Vituko mitandaoni. Tupia chako

Hakuna machungu yanachoma kama kuanguka ukiwa wima.
Kumbuka huyu ndugu alikuwa juu ya kila kitu ndani ya CCM, kisha kwa muda mfupi akawa juu ya kila mtumishi serikalini.
Hapo alipo sasa yupo chini kuliko mbunge wa jimbo.
Inauma hiyo ila huioni.

Kuna mazingira hela siyo kitu mbele ya heshima hasa kwa jamii aliyotokana nayo ndugu yetu huyo
 
Mwenyewe amewahi kulisema hili? Kuwa anaumia sana kupoteza hizo nafasi? Ataumia tu kama hajitambui. Wangapi tumewaona wakipoteza hizo nafasi wakakaa kimya halafu wakarudi, tena kwa nafasi za juu zaidi? Tena huyu balozi na mbunge?

Simtetei na wala simjui lakini Wabongo tuna tabia mbaya ya kufurahi na kushangilia "wenzetu" wanapoanguka hata kama kuanguka kwao hakutusaidii kwa namna yo yote ile. Tabia hii ipo kuanzia kwenye familia na kwingineko. Ni tabia ya hovyo!
 
Nimecheka kamanda

Watu wanaweza kufurahia kuanguka kwako kama uliwaumiza kwenye utumishi wako.

Hata hivyo kupelekwa bungeni ni sawa na kuhamishiwa field ili aone namna siasa zinavyofanywa kwenye jumba hilo la kutunga sheria.
Kuhusu ubalozi ni sawa, lakini hawezi kulipwa mpaka apangiwe kituo cha kazi.
Kwamba anaweza kuibuka kivingine hilo halina shaka, lakini kwa sasa kuongelea majaribu anayopitia ni haki yetu maana linatuachia funzo kwenye maisha ya siasa.
 
Hana majaribu yo yote huyu. Nyie endeleeni kufurahia kwa sababu ni haki yenu. Ndivyo dunia ilivyo. Hata uwe mwema namna gani siku ukitetereka jua utachekwa tu. Alichekwa Bwana Yesu sembuse mimi na weye Ostaadh? Funzo hapa kwangu na wewe ni kwamba tuishi kwa wema na haki lakini pia tutambue kuwa siku tukianguka watu wengi tu watafurahi; na watacheka. Na kama tuliishi maisha mema na yenye kuliwaza roho zetu na za wengine hilo halipaswi kutuumiza
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…