Vituko vya Suleiman “Mbwembwe”

Cesar Saint

JF-Expert Member
Joined
Nov 18, 2016
Posts
423
Reaction score
727
Wasalaam;

Kipindi cha utawala wa bendi Tanzania alikuwapo kijana machachari kutokea Tanga aliyeanza usanii akiwa kama mcheza show katika kumbi mbalimbali za starehe aliyejulikana kwa jina la Suleiman.


Mzee Karenga mwenye gitaa na Mbwembwe kwenye Mic


Mbwembwe,Shabaan Dede na Nasir lubuva

Uwezo wake wa kutunga na kuimba ulimpatia jina la Electronic Voice akipita katika bendi mbalimbali kama Tanzania Stars ,JKT Kimbunga,JUWATA,Vijana Jazz na OTTU (angalia kwenye nyimbo ya kilio cha mtu mzima baada ya verse ya TX Moshi)


Dr Remy ,Mbwembwe na Kawalee Mutimwana

Licha ya kuishi uingereza kwa kipindi flani kituko kikubwa kilichompatia huyu bwana story midomoni mwa watu na wapenzi wa muziki ni kujipenda akitambulishwa kwa mbali na “Mustachi” yake malidhawa.


Suleiman Mbwembwe

Basi kuna kipindi aliyesemekana mpenzi wake wa wakati huo “Salome” aliugua maradhi flani wadau wanasema ilikuwa malaria basi huyu bwana akampeleka bibie Italy eeeh ndio “ITALY” kutibiwa malaria kisha kurejea nae bongo.


Mbwembwe na Hamza Kalala


Huyo ndio Suleiman Mbwembwe .

Mungu amrehemu fundi huyu wa mziki.

Hebu leta kituko au kisa cha Star wa zamani unachokikumbuka.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…