Vodacom wajiulize wapi wamezidiwa na Tigo

Tryagain

Member
Nov 23, 2021
66
436
Ndugu zangu mara nyingi tumekuwa na sababu nyepesi sana za kiuchumi pale kampuni zetu zinapoanza kufanya vibaya kwenye soko.

Nimeona kuna taarifa zinazosambaa kuhusu wateja milioni 1.3 kuacha kutumia mtandao wa Vodacom na sababu wakasema ni Tozo hii si kweli kwa asilimia 100.

Wakati wa Utendaji wa Bodi ya wakurugenzi Rostam Aziz Vodacom ilitengeneza mapato mengi kutoka na strategy yao ya kuanzia chini kwenye grass root level kupeleka huduma kwa Wananchi.

Voda wameuacha huu muundo wamebakia mijini huduma za M-Pesa katika mikoa ya Morogoro, Tanga, Manyara, Lindi, Mtwara, Mbeya, Ruvuma zinapatikana mijini tu na Wilaya ni tabu kupatikana.

Huku Tigo wanapatikana katika kila kitongoji na kila kijiji achana na huduma ya Mobile Money tu, huduma ya mawasiliano kwa voda ni tabu na pia imekuwa ya gharama sana ukilinganisha na huduma za mawasiliano kama Tigo na Airtel.

Kama ni Tozo zimewaondoa wateja wa Voda, Airtel ingepata wateja wengi zaidi ila Tigo waliona soko mapema wakajikita kuboresha huduma kwa kipindi cha miezi mitano kampuni ya Tigo imeongeza wateja milioni 1.2.

Kama Voda wanasema kuwa ni Tozo zimewaondolea wateja, vipi kuhusu Halotel na TTCL ambazo zimepoteza wateja wengi ndani ya kipindi kifupi.

Wananchi wa Tanzania wanaishi kwenye word of mouth hawa Tigo wameweza sana kuishi nao wana ubunifu ukitazama kwa kipindi cha miezi mitano Voda hana jambo lolote la kibunifu kwa wateja wake.

Idara ya masoko ya Vodacom imefeli pakubwa haina jipya itafute sababu nyingine.

Mbuzi wa kafara hufa huku akilia.
 
Hili la kwamba tigo wamesambaza mtandao vijijini hebu jitahidi ufanye utafiti upya Mkuu. Nimetembelea wilaya nyingi tigo imeishia makao makuu ya wilaya. Mtandao uliojikita Sana vijijini na ulijinasibu kama mtandao wa wanakijiji ni Halotel.

Tangu ikiwa Vietel lengo lilikuwa ni kuteka soko la vijijini. Nadhani mbia wake Mkuu anajua Sana kucheza na namba si kwenye siasa pekee bali hata kwenye Biashara. Voda na Airtel wanafuatia Kwa wateja vijijini. Kama hutaki kuamini kuwa tozo ni Tatizo basi labda unanufaika binafsi na Tozo.

Kama huamini subiri mabenki yatakachoongea baada ya miezi 6. Watu wameanza kupiga hesabu kabisa ya kutoa hela Benki.

Benki zilikuwa zinatengeneza faida kutokana na service na withdraw fee ili kuencourage deposits. Lakini Sasa Mtu akiweka hela hata mara 5 Kwa mwezi anatoa mara1.
 
Hata Mimi tigo naipenda Sana
..niereweke sio tigo ile ya kwa mparange.nasema uwongo ndugu zangu?
Nadhan kama taifa tumefikia pabaya sana,unaweza jitahidi kufanya kila unaloweza kuzuia akili yako isiwe spoiled na mambo ya kishenzi,lakini mambo ya kishenzi yatakufuata kila mahali. Kulikuwa na umuhimu gani wa kuleta comment ya namna hii kwenye mjadala wa namna hii ikiwa kuna nyuzi nyingi zinazojadili haya mambo unayotaka?
 
Siamini kuwa Vodacom wametoa taarifa ya ukweli kuhusu kupungua kwa mapato.

1. Hawa wanataka kutumia excuse ya tozo ili kudeclare mapato kidogo.

2. Hawataki waonekane kuwa nao wanapiga hela ndefu sababu ya tozo za wananchi. Unajua kwenye hizi tozo, makampuni ya simu na serikali wanagawana hela za watu
 
Siamini kuwa Vodacom wametoa taarifa ya ukweli kuhusu kupungua kwa mapato.

1. Hawa wanataka kutumia excuse ya tozo ili kudeclare mapato kidogo.

2. Hawataki waonekane kuwa nao wanapiga hela ndefu sababu ya tozo za wananchi. Unajua kwenye hizi tozo, makampuni ya simu na serikali wanagawana hela za watu
Nan kakudanganya kwenye tozo,kampuni na serikali wanagawana...

Kitu pekee wanachogawana ni ada ya utoaji.. na sio tozo za serikali...

Then ukwel ubaki wazi tozo zimepunguza wateja wengi sana... Wengi tunaweka ela kwa mitandao ya simu kwa sbbu ya kufanya manunuzi online.. kama luku na maji..

Lakin sio sehemu ya kutunza ela zako kama zamani
 
Nadhan kama taifa tumefikia pabaya sana,unaweza jitahidi kufanya kila unaloweza kuzuia akili yako isiwe spoiled na mambo ya kishenzi,lakini mambo ya kishenzi yatakufuata kila mahali. Kulikuwa na umuhimu gani wa kuleta comment ya namna hii kwenye mjadala wa namna hii ikiwa kuna nyuzi nyingi zinazojadili haya mambo unayotaka?
Ok..mkuu Nimekuelewa
 
Back
Top Bottom