Hana majaribu yo yote huyu. Nyie endeleeni kufurahia kwa sababu ni haki yenu. Ndivyo dunia ilivyo. Hata uwe mwema namna gani siku ukitetereka jua utachekwa tu. Alichekwa Bwana Yesu sembuse mimi na weye Ostaadh? Funzo hapa kwangu na wewe ni kwamba tuishi kwa wema na haki lakini pia tutambue kuwa siku tukianguka watu wengi tu watafurahi; na watacheka. Na kama tuliishi maisha mema na yenye kuliwaza roho zetu na za wengine hilo halipaswi kutuumiza