Sisimizi anajaribu kuangusha tembo! Hawa watu wa Asia sijui wana matatizo gani, walianza japan kuwashambulia marekani yalio wakuta mungu anajua kwa sisi tunaoishi japan tuliowahi kutembelea Nagasaki na Hiroshima ndugu zangu hayo mabomu yasikieni tu! Na hiyo ilikuwa atomic bomb sijui mziki wa nyuklia unakuwaje! Miaka Leo wajapan wanawataka marekani waombe msamaha kwa vita walioianzisha wenyewe! Kama North Korea anataka kuwachokonoa wamarekani awaulize ndugu jirani zake wajapan, ila watajuta Kama sio kulia na kusaga meno, wamarekani wameshapeleka ndege tatu mpaka sasa zenye uwezo wa kubeba nyuklia, ndege hizo zilizosafiri umbali wa karibu 20,000 kilomita non stop! Huu mziki Kama utaanza nikupanda ndege faster kurudi bongo kupumzika, kwani Nina uhakika north korea atapiga japan pia kwani wajapan ni washirika wa kubwa wa wamarekani.