HAPA BUSARA INAHITAJIKA
Mwanamke kaazima ndoo ya mpangaji mwenzake chumba cha pili ambae ni kijana hajaoa.Alipomaliza kuoga akajifunga khanga yake moja akatoka bafuni akairudisha ndoo, alipofika ndani kwake akakumbuka amesahau chupi yake kwenye ile ndoo, akatoka harakaharaka vilevile na khanga moja na kugonga mlango.
Jamaa akamwambia aingie ndani aichukue, Anatoka tu mlangoni anakutana na mumewe anatoka kazini kamuona mkewe kavaa khanga moja na mkononi kashika chupi.
Je wewe ungekuwa ni mume au mchumba wake ungefanya maamuzi gani?