Vodacom tz kwafukuta..

Join Date : 15th September 2012
Posts : 1
Rep Power : 0
Likes Received0
Likes Given0




Umeamua register account kabisa kwa kutetea mkuu kinachozungumzwa??poa karibu bana JF ulingo wa hoja nzito!
 
watz mmezidi kuiba hamuaminiki

Kwanini wanaiba? mimi binafsi spendi wizi and so siwezi Kwa namna yyte kuutetea.
Hawa waTz wanaoiba wanajua kwamba wanazalisha pesa nyingi sana halafu wanalipwa kijimshahara ambacho hakifiki hata tar5 ya mwezi unaofuata. So, wanakuwa hawana ownership ya mradi husika wanaamua kujigawia chao waanze.
 
Wewe unafurahisha kweli, unajua sheria ya kuajiri foreigner kama kuna mtanzania mwenye sifa hiyo hutakiwi kufanya hivyo. Unasema watz wezi lini wamekuwariported police na kupelekwa mahakamani. Wizi uko kote hata hao wanaiba mstafute sababu dhaifu kujustify kuvunja sheria za tz
 
teh teh teh....hata wewe na mimi tukisema no, haina maana wataondolewa Tanzania. By the way, hilo ni duka lake kweli. Ana hiari ya kufanya anachotaka. Namna pekee ya kumbana ni kuwa na sheria zinazofuatiliwa na zinapewa meno ya kufanya kazi.

Well said, tatizo la tanzania tunasheria nzuri lakini hatuzitumii. Na wasiwasi na watu wanaotetea huu upuuzi na kusema wafanyakazi wa voda ni wezi wasiwe wao na wafanyakazi wa uhamiaji wanachukua rushwa kwa hao watu constantly au wananufaika na mfumo huo kwa namna fulani
 

Voda!!! khaaaa nilisikitika sana watu wa CC walioajiriwa na Vodacom walipohamishiwa Ero link na kulipwa pesa ndogo mnoo. Katiba mpya kwa kweli iweke wazi mtu akisitishwa kazi ambayo ni permanet alipwe sahihi na si ule usanii inaniuma sanaa watu walikuwa na 6yrs wakalipwa 2m pamoja na kuchakaza masikio yao
 
Dah, nawashukuru wachangiaji. Kwakweli mmeweka mawazo yenu ya hali na mali, mm nakubaliana na wengi kua c haki kbs coz wa-tz wenye qualification za kufanya hizo kazi.
Lkn nikionacho mm ni kua watanzania wengin tunapenda "ready made" na mbaya zaidi hua tunapenda nyanyasana cc kwa cc, mmesikia huko Tanga RC kamnasa mtumishi wa serikali kibao kwa kunywa maji mbele yake!
Sasa hawa foreigners wameshatusoma na kujua ubovu wetu kua hatupendani thats y wao wanapeana vyeo tu hata km huyo mwajiriwa ameshindwa huko kwako wanaamini kwa Tz ataweza tu.
 
nimesikitika sana kuona jinsi hii mada ilivyochangiwa!

wengine wametokea kuwachafua baadhi ya wafanyakazi wa voda/nsn tofauti na mada ilivoelekeza, hii inaonyesha ni jinsi gani watanzania hatupendani kwa hali yoyote. Nilitegemea kama huyo mwenye mada tofauti angeianzisha kimpango wake kukidhi matakwa yake, kama ni kukamatwa kwa hao anaowaita wezi lakini sio kuleta umbeya jamii forum. tungejaribu kufocus kwenye mada husika kwanza tuone watanzania wenzetu ndani ya nsn wanavoweza kusaidiwa.

tatizo lilipo NSN ni la kweli kabisa, experts ni wengi zaidi ya 35 wakifanya kazi zinazoweza kufanywa na watanzania wenzetu na naamini wenye qualification zao ni wengi sana na tena wako vzr kuliko hawa foreigners kwani wengi wao ni diploma holders tu. Lakini utaona kazi hizo hazitangazwi nchini bali huletana kwa kujuana wenyewe.

ukiangalia kiini cha tatizo ni kile wanachokiita global crisis; ila utaona kiini cha hio crisis ni pengine nchi nyingine huko na sio tz; pia utaona wakileta foreigners nchini kisa tu baadhi yao wamekosa kazi nchini kwao na kwa kujuana ndio wanaletana nchini tanzania kwani hamna uangalizi wa kina kutetea watu wao.

na tukienda global kwa kina zaidi hata management ya nsn haina uhakika kuhusu annual loss iliyopo. Soma link hapa chini:-

The future of NSN: can NSN survive without its Managed Services business? | INVESTAURA

sasa tutafika kweli? kiinua mgongo chenyewe cha nssf kimekuwa utata bado, malipo ya kuachishwa kazi nayo ni peanuts tu tofauti na nchi kama south africa ambako wafanyakazi wa nsn walioachishwa kazi walilipwa 18 times ya salary yao pamoja na marupurupu mengine.

Nilitegemea hii mada ingepewa uzito hata kisiasa, iwe hata hoja binafsi bungeni tuone hili swala la kuongezeka foreign experts kiholela litaweza kukomeshwaje hapa nchini; sijaona michango ya wanasiasa katika hili..najua wengi wako humu na wanalisoma hili; japo ushauri wao basi jamani.

watanzania wenzetu wakiwa kazini wanalipa PAYE, wanaweza kufanya shopping na familia zao na kulipa TAX, wakijikwamua zaidi ndio hao hao future investors ndani ya nchi yao. Je kuwatetea imekuwa tabu? Kweli??

ni hayo tu wadau.
 
Bahati mbaya sana huyo mlalamikiwa-wizara ya kazi na ajira ndiyo inawasaidia wageni kukiuka sheria za kazi na ajira, kwa kuwawezesha kupata vibali vya kufanya kazi nchini, hata kazi ambazo zingeweza kufanywa kwa ufanisi mkubwa na wazawa.

Na katika hilo wizara ya kazi wanashirikiana kwa karibu sana na idara ya uhamiaji ili kuona kwamba wageni wanazidi kujazana nchini na kunyima ajira za wazawa kwakuwa tu wao wanawezeshwa binafsi. Haya makampuni ya kigeni hayaoni hasara hata kidogo kutoa rushwa ili wageni wapate vibali vya kuishi na kufanya kazi nchini.
 
Wale wanaosema tuna serikali makini ngoja tuone kama watafanyia kazi hii barua. Serikali yetu wala hata haijali. Nenda pale white sand na Golden tulipu ukute jinsi wahindi wanavyohudumia. Unajiuliza kweli hawa wana working permit. Unajiuliza tena mbona hizi hotel kuna mikutano mingi sana ya serikali inafanyika hapo, hawa viongozi wetu hawaoni hilo? Kweli serikali makini inaweza mpa permit mhindi aje apakue chakula hotelini? Je vijana wetu watafanya kazi gani. Nikiifikiria hii serikali yetu jamani huwa nachoka hoi.

Nilimwuliza rafiki yangu ambaye ni mwanachama wa chama tawala akaniambia ni sera ya chama hiyo. Eti ni kweli?
 
Kaka mimi niko humu toka 2004,wakati huo Voda,yaani uliyosema nakupa 5

 

ulitaka wapewe nani??? mfano mzuri ni benki mpya nyingi ziliajiri vijana wasomi kwenye nafasi nzuri tuu lakini few years later wote wamefukuzwa kwa ajili wa wizi na ubadhirifu. tukubali ukweli hata sisi tunaopiga mayowe kuhusu ufisadi tuulize nafsi zetu jee tungepata hizo nafasi tungefanya tofauti??? na mimi kwa uzoefu ninaamini wapigaji mayowe sana ndiyo potential mafisadi. Inafika wakati lazima tukubali ukweli kuwa wengi wetu siyo waaminifu, wengi wetu siyo wachapa kazi na wengi wetu ni watu wa wakulalamika tu. waache wakenya, waganda na wengineo watufundishe namna ya kuchapa kazi. Investor anapokuja kuwekeza mahala anataka kulinda investiments zake na zilete faida. kama kutuajiri sisi wa tz kutamletea matatizo ya mchwa ni bora alete manpower toka mbali.
 
Kwani muhindi haruhusiwi kuwa muhudumu wa hotel? Au wahindi sio watanzania?
 
Mmesahau tafuteni ni kiasi gani kinalipwa kwa hawa expatriates pelekeni TRA, pia msisahau WHT kwenye service mnazopeleka nje (outsourced).
 
hatunasaibabu ya rejareja, hizo nndio sera za CCM, kuna tofauti gani na wakina Mwammvita Makamba na hao wakina Ngejeja na yule finance aliyeenda TANESCO, hivi unampa mpumbavu kama Rostam nchi unate ya gemea vitu tofauti? tena bado hamjajua kati yao wanaume wangapi wameoana humo na wanaoa wangapi umo ndani, tunashindwa kuwalinda wat oto wetu kwa kuwaendeleza viongozi wasio na vigezo na serikali ya chama dhaifu, fagieni hao CCM kama mnataka maisha ya heshima, watoto wetu wakiume wataolewa mbele yetu na sisi tutachekelea, hiyo kampuni ifutwe vodacome ilikuja kwa mkataba kuwa na waajiriwa wake, huo ni utapeli mwingine wa kutumia uhamiaji dhaifu, na serikali dhaifu, usishangae watoto wa hao viongozi wangapi wanaosomeshwa India bilashaka kwa dola hata 1000 kwa mmoja lakini watanzania wangapi vijana wetu wanapoteza nafasi za maisha yao kwa kodi za baba zao,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…