Viwanja vya NMC Arusha: Dr. Slaa akamatwa, Polisi yajaribu kuwaondoa kwa nguvu CHADEMA

Jamani, hivi kweli hakuna njia mbadala ya kulishughulikia hili jambo?. Kama Lema yuko ndani kwanini tusiache sheria ifuate mkondo wake?, huo mkutano hapo NMC utasaidia vipi katika kutatua tatizo hili?. Kweli imeshindikana kukaa mezani na kulizungumza suala hili kistaarabu?.

Inawezekana kabisa kuna mambo hayaendi ipasavyo lakini pia jinsi ya kudai haki isitumike fujo, busara na hekima itumike badala yake.

Busara hiyo hiyo ingetumika kumwachia Lema hata bila dhamana kwan Lema siyo mtu ambaye unaweza kumtafuta usimpate' wangemtoa ili kuepuka haya yote!
 
Daima taifa la amani linahitajika kutimiza haki na kutoa uhuru wa wananchi wake , lakini ninachoona mimi ni kuwa taifa letu limefikia wakati wa kusitisha vitisho dhidi ya wananchi wasio na zana.

Kinachoendelea arusha ni ukandamizaji wa haki za binadamu na uhuru wa watu kutoa maoni yao, pia kitendo cha hakimu au jaji kutotoa dhamana kwa Mh.Lema ni dhahiri inaonyesha jinsi gani mahakama zetu haziko huru na zinajiendesha kwa mashinikizo ya chama tawala.

Wito kwa polisi kuwa wazalendo na kuheshimu haki za wananchi za kueleza hisia zao na chombo cha mahakama kuwa huru na si kukandamiza wananchi la sivyo taifa litaelekea katika mkondo mbaya

Mungu ibariki Tanzania
 
Tupo pamoja wana ARUSHA mapambano muda wote,dhuruma inayofanywa na mkoloni mweusi CCM inatosha.Wao wana PESA na MAFISADI na POLISI,sisi tuna CHADEMA Tuna MUNGU anayetulinda.VIVA CHADEMA
 
Nimeanza kuamini kuwa humu ndani kuna watu huwa wanatulisha na kutujaza vitu visvyoaminika kabisa

kama huwezi amin kivyako mie nnae kwambia nimekesha hapo mpaka walipo kuja hao polis vibalaka wa ccm.
 
Wakuu watu wametawanywa na polisi viwanja vya NMC ni polisi na magari yao, lakini jambo hili ndiyo mwaafaka wa amani Arusha?????
 
Hapo kwenye RED kama hizo ndizo ajenda basi CHADEMA ijitazame upya!
USHAURI KWA CHADEMA
Jaribu kadri muwezavyo kujitenga na hili jambo la Vurugu/uvunjifu wa amani mnalousishwa nalo. Imesemekana Chadema ni chama cha vurugu kwa muda mrefu na kumbukeni uongo ukirudiwa mara nyingi basi ugeuka kuwa ukweli.

Tunapinga mipango yoyote ya kulipa kisasi kwa kuwaua askari wetu, jifunzeni kutoka ARAB SPRING. Ili maandamano yafanikiwe ni bora waandamanaji wajitenge na vitendo vya vurugu otherwise sahau Public sympathy!
Askari wa nani. Kibaraka wa mafisi mwitu unalipwa bei gani!??
 
Katika kile kilichosadikiwa tangu awali hakika imetimia kwani yapata majira ya saa tisa na nusu hata kumi kasorobo alfajiri,Askari wakiwa tayari kupambana na NGUVU ya UMMA ilikuwa kwenye mkesha,walivamia uwanja wa NMC na kuwatawanya raia walikuwa uwanjani usiku kucha kwenye mkesha. Sijajua kama wamejeruhi ama wameua lakini hakika risasi ya moto zilisikika kila corner hp A town. NAWASILISHA!!

natamani 2015. hamtashinda. waTZ wa leo tunaujua ukweli. ccm wote wanaofurahia
 
Ni saa kumi na nusu alfajiri. Mabomu ghafla yanaanza kurindima kwenye viwanja vya NMC Arusha. Tutarajie injuries kwan hadi saa kumi na moja vishindo vya milipuko vinaendelea.
Wanachama wa Chadema walikuwa wamefanikiwa kukesha hadi muda huo na usiku ulipambwa na hotuba mbali-mbali pamoja na nyimbo.
Will keep you posted on new developments



eeeh mapinduzi yanaendelea...
 
Asanteni sana wakuu kwa kuendelea kutupasha habari!!! Mungu ibariki chadema pamoja sana wana A.town
 
Always a nation of peace is required to fulfill the rights and freedoms of its citizens, but I saw that I am that our nation has reached the time of stopping threats against citizens without tools.

What is going on arusha is the suppression of human rights and freedom of people to express their views, too the act of a judge or the judge withhold bail for Mh.Lema obviously shows how our courts are not independent and zinajiendesha to pressures of the ruling party.

Call for police to be patriotic and respect the rights of citizens to express their feelings and a judiciary to be independent and not suppress the public is bound to state otherwise in bad stream God Bless Tanzania
 
Ni ujinga kutumia silaha ya woga, mashaka, ubinafsi na chuki kuondoa maadui maradhi, umaskini, ujinga, rushwa, ufisadi na ukandamizaji katika nchi yenye utawala wa kidhalimu duniani kama Tanzania.
Ni heri kufa siku 1 ukiwa umesimama kwa miguu yako kuliko kuishi miaka 1000 Ukiwa umepiga magoti. Twende NMC WANA WA ARUSHA TUKAIKOMBOE NCHI YETU. Mungu atasimama upande wetu.
 
JAMANI LILE GARI LA MATANGAZO PA CHADEMA,LIKO UKU MBAUDA POLIS WANALAZIMISHA KULITEKA KAMA VP MSAADA JAMANI MAANA HUU UKIMAAAAAAAAAMAMAZAO POLISI,na taarifa nilizonazo tayar kuna maiti zimeokotwa.
 
Ili maandamano yafanikiwe ni bora waandamanaji wajitenge na vitendo vya vurugu otherwise sahau Public sympathy!

Taarifa zilizopo ni kwamba walikuwa wamekesha hapo NMC hawakua wakiaandamana.,tatizo ni hawa wenye madaraka kudhani kwamba nguvu pekee ndio suluhisho la kila kitu..lazima tubadilike kwa manufaa ya kizazi kijacho..
 
wacha wewe upuuzi...watu tache kufanya kazi kwa ajili ya maendeleo yetu na vizazi vyetu vijavyo tuhangaikie maandamano na kukesha kusiko na tija.


hana jipya,,,kasjaishiwa sera.


Mtajipanga sana upya mwaka huu


Kwa ujinga wao lazima wadhurike...wangekuwa wanajitambua wasingeenda kuandamana


Naona kujipeleka GERezani ishakuwa staili mpya ya viongozi wa chadema


Great thinkers! It is high time now to discuss sensitive issues like this one as a real human being of Tanzanian nature and not otherwise. Sisi sote tu mashuhuda wa ghasia zinazoendelea hivi sasa ktk nchi mbalimbali hapa duniani, kote huko vurugu na hata vifo vya raia wengi akiwemo THE AFRICAN GIANT MAN (GADAFI) zilianza kidogo kidogo kama ambavyo hali inavyo ashiria hapa kwetu.

Viongozi wetu wa nchi hii iliyo batizwa kwa jina KISIWA CHA AMANI waamke na kufanya kazi kama watanzania kweli katika kutatua kero za wananchi na siyo kutumia NGUVU kama ambavyo baadhi yetu wamejisahua na hata kushabikia huu ufedhuli. Yatupasa tusome alama za nyakati na kuelewa kuwa AMANI bila HAKI kwa ulimwengu wa sasa ni kujidanganya.

Ee MUNGU wape viongozi wetu uwezo wa kutuepusha na ghasia hatarishi kwa busara zaidi.
 
Back
Top Bottom