Vodacom mnakera na meseji zenu

Vodacom mnakera na meseji zenu

Deo Haule

Member
Joined
Aug 9, 2016
Posts
41
Reaction score
34
Nadhani kuna wadau wataniunga mkono kwa hili
Vodacom mmezi na mameseji yenu ya promo yani nimejaribu kufuatilia mitandao yote lakini kwa vodacom mmezidi yote punguzeni jamani had I mda mwingine tuapuuzia kusoma meseji za maana kwa kudhani mmetuma nyie hizo za kwetu
 
Voda wanakera sana. Kuna wakati simu inaingia ukipokea unakutana na matangazo na adithi. Wanakera....wakicheza watapigwa show ya kibabe mahakamani
 
Wanafanya simu zetu ndio vituo vyao vya matangazo, inabidi waanze kutulipa shuaini hawa. Mameseji yao hadi usiku umelala yenyewe yanatuma tu!
 
Wanafanya simu zetu ndio vituo vyao vya matangazo, inabidi waanze kutulipa shuaini hawa. Mameseji yao hadi usiku umelala yenyewe yanatuma tu!
😃😃😃😂
 
Unaziblock vipi? Maana nyingi hazina namba
Report as spam then ok
Screenshot_20210627-215214~2.png
 
Unaziblock vipi? Maana nyingi hazina namba
Mimi simu yangu ina 'block phrases" unaandika maneno yote ambayo yakiwa kwenye msg hiyo msg iblokiwe.
Mfano "Mkopo" mameseji yao yenye neno mkopo yote hautayaona.
Songesha, Shangwena, hongera ! Wow! Ni rahisi! Milionea! Sport pesa, soka letu nk. Hayo maneno yote nimeyalima block hivo sipokei mimeseji yao. Na namba zinazopiga nimeblok pia.
 
Nadhani kuna wadau wataniunga mkono kwa hili
Vodacom mmezi na mameseji yenu ya promo yani nimejaribu kufuatilia mitandao yote lakini kwa vodacom mmezidi yote punguzeni jamani had I mda mwingine tuapuuzia kusoma meseji za maana kwa kudhani mmetuma nyie hizo za kwetu

Aisee haunishindi mimi kwa kukasirishwa na haya mameseji ya Voda! Yaani hili li mtandao kwanza linatukamua hela nyingi kuliko mtandao wowote hapa nchini. Bando zao ni very expensive!! As if hiyo haitoshi, kila dakika ni kujaziwa mameseji yasiyo na kichwa wala miguu mfano:
  • Twende mjini
  • Whatsap Statasi (hizi ukisoma utatamani kutapika)
  • Pesa ni mpesa
  • Kimataifa
  • Sokaletu
  • Bahati nasibu
  • Voda Bima
  • Vodacom ofa
  • Songesha
  • Jimixie
  • Mara umezawadiwa muito gani sijui
  • Vodacom App
  • The Best
  • Ofa maalum
  • PATAZAIDI
  • VodacomLive
  • Shangwena
  • VodaMtonyo.........!!!
  • Na upuuzi mwingine mwingi

Hapo bado hujatumiwa matangazo ya makampuni mara KFC, Bayport, sijui Betting gani... mpaka inafika mda mtu unawaza hii simu ni yakwangu au ni bango la vodacom kubandika matangazo..??🙄🙄

Vodacom mnakera mnakera mnakera!!
 
Mimi simu yangu ina 'block phrases" unaandika maneno yote ambayo yakiwa kwenye msg hiyo msg iblokiwe.
Mfano "Mkopo" mameseji yao yenye neno mkopo yote hautayaona.
Songesha, Shangwena, hongera ! Wow! Ni rahisi! Milionea! Sport pesa, soka letu nk. Hayo maneno yote nimeyalima block hivo sipokei mimeseji yao. Na namba zinazopiga nimeblok pia.
Mwe mwe mweeeh!! Kwahiyo hii tekino yangu nipambane na hali yangu?
 
Back
Top Bottom