Vita ya madawa ianzie kwa kutibu arosto kwanza

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
13,718
14,152
Kuyaondoa madawa kwenye jamii kabla ya kuwatambua na kuwasaidia waathirika wote wa dawa hizo ni sawa na kubandika tangazo la kifo kwa waathirika wa dawa hizo.

Watakufa kwa arosto kama wakizikosa dawa hizo ghafla. Ni vema tuanze kwa kuongeza vituo vya kuwasaidia walevi hawa nchini hadi kwenye ngazi ya kila wilaya na kata/ dispensary nchi nzima ili kuwahudumia waathirika watakaozikosa ghafla dawa hizo baada ya dawa hizi kuadimika mitaani, kwa sasa hivi vituo vya aina hii ni vichache sana kuliko idadi ya wagonjwa waliopo nchini.

Vita hii inataka maandalizi, kule ulaya na Marekakani huwa yanaachwa maduka/hospitali maalumu ambazo yanaruhusiwa kuendelea kuuza/kuwapatia madawa hayo waathirika sugu wakati na vituo vya methodon vikiwa vimeenea kila kona ili kuepuka kutenda kosa lingine wakati wa kutatua kosa la kwanza.
 
Nafikiri Serikali kuruhusu vituo vishamiri Ni kuongeza tatizo.
Vituo vifungwe wafe tuu.
Nchi nyingine ukihisiwa umetumia unga Ni matatizo. Ukikamatwa nao Ni kifo.
Sheria za Tanzania Ni dhaifu sana, we are not serious .
 
Nafikiri Serikali kuruhusu vituo vishamiri Ni kuongeza tatizo.
Vituo vifungwe wafe tuu.
Nchi nyingine ukihisiwa umetumia unga Ni matatizo. Ukikamatwa nao Ni kifo.
Sheria za Tanzania Ni dhaifu sana, we are not serious .
nchi gani hizo? Kila project lazima pia izingatie matakwa ya sayansi na haki za watu.

Mtu aliyezoea madawa ukimnyima madawa yake ghafla sayansi inasemaje kwa mtu huyo? ukiambiwa umesababisha kifo chake utabisha?
 
Waache wafe walibwia unga kwa ujinga Wao tunataka taifa lisilo na mateja pumbavu hao wanaotumia
wengine ni watoto wadogo waliodanganywa na kushawishiwa kimakosa, na hawa waachwe wafe? are you serious? na kwa bahati mbaya watumiaji wamesambaa nchi nzima hadi vijijini lakini vituo vya kusaidia arosto viko Dar es Salaam na miji mingine labla miwili mitatu tu. Hatutaeleweka kimataifa! Lazima vita hii iende sambamba na uhudumiaji wa wale watakaopata shida kutokana na kuyakosa haya madawa mitaani, vinginevyo hii vita itakuwa ngumu sana. Mtu mwenye arosto yuko tayari kufanya chochote na yuko tayari kwa lolote hadi apate hizo dawa haramu. Hadi sasa pesa za madawa ya methadone zinatoka nje ya nchi.
 
wengine ni watoto wadogo waliodanganywa na kushawishiwa kimakosa, na hawa waachwe wafe? are you serious? na kwa bahati mbaya watumiaji wamesambaa nchi nzima hadi vijijini lakini vituo vya kusaidia arosto viko Dar es Salaam na miji mingine labla miwili mitatu tu. Hatutaeleweka kimataifa! Lazima vita hii iende sambamba na uhudumiaji wa wale watakaopata shida kutokana na kuyakosa haya madawa mitaani, vinginevyo hii vita itakuwa ngumu sana. Mtu mwenye arosto yuko tayari kufanya chochote na yuko tayari kwa lolote hadi apate hizo dawa haramu. Hadi sasa pesa za madawa ya methadone zinatoka nje ya nchi.

mkuu unamaanisha tutumie kodi zetu kutibu alosto badala ya kuzitumia kuboresha elimu ya watoto wetu
 
mkuu unamaanisha tutumie kodi zetu kutibu alosto badala ya kuzitumia kuboresha elimu ya watoto wetu
kwenye kodi zenu mna kodi zao pia, hata ukinunua chumvi na soda unalipa kodi pia. Takwimu za watumia madawa nchini unazo? wamo maprofesa, madaktari, wahandisi, wafamasia, wanajeshi, wabunge, mawaziri, wanafunzi, matajiri, maskini, wanafunzi, wasanii, wakulima, watoto, wazee, maaskofu, masheikh, n.k
 
Kuyaondoa madawa kwenye jamii kabla ya kuwatambua na kuwasaidia waathirika wote wa dawa hizo ni sawa na kubandika tangazo la kifo kwa waathirika wa dawa hizo.

Watakufa kwa arosto kama wakizikosa dawa hizo ghafla. Ni vema tuanze kwa kuongeza vituo vya kuwasaidia walevi hawa nchini hadi kwenye ngazi ya kila wilaya na kata/ dispensary nchi nzima ili kuwahudumia waathirika watakaozikosa ghafla dawa hizo baada ya dawa hizi kuadimika mitaani, kwa sasa hivi vituo vya aina hii ni vichache sana kuliko idadi ya wagonjwa waliopo nchini.

Vita hii inataka maandalizi, kule ulaya na Marekakani huwa yanaachwa maduka/hospitali maalumu ambazo yanaruhusiwa kuendelea kuuza/kuwapatia madawa hayo waathirika sugu wakati na vituo vya methodon vikiwa vimeenea kila kona ili kuepuka kutenda kosa lingine wakati wa kutatua kosa la kwanza.
Ushawahi kutumia dawa hizo? Hakuna kitu kinaitwa arosto.. huwezi kufa sijui kwa nini unatetea vitu usivyovijua.
 
Nimegundua upelelezi wa watumiaji wa madawa ya kulevya ni mrahisi sana. Unayemshuku ukimuweka korokoroni siku moja tuu lazima aflet kwa kuishiwa nguvu baada ya kukosa madawa.
 
Ushawahi kutumia dawa hizo? Hakuna kitu kinaitwa arosto.. huwezi kufa sijui kwa nini unatetea vitu usivyovijua.
Je wajua madawa ya kulevya yanaathiri kabisa mfumo wa damu? Je ! uliwahi kulala na damu haikuzunguka vizuri mwilini ukaamka umechoka na viungo vinauma nyanganyanga na uswahilini wanasema ulikuwa unafanyishwa kazi na wachawi? Basi kwa taarifa yako mtumiaji aliyebobea akikosa kabisa hata mwili unakuwa wa baridi kabisa kwa moyo kushinwa kusukuma damu, viungo vyote vinauma na kulegea. Kwa kifupi Husababisha ukilema mbaya sana ambao kuutibu unahitaji umakini mkubwa na sii process ya siku moja na mgojwa lazima awe na nia ya dhati ya kuyaacha ashindane na tamaa ya mwili wake. Tuombe Mungu aliondoe janga hili Tanzania.
 
Back
Top Bottom