Vita vya korea kaskazini vyaiva......

Vita vya korea kaskazini vyaiva......

Malyenge

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2012
Posts
6,658
Reaction score
3,664
Kwa mujibu wa vyombo mbalimbali vya habari alfajiri hii, kuna uwezekano mkubwa vita vikazuka kati ya Korea kaskazini na Marekani mpaka Korea Kusini. Vyombo vya habari vimekariri wizara ya ulinzi ya Marekani kuwa inalichukulia tishio la Korea Kaskazini kwa uzito mkubwa baada ya jana rais wa Korea Kaskazini Kim Jong Un kusaini nyaraka za kuidhinisha maroketi kuishambulia ardhi ya Marekani.
Hata hivyo, the Pentagon imesema haina uhakika kama Korea Kaskazini inao uwezo na silaha za kushambulia Washington, Hawaii, Los Angeles na Austin, Texas.
 

Attachments

Mkuu achana na B - 2, lakini pia North Korea nao wasikie tu jamaa wanaspirit ya kufa mtu, inawezekana wakawa na siraha kali zaidi. Watu wanasema China ameungana na Marekani kuilaani North Korea, lakini yawezekana ukawa mpango maalumu wa kuendelea kumhujumu marekani aingie kwenda vita ili azidi kushuka kiuchumi. Binafsi siamini kama North Korea anaweza kuishambulia US, naamini anaweza kuishambulia South Korea pamoja na kuwa inakinga kubwa kutoka kwa US.
 
r
Katoto kakililia wembe, mpe ajione mwenyewe. :yo:
 
Kwa mujibu wa vyombo mbalimbali vya habari alfajiri hii, kuna uwezekano mkubwa vita vikazuka kati ya Korea kaskazini na Marekani mpaka Korea Kusini. Vyombo vya habari vimekariri wizara ya ulinzi ya Marekani kuwa inalichukulia tishio la Korea Kaskazini kwa uzito mkubwa baada ya jana rais wa Korea Kaskazini Kim Jong Un kusaini nyaraka za kuidhinisha maroketi kuishambulia ardhi ya Marekani.
Hata hivyo, the Pentagon imesema haina uhakika kama Korea Kaskazini inao uwezo na silaha za kushambulia Washington, Hawaii, Los Angeles na Austin, Texas.
Korea kaskazini nao wamezidi kumuabudu KIm IL Jong na vizazi vyake. Imefikia mahala wanafikia hata kumkabidhi madaraka mtoto mdogo kama huyo raisi wao, eti tuu kwa sababu ni damu ya utawala!! acha marekani waiteketeze maana kufuru ya kuabudu mtu nayo ni kichefu chefu!!!
 
Kama wakipigana hiyo vita haitakuwa nyepesi kama tunavyofikiria wengi! Wananchi wa North Korea wote ni wanajeshi na uzalendo kwa nchi yao ni 100%.

Ingawa binafsi naona huu ni upepo tu unapita hakuna vita itakayopiganwa hapo!!
 
hakuna vita wala nini hapo, hizo ni mbwembwe na hasira za kuku au paka... kujitutumua manyoya na kujivimbisha ili waonekane wakubwa...
 
Back
Top Bottom