Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,262
Hello Hello.....
Patashika ya Ligi Kuu Tanzania Vodacom Premier League kuendelea kuvurumishwa leo December 31, 2019 kunako Uwanja wa Taifa, ambapo Mabingwa wa Nchi Simba SC Mnyama Mkali Mwituni, wanawakabili Ndanda FC Wanakuchele kutoka mkoani Mtwara.
Mchezo wa leo unatarajiwa kuwa mkali na wa kusisimua kwa muda wote wa dakika 90 huku kila timu ikihitaji alama tatu muhimu.
Simba SC, ambayo inaongoza ligi kwa kukusanya alama 31 kwa michezo 12 inahitaji ushindi ili iendelee kujikita zaidi kwenye msimamo wa VPL na kuongeza morali kuelekea mpambano wake na Mtani wake Jumamosi ya January 4, 2020.
Ndanda FC kwa upande wao wanahitaji ushindi mno baada ya msimu huu kuanza kwa kuchechemea, ambapo mpaka sasa ni ya pili kutoka chini ya msimamo wa VPL kwa alama 7 wakiwa wamecheza michezo 13.
Wanasimba na madau wa soka popote ulipo sikiliza matangazo au shuhudia kandanda ya viwango wa shirikisho la soka barani Afrika kutoka kwa Simba SC, Mnyama Mkali kuanzia saa 10:00 jioni..! Usikose Ukaambiwa
Kulitaka Mwana..Kulipewa Mwana
••••••••••========•••••
Timu ya Simba SC, leo wameweza kuibuka na ushindi wa mabao mawili bila majibu dhidi ya Ndanda FC kwenye mfululizo wa VPL
Simba walianza kufunga bao la kwanza kwa free kick iliyopigwa na Francis Kahata katika dakika ya 13 ya mchezo.
Deo Kanda aliyeingia baada ya Kahata, aliweza kuhitimisha ushindi kwa kufunga bao la pili kunako dakika ya 85' ya mchezo, kwa matokeo hayo Simba SC wameendelea kujikita kileleni kwa jumla ya alama 34 kwa michezo 13.
FT: Simba SC 2-0 Ndanda FC
Patashika ya Ligi Kuu Tanzania Vodacom Premier League kuendelea kuvurumishwa leo December 31, 2019 kunako Uwanja wa Taifa, ambapo Mabingwa wa Nchi Simba SC Mnyama Mkali Mwituni, wanawakabili Ndanda FC Wanakuchele kutoka mkoani Mtwara.
Mchezo wa leo unatarajiwa kuwa mkali na wa kusisimua kwa muda wote wa dakika 90 huku kila timu ikihitaji alama tatu muhimu.
Simba SC, ambayo inaongoza ligi kwa kukusanya alama 31 kwa michezo 12 inahitaji ushindi ili iendelee kujikita zaidi kwenye msimamo wa VPL na kuongeza morali kuelekea mpambano wake na Mtani wake Jumamosi ya January 4, 2020.
Ndanda FC kwa upande wao wanahitaji ushindi mno baada ya msimu huu kuanza kwa kuchechemea, ambapo mpaka sasa ni ya pili kutoka chini ya msimamo wa VPL kwa alama 7 wakiwa wamecheza michezo 13.
Wanasimba na madau wa soka popote ulipo sikiliza matangazo au shuhudia kandanda ya viwango wa shirikisho la soka barani Afrika kutoka kwa Simba SC, Mnyama Mkali kuanzia saa 10:00 jioni..! Usikose Ukaambiwa
Kulitaka Mwana..Kulipewa Mwana
••••••••••========•••••
Timu ya Simba SC, leo wameweza kuibuka na ushindi wa mabao mawili bila majibu dhidi ya Ndanda FC kwenye mfululizo wa VPL
Simba walianza kufunga bao la kwanza kwa free kick iliyopigwa na Francis Kahata katika dakika ya 13 ya mchezo.
Deo Kanda aliyeingia baada ya Kahata, aliweza kuhitimisha ushindi kwa kufunga bao la pili kunako dakika ya 85' ya mchezo, kwa matokeo hayo Simba SC wameendelea kujikita kileleni kwa jumla ya alama 34 kwa michezo 13.
FT: Simba SC 2-0 Ndanda FC