Vituko mitandaoni. Tupia chako

Kuna wakati tulikuwa tunaenda vizuri kwenye huu uzi ,lakini siku mbili hizi kuna Id sijui zilizotokea ni taabu tupu yaani!

Una ziblock tu mkuu maisha ni rahisi sana.
1. Usijibizane nazo

2. Tia kwenye ignore list

3. Endelea na mishe zako

4. Hatuwezi kufanana!
 
Ndiyo maana mimi huwa siamini hii miujiza. Mara ooh aliyekufa miaka 7 iliyopita kafufuka. Ukiuliza ni kweli alikuwa amekufa. Kuna cheti chake cha kifo? Nani alithibitisha?

Oooh inasemekana alifia kwenye machimbo Mwadui. Kuna watu waliomzika. Kamba tupu!

Hata hii miujiza mingi ya mitume na manabii. Kamwe huwezi kukuta kiwete waliyemfanya akatupa magongo kuwa ni wa hapo mtaani mnayemfahamu. Always ni watu wa mbali na magongo yao mapyaaaa!


 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…