Vodacom na CRDB kuna mtandao wa wizi hatari

Vodacom na CRDB kuna mtandao wa wizi hatari

wiseboy.

JF-Expert Member
Joined
Aug 11, 2014
Posts
2,931
Reaction score
4,549
Kwa kweli siwezi kuvumilia kwa hili,huu ni wizi wa kishenzi kabisa mnataka kunifanya na naapa nitawadhalilisha nyie watu na mtanilipa fidia kubwa sana,leo nimehamisha salio kidogo la pesa kutoka ktk akaunti yangu ya CRDB kwenda m pesa,nipo mbali na benk nikaona huduma hii itanifaa na nina shida hasa sina hata cent,cha ajabu tangu asubuhi hadi sasa pesa haijaingia kwenye m pesa yangu pamoja na CRDB kunitumia msg ya ref kuonyesha kuwa pesa imetumwa ktk m pesa na namba ya ref ninayo,kwenye akaunt yangu nimeangalia salio nikaona limepungua kwa kuhamishwa kwenda m pesa,sasa pesa zangu mmepeleka wapi nyie watu?

Mbona mnaonekana kabisa kuwa mmeniibia,nitawapeleka mahakamani nyote nidai fidia kwa usumbufu mlionipa, nitadai mamilioni ya fidia,mnajitangaza kwa gharama kubwa,kumbe hamna lolote utapeli tu umewajaa,mi nina shida bwana,pesa zangu ziko wapi? tangu asubuhi? nyie ni wezi mmepanga kunipiga kimya,nataka pesa zangu bwana mbona hamna hata aibu nyie mkoje lakini? NATAKA PESA ZANGU MIE NINA SHIDA HAPA NILIPO.

UPDATES

Wakuu,naamini kabisa humu ndani kuna maagent wa vodacom na CRDB,baada ya kuchimba mkwara wa kufa mtu kuwa kwa nini hawajaniwekea pesa zangu tangu asubuhi ambazo nilizihamisha kutoka ktk akaunt yangu kwenda m pesa,nimeshangaa ndani ya dk 30 tu pesa ikawa imeingia,nikajaribu kuhamisha tena laki kwenda m pesa ajabu ndani ya dk 1 tu ikawa imeingia,japokuwa sikutoa details zangu hapa,lakini naamini nimeokoa wengi siku ya leo wasidhulumiwe baada ya maagent wao kusoma mkwara wangu nadhani wali access ili kila aliyefanya transfer apate chake kabla mambo hayajaharibika,hawa jamaa huwa siyo wa kuchekea,ukilemaa wanakuliza kweli,kama ishu ilikuwa mtandao mbona transaction ya pili imechukua dk 1 tu?

wakati kwa kawaida huwa inachukua hata dk 15,acheni wizi wa kishamba nyie,yaani ningewafunga kweli,sasa hivi karoho kametulia,nipo hapa napata safari ya baridi na nimeagiza mbuzi choma kilo nzima,napepesa macho kuona kama naweza kupata ka mrembo kakunifariji night yote hii,usiku mwema wakuu,wacha nile kilaji mtoto wa watu mie
 
Ha!haha! hayo yote ulioandika hapa si sehemu yake kiongozi,,unatakiwa upige simu vodacom makao makuu au crdb huduma kwa wateja watakusaidia sana.
 
Punguza munkari....

Matatizo ya network yapo....

Ni pale upo desparate una shida halafu ngoma inachelewa loh!!!

Pole
 
Kwa kweli siwezi kuvumilia kwa hili,huu ni wizi wa kishenzi kabisa mnataka kunifanya na naapa nitawadhalilisha nyie watu na mtanilipa fidia kubwa sana,leo nimehamisha salio kidogo la pesa kutoka ktk akaunti yangu ya CRDB kwenda m pesa,nipo mbali na benk nikaona huduma hii itanifaa na nina shida hasa sina hata cent,cha ajabu tangu asubuhi hadi sasa pesa haijaingia kwenye m pesa yangu pamoja na CRDB kunitumia msg ya ref kuonyesha kuwa pesa imetumwa ktk m pesa na namba ya ref ninayo,kwenye akaunt yangu nimeangalia salio nikaona limepungua kwa kuhamishwa kwenda m pesa,sasa pesa zangu mmepeleka wapi nyie watu? mbona mnaonekana kabisa kuwa mmeniibia,nitawapeleka mahakamani nyote nidai fidia kwa usumbufu mlionipa, nitadai mamilioni ya fidia,mnajitangaza kwa gharama kubwa,kumbe hamna lolote utapeli tu umewajaa,mi nina shida bwana,pesa zangu ziko wapi? tangu asubuhi? nyie ni wezi mmepanga kunipiga kimya,nataka pesa zangu bwana mbona hamna hata aibu nyie mkoje lakini? NATAKA PESA ZANGU MIE NINA SHIDA HAPA NILIPO.

Wapigie Voda 15366, watakwambia hela iko wapi; kama haijafika kwao basi itakuwa hewani na unaweza ukawaambia CRDB wairudishe kwenye account yako.
 
CRDB huwa wanaibiwa mabilioni mengi tu kila mwezi na wafanyakazi wao.
Taratibu zinakataza kutangaza magnitude ya wizi ndani ya benki hiyo.
Mabenki mengine pia wana kansa hiyo hiyo.
 
Wapigie Voda 15366, watakwambia hela iko wapi; kama haijafika kwao basi itakuwa hewani na unaweza ukawaambia CRDB wairudishe kwenye account yako.

Pole sana wiseboy.Ni tatizo la mawasiliano tu hilo halina dawa kwa nchi za kiafrika.Kuna msemo wa kiingereza usemao 'system is always 100% not perfect'.Tuombe mungu huo mkongo wa taifa ukiimarika pengine utasaidia kuimarisha mtandao hapa nchini.Nadhani kama haitofika ktk namba ya m pesa nadhani itarudishwa ktk akaunti yako ya crdb
 
Pole sana mdau! Ipo hewani hiyo! Wapigie wahusika, hapa si mahali pake wiseboy!
 
Jf sehemu ya faraja japo wakati mwingine ukibugi unaporomoshewa madongo!
 
Vodacom na mabenki ni wezi sana. Jifunzeni kuwa mnapata statement za account zenu kila wakati.
 
Unaitwa "Wiseboy",jaribu kulitendea haki jina lako.Pamoja nakushauriwa uwe na subira,jifunze kupeleka malalamiko mahali husika.Lugha na namna ulivyotoa madai yako havisadifu jina lako.
 
Wakuu,naamini kabisa humu ndani kuna maagent wa vodacom na CRDB,baada ya kuchimba mkwara wa kufa mtu kuwa kwa nini hawajaniwekea pesa zangu tangu asubuhi ambazo nilizihamisha kutoka ktk akaunt yangu kwenda m pesa,nimeshangaa ndani ya dk 30 tu pesa ikawa imeingia,nikajaribu kuhamisha tena laki kwenda m pesa ajabu ndani ya dk 1 tu ikawa imeingia,japokuwa sikutoa details zangu hapa,lakini naamini nimeokoa wengi siku ya leo wasidhulumiwe baada ya maagent wao kusoma mkwara wangu nadhani wali access ili kila aliyefanya transfer apate chake kabla mambo hayajaharibika,hawa jamaa huwa siyo wa kuchekea,ukilemaa wanakuliza kweli,kama ishu ilikuwa mtandao mbona transaction ya pili imechukua dk 1 tu? wakati kwa kawaida huwa inachukua hata dk 15,acheni wizi wa kishamba nyie,yaani ningewafunga kweli,sasa hivi karoho kametulia,nipo hapa napata safari ya baridi na nimeagiza mbuzi choma kilo nzima,napepesa macho kuona kama naweza kupata ka mrembo kakunifariji night yote hii,usiku mwema wakuu,wacha nile kilaji mtoto wa watu mie
 
Wakuu,naamini kabisa humu ndani kuna maagent wa vodacom na CRDB,baada ya kuchimba mkwara wa kufa mtu kuwa kwa nini hawajaniwekea pesa zangu tangu asubuhi ambazo nilizihamisha kutoka ktk akaunt yangu kwenda m pesa,nimeshangaa ndani ya dk 30 tu pesa ikawa imeingia,nikajaribu kuhamisha tena laki kwenda m pesa ajabu ndani ya dk 1 tu ikawa imeingia,japokuwa sikutoa details zangu hapa,lakini naamini nimeokoa wengi siku ya leo wasidhulumiwe baada ya maagent wao kusoma mkwara wangu nadhani wali access ili kila aliyefanya transfer apate chake kabla mambo hayajaharibika,hawa jamaa huwa siyo wa kuchekea,ukilemaa wanakuliza kweli,kama ishu ilikuwa mtandao mbona transaction ya pili imechukua dk 1 tu? wakati kwa kawaida huwa inachukua hata dk 15,acheni wizi wa kishamba nyie,yaani ningewafunga kweli,sasa hivi karoho kametulia,nipo hapa napata safari ya baridi na nimeagiza mbuzi choma kilo nzima,napepesa macho kuona kama naweza kupata ka mrembo kakunifariji night yote hii,usiku mwema wakuu,wacha nile kilaji mtoto wa watu mie

kwa hiyo povu lote lile lengo lilikuwa upate bia na kuutafuta ukimwi!
 
Wakuu,naamini kabisa humu ndani kuna maagent wa vodacom na CRDB,baada ya kuchimba mkwara wa kufa mtu kuwa kwa nini hawajaniwekea pesa zangu tangu asubuhi ambazo nilizihamisha kutoka ktk akaunt yangu kwenda m pesa,nimeshangaa ndani ya dk 30 tu pesa ikawa imeingia,nikajaribu kuhamisha tena laki kwenda m pesa ajabu ndani ya dk 1 tu ikawa imeingia,japokuwa sikutoa details zangu hapa,lakini naamini nimeokoa wengi siku ya leo wasidhulumiwe baada ya maagent wao kusoma mkwara wangu nadhani wali access ili kila aliyefanya transfer apate chake kabla mambo hayajaharibika,hawa jamaa huwa siyo wa kuchekea,ukilemaa wanakuliza kweli,kama ishu ilikuwa mtandao mbona transaction ya pili imechukua dk 1 tu? wakati kwa kawaida huwa inachukua hata dk 15,acheni wizi wa kishamba nyie,yaani ningewafunga kweli,sasa hivi karoho kametulia,nipo hapa napata safari ya baridi na nimeagiza mbuzi choma kilo nzima,napepesa macho kuona kama naweza kupata ka mrembo kakunifariji night yote hii,usiku mwema wakuu,wacha nile kilaji mtoto wa watu mie
Benki wakati wote wanaogopa "a run on the bank" yaani mass withdrawal kutokana na kukosa imani na benki hiyo.

Kwa kweli wateja wengine mkiona matatizo yoyote wajulisheni wadau kwa mtindo huu, na matatixo yasiporekebishwa unasepa na cash yako.

Hilo la fogo dogo na mbuzi choma ni la kwako mwenyewe, hsla hala lakini!
 
Pia msiangalie tu hizo huduma pekee. Kwenye kaunta zao hasa wakati unachukua hela muwe makini sana. Ukichukua kuanzia laki tano kagua hela zako vizuri. Aidha zisitimie au wanakuchanganyia na noti mbovuu. Yameshanikuta ila niliwarudishia wakanibadilishia
 
Sina uhakika kama mkwala wako ndio umesaidia sababu hata namba za account na simu hukuweka, wangekutambuaje? Pesa ikitoka kwa account unatumiwa taarifa. Wakati huo inaenda vodacom. Na ikitoka vodacom kuingia mpesa account yako unatumiwa taarifa. Sometimes process inachelewa kutokana na shida ya mtandao.
 
Back
Top Bottom