Hamuonewi maana nimeishi na nyie kipindi nilikua nafanya mradi fulani hospitali ya Bugando, mnaendana na Waluhya yaani ile balaa, ukitaka ugomvi na Mluhya leta mzaha kwenye ugali. Ni mashemeji zangu huku.
"Tukatae tukubali Wenzetu wa Simba SC Kibiashara wametuzidi na hili Wala halihitaji Mjadala hivyo ni Jukumu letu wana Yanga SC nasi Kujitangaza zaidi kwa Mambo na Maendeleo yetu kuliko kila mara Kuizungumzia Simba SC wakati Sisi bado tuna Safari ndefu ya Kufikia pale walipotutangulia"
"Yaani wana Yanga SC Wenzangu tunaacha kutumia Nguvu Kubwa kutangaza Jezi zetu ambazo bado hazijauzika kihivyo Sisi tuko busy Mitandaoni na Vijiweni Kukosoa Jezi za Simba SC ambayo hata Kimafanikio ya Kimpira kwa sasa wameshatuzidi. Huu ni Upuuzi mkubwa na yatupasa kubadilika"
"Nimesikitika sana kuona Leo hii Yanga SC tumemchukua aliyekuwa Msemaji wao Mkuu ambaye ni Mchumia Tumbo na Kumuamini na kuwa nae. Huyu ndiyo Mtu ambaye Kutwa alikuwa akitutukana vibaya wana Yanga SC mpaka Kutudhalilisha leo kwa Upumbavu Wetu na kwa Utashi fulani tumemkaribisha Kwetu"
Ridhiwani Kikwete MB