Voda waongeza gharama za Bando?

Voda waongeza gharama za Bando?

Mi natumia kuweka pesa tu
na gharama za m-pesa zimepanda kuanzia gharama za kutuma na kutoa. mf. kutuma 100,000 sio 650/= ni 800/=. ongezeko la 150/= kwa mtandao si haba MBAYA ZAIDI MAWAKALA HAWALIJUI HILO ONGEZEKO MAANA HAWAJAPEWA MABANGO (CHARTS).
 
Sielewi tatizo ni simu yangu au ni mtandao wa voda tangu juzi napata taabu sana ya kupata data..3G inapatikana kwa taabu kwa dar aah..!
 
Vifurushi vyote vipo wadau! Isipokuwa wameongeza na kubadilisha mpangilio wa kuingia. Bonyeza *149*01# chagua 5(Internet mwaka 1bure), tena chagua 1. Internet (mwaka 1 bure). Ndipo utaona Vifurushi vyote vya 24hrs, week na mwezi.
Yaani hata Vifurushi vya walalahoi vipo kama kawa.
Mkuu Ndulime nimeona lakini jana walikuwa hawajaweka hayo mabando ya walala hoyi nimeangaika sana hadi nikanunua la sh. 2500 halafu wameyaficha sana hayo mabando
 
Back
Top Bottom