Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 360,000
- 828,761
Ni wazi sasa baadhi ya nchi ya kiafrika zimeamua kwenda kinyume na kanuni za kimataifa za kitaalam za kupambana na virus vya Corona. Ni kama vile Afrika inataka kutoka kivyake na kuithibitishia dunia kuwa AFRIKA IKIAMUA INAWEZA...
Huko Madagascar rais wa nchi hiyo ametangaza kuwa majani ya aina fulani ya chai yanatibu virus vya Corona huku akithibitisha wagonjwa 20 kupona.. Shirika la afya duniani limesema dawa hiyo haijathibitishwa kitaalam na inaweza kuwa na madhara makubwa kiafya
Nchini Tanzania mkuu wa nchi amesisitiza maombi na matumizi ya kuvukiza maji ya mvuke kama tiba na kinga sahihi ya corona lakini wakati huo huo waziri wake wa afya akisema kuvukiza sio njia sahihi na salama kwakuwa njia ya hewa haikuumbwa kupitisha moto... Wananchi wamebaki na kizungumkuti kikubwa kushindwa kujua wamuamini nani
Nchini DRC wao wametoka kivyao... Wanasema virus vya Corona ni uzushi mtupu na wananchi wameanza kuhamasishana kwa njia ya muziki na kula bata.. Kwamba ukijichanganya kwenye kucheza na kurukaruka (dhana ya kutoka jasho) kama ile ya kuvukiza tuu... Virus vinakimbia
Nchini Uganda hali ni tofauti kidogo.. Spika wa Bunge la nchi hiyo ameidhinisha USD million 3 kinyume na maagizo ya mahakama ili zikasaidie mapambano dhidi ya corona huku kila mbunge akiingiziwa USD 3000 toka kwenye hilo fungu.. Ukostaajabu ya Musa utaona ya firauni.. Eti Museveni hana habari na hilo jambo na amewatahadharisha wabunge wasitumie hizo pesa kwakuwa ni kinyume na maamuzi ya mahakama
Huku mitaani mafundi nguo wamepata biashara ya kushona barakoa.. Usalama wake ni kiasi gani? Hilo sio muhimu kwa sasa.. Kikubwa kuziba pua... Utadhani corona ina harufu...
Vyovyote iwavyo Afrika inajaribu kutoa ujumbe fulani kwa mabeberu na hii inaweza kuwa mwanzo wa kuwindana hasa kama njia za Afrika zitafanya kazi.. Lakini mpaka hii corona ipite tutashuhudia mengi mno
Je umesikia na hiki kilio cha nchi za Afrika kutaka kusamehewa madeni yake makubwa na mabeberu ili pesa hizo zitumike kupambana na korona?
Nje ya mada: corona imeua biashara ya lipstick
Jr
Huko Madagascar rais wa nchi hiyo ametangaza kuwa majani ya aina fulani ya chai yanatibu virus vya Corona huku akithibitisha wagonjwa 20 kupona.. Shirika la afya duniani limesema dawa hiyo haijathibitishwa kitaalam na inaweza kuwa na madhara makubwa kiafya
Nchini Tanzania mkuu wa nchi amesisitiza maombi na matumizi ya kuvukiza maji ya mvuke kama tiba na kinga sahihi ya corona lakini wakati huo huo waziri wake wa afya akisema kuvukiza sio njia sahihi na salama kwakuwa njia ya hewa haikuumbwa kupitisha moto... Wananchi wamebaki na kizungumkuti kikubwa kushindwa kujua wamuamini nani
Nchini DRC wao wametoka kivyao... Wanasema virus vya Corona ni uzushi mtupu na wananchi wameanza kuhamasishana kwa njia ya muziki na kula bata.. Kwamba ukijichanganya kwenye kucheza na kurukaruka (dhana ya kutoka jasho) kama ile ya kuvukiza tuu... Virus vinakimbia
Nchini Uganda hali ni tofauti kidogo.. Spika wa Bunge la nchi hiyo ameidhinisha USD million 3 kinyume na maagizo ya mahakama ili zikasaidie mapambano dhidi ya corona huku kila mbunge akiingiziwa USD 3000 toka kwenye hilo fungu.. Ukostaajabu ya Musa utaona ya firauni.. Eti Museveni hana habari na hilo jambo na amewatahadharisha wabunge wasitumie hizo pesa kwakuwa ni kinyume na maamuzi ya mahakama
Huku mitaani mafundi nguo wamepata biashara ya kushona barakoa.. Usalama wake ni kiasi gani? Hilo sio muhimu kwa sasa.. Kikubwa kuziba pua... Utadhani corona ina harufu...
Vyovyote iwavyo Afrika inajaribu kutoa ujumbe fulani kwa mabeberu na hii inaweza kuwa mwanzo wa kuwindana hasa kama njia za Afrika zitafanya kazi.. Lakini mpaka hii corona ipite tutashuhudia mengi mno
Je umesikia na hiki kilio cha nchi za Afrika kutaka kusamehewa madeni yake makubwa na mabeberu ili pesa hizo zitumike kupambana na korona?
Nje ya mada: corona imeua biashara ya lipstick
Jr