LOTH HEMA
JF-Expert Member
- Dec 6, 2015
- 26,860
- 41,401
Watu wamejazana kusachi mifukoni ili angalau watapata hela zilizosahaulika na wenye nguo wa awali. Kuna wafanyabiashara wa nguo za mitumba ambao huwa hawachambui kwanza mitumba yao, wao hufungua palepale marobota na kuyamwaga watu wajichagulie nguo wanazozitaka. Utakuta watu wamejazana wakichagua huku wakisachi mifuko ya mitumba kumbe wengine wanasachi hela za kigeni. Wanapata sarafu na noti za nchi ambazo thamani yake haijulikani ukibadilisha na shilingi ya tanzania. Wanasachi wapate dola ya marekani, pound ya uingereza, euro, rand ya afrika kusini hawapati wanaishia kupata hela za nchi fulani ambazo hazijulikani thamani yake kubadilisha na shilingi ya tanzania na hazipo kwenye orodha ya fedha za kigeni zinazobadilishwa katika benki zetu. Ni kwamba mitumba ya marekani, uingereza haiji Tanzania, ingekuja basi dola na pound zingekutwa zimesahaulika humo mitumbani inayotoka kwenye hizo nchi. Dola ya marekani ndiyo inayotafutwa sana mitumbani