio uliokamilisha uhuru wa Tanganyika na Zanzibar
Tanzania ni jina la kizalendo
tena linaakisi uhuru na azma ya kujitawala
tanganyika inaakisi utumwa, ukoloni, na unyonyaji
siipendi Tanganyika,
siipendi Zanzibar
napenda Tanzania
daima nitaililia Tanzania
Mungu ibariki Tanzania!!!
Angalizo kwenu wapendwa, Mwanaone na Miss Judith.
Jitayarisheni na heart attack!
Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulizaa Tanzania baada ya miezi sita tokea kuundwa kwa Muungano. Kabla ya hapo mnajua jina la Muungano liliitwaje?
Baada ya Muungano ,Jina Tanganyika limeyeyushwa kinyemela!
Sasa vipi mnatarajia jina Tanzania litabaki na utanzania utabaki baada ya operation "East African Federation"?
Kama tutafuata utaratibu wa kubadilisha jina kama tulivyofanya kwa Muungano huu tulionao, basi Tanzania, itapata jina jipya la Afrikamashariki baravisiwani na uraia utakuwa Uafrikamashariki.
Kama hamtaki Tanganyika na Utanganyika, wala Zanzibar na uzanzibari... basi na Tanzania na utanzania utabaki kwenye historia tu kama ilivyo kwa jina Tanganyika leo.
Au hamfuatilii mwenendo na hatua za Muungano wa EAC?
Muungano sio kero, ni matatizo. Kwa nini hatutumii Kiswahili fasaha kuelezea matatizo yetu?
Ninapoona Bunge limejaa wawakilishi kutoka Zanzibar tofauti na uwiano wao, hayo mabilioni ya kugharimia hawa wabunge wa kigeni ni kero au balaa?
Ninapoona waziri wa Zanzibar anatangaza hadharani kimabavu kwamba hatalipia Umeme wakati mimi Mtanganyika sithubutu kuikoromea TANESCO, hiyo ni kero au uonevu?
Ninapoona nusu ya mabalozi, mawaziri wa Muungano, viongozi wa vyama, wanatoka sehemu moja ndoooogo ya nchi, hiyo ni kero au upendeleo?
Ninapoona Zanzibar inaandika Katiba inayokinzana na Katiba ya Muungano na kutangaza unilaterally kufuta kitu fulani katika orodha ya mambo ya Muungano, hiyo ni kero au jinai ya dharau?
Ndio maana wengine tunasema to hell with the Muungano!
Mkuu.kheri kuwa mwanafrica mashariki kuliko kuvunjika kwa muungano nicholilia mimi ndugu zangu ni umoja na si chingine.narudia tena kusema tutibu kasoro za muungano ili tuwe na muungano imara badala ya kuuvunja muungano . TUKIANZA KUSEMA SISI NI WATANGANYIKA KESHO TUTASEMA SI NI WAKSAKAZINI TUJIAMULIE NA WENGINE WATASEMA SISI WA KUSINI NA WAZANZIBAR NAO MWISHO WATASEMA SISI WAPEMBA NA HAWA NAO WATASEMA SISI WAUNGUJA. NA SIKU ZOTE UMOJA NI NGUVU UTENGANO DHAIFU. MIMI NAHISI TUWE NA BUNGE LA TANGANYIKA, TUWE NA BUNGE LA ZANZIBAR KAMA ILIVYO SASA NA TUWE NA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WATANZANIA. TUWE NA WIZARA MOJA YA MAMBO YA NJE, MAMBO YA NDANI , ULINZI. HIZI WIZARA TAU ZISITENGANISHWE. YAANI KWA UFUPI UPANDE WA TANGANYIKA WAWE NA MAMBO AMBAYO WATAJIAMULIA WENYWE NA ZANZIBAR WAWE NA MAMBO AMBAYO WATAJIAMULIA WENYWE LKN KUNA MAMBO NI LAZIMA YAWE NA MAAMUZI YA PAMOJA HUSUSANI KTK WIZARA HIZO TATU NILIZOZISEMA.
Mkuu.
Watanganyika wanautaka Muungano na wazanzibari wanautaka muungano. Hii ni kutokana na maoni ninayosoma juu ya mijadala ya Muungano huu.
Ambacho watanganyika na wazanzibari hawataki ni muungano usioeleweka. Muungano wa mazingaombwe, changa la macho au usanii.
Lakini njia nzuri ya kuthibitisha kauli yako ni kwa kuwepo mjadala wa wazi wa kitaifa juu ya muungano na muundo wake na pia kuitisha kura ya maoni.
kwa kuanzia, ule mkataba halisi wa muungano inapasa kutolewa hadharani ili wananchi washuhudie ni nini hasa kilikubaliwa kwa kuanzia.
Mkuu.Hata mimi nitabaki mtz, tz inaweza kubaki hata bila ya znz kwa kuwa hilo ni jina tu ndio maana kuna neno "nia" ambalo liliwekwa kukamilisha jina.Huyo anayesema znz kwa kuwa inabendera,bunge,mahakama nk basi znz ni nchi ni mvivu wa kufikiri na hajui ni vigezo vipi vinatakiwa ili kuifanya znz nchi ktk masuala ya kimataifa.Kwa taarifa yake znz kimataifa sio nchi na wala hakuna anayeijua znz ni nchi huko nje,na kama anabisha asafiri nje ya nchi kama ataiona bendera ya znz nchi za nje zaidi ya bendera ya tz, kama atasikia wimbo wa nchi ya zanzibar ukipigwa zaidi ya wimbo wa taifa la tz, kama ataona ubalozi wa znz zaidi ya ubalozi wa tz, kama ataona passport ya znz zaidi ya passport na visa ya tz, kama atakutana na mtu anayejitambulisha mznz zaidi ya mtu anayejitambulisha kama mtz nk.Kwa hiyo znz kuwa na bendera,wimbo wa znz maana sio wa taifa,mahakama na bunge nk hauifanyi znz kuwa na hadhi ya nchi kimataifa, hayo ni mambo madogo sana ambayo siyo sifa ya kuwa nchi.USA na Canada imeundwa na states na provinces ambazo zinabendera ,mahakama, bunge, nyimbo nk lakini hazina hadhi ya nchi , nchi ni USA na Canada.
Tanzania haiwezi kukwepa historia! Miungano yote ya kulazimisha inapata kifo cha asili. Iangalie USSR Kuanzia vita vikuu vya 2 Hadi 1990 au Yugoslavia chink ya Tito iliyogeuka kuwa nchi Saba za eneo la Baltic. Kwa hapa Africa angalia iliyokuwa Senegambia sasa hivi kuna Senegal na Gambia. Mambo ya muungano hayapaswi kulazimishwa bali watu waingie kwanhiari baada ya referandum.
USA ina muungano wa tofauti ambapo zile states ziliunganishwa kwenye umoja kwa civil wars zilizodumu kuanzia 1776 mpaka mwamzoni mwankarne ya 18. Lakini zile states Zina autonomy kubwa kisiasa na kiuchumi. Status ya Gavana wa California Schwazznegger yaweza kuwa kubwa kuliko hata PM wa Uingereza