Vituo vyetu vya TV uozo mtupu........

Vituo vyetu vya TV uozo mtupu........

TCleverly

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2013
Posts
1,921
Reaction score
873
Pamoja na kusikia kwamba mtwara kuna vurugu kubwa lakini hakuna hata kituo kimoja cha television kinachoonyesha au breaking news hizo.....tbc wanaonyesha harusi,channel 10 wanaonyeshamakwaia wa kuhenga sijui,stat tv wanaonyesha wanyama,itv wanaonyesha tamthilia,eatv wanaonyesha irene kiwia,clouds tv muziki!!!!!!hivi ni kwamba hawana anchors huko au ndio wako kisiasa na woga????
 
anza kuilaumu TBC kwanza ndipo ufwate hizo binafsi ambazo angalau zinajitahidi kutupa breaking news mfano ITV ....... TBC NDO TELEVISION YETU YA TAIFA
 
anza kuilaumu TBC kwanza ndipo ufwate hizo binafsi ambazo angalau zinajitahidi kutupa breaking news mfano ITV ....... TBC NDO TELEVISION YETU YA TAIFA

mkutano wa chama cha mapinduzi,popote utarushwa tena live,tbc1 lakini mambo muhimu tena yanayo wagusa watanzania ni mwiko kuonyeshwa tbc sasa tunajiuliza hii tbc niya nani,wananchi au ccm na kama niya ccm kwanini sisi wananchi tukilipie chombo cha chama kodi zetu na kiwafaidishe ccm badala ya walipa kodi,dawa ni serikali itakayo ingia madarakani 2015 kuwatimua viongozi wote wa tbc na kulisuka upya shirika hili ikiwa kumrudisha comrade [tido mhuando] na kuwarudishia watanzania chombo chao,
 
Shame upon them, uzalendo sifuri, tuna waandishi makanjanja, na wote wamefikiwa bei ispokuwa kubenea,kichere na wenzake wa gazeti la mwanahalisi.
Tbcccm ni zaidi ya aibu,
 
Sio lazima Vituo vya Television hata Blog zitakuelezea
MTWARA KUMEKUCHA
Labda nikuelezee tu kuwa hii hali itatulia km upepo upitao na Bajeti itaendelea na kupita
Hata Bomba la gesi litajengwa, vurugu ni kitu cha kawaida hasa kwa vijana, iwe Simba na Yanga au Manchester & Bayern ni hulka ya kishabiki kufuata mkumbo
Hivi mnataka Tanzania yote wafanye hivyo ili Nchi isitawalike,

  • Kilimanjaro wawadhuru watalii ili wasipande Mlima?
  • Loliondo watumie mishale na mikuki kuwafukuz watalii
  • Mtera na Dodoma waangushe nguzo za umeme Nchi ikae gizani?
  • Tabora na Kilosa waing'oe reli ya kati kwa kufungua mataluma ili tukose wote
IMG_20130522_102259.jpg

Iko siku wala haitachukua mwezi hawa vijana watajua wajibu wao na kuwataja wachochezi na ajira watapata tu wala Bomba hawataligusa
 
Hao watakuja juta hawajui baada ya hapo wanarudi kulala na maumivu na vilio vya kuumia, kupoteza pesa zao. Amini siku zote fujo hazisaidii. Baada ya hapo mmoja mmoja ataanza juta kwa kile afanyacho.
 
Na diliki kusema wana mtwara mmetenda jambo baya sana ktk historia ya maisha yenu! Ni nani huyo anayewadanganya? Mtajuta na mnadhurumu haki ya vizazi vyenu.
 
tuna vyombo viwili vya kutupa habari hapa tz ni itv na jamiiforum basi.
 
Ukiona kituo kikubwa cha kitaifa tbc1 kimekaa kimya nini vituo binafc vifanye, uliza mwanahalisi lilikopotelea!
 
Kama sikosei ITV walionesha BREAKING NEWS mchana wa saa nane tisa hivi!!!!
 
Back
Top Bottom