Swahilian
JF-Expert Member
- Apr 28, 2009
- 591
- 66
Maisha ya sasa yamekuwa ni tete na siku zinaposonga hakuna kinachoeleweka, hii imekuwa kama laana kwani hata kama unapata pesa basi hazisaidii ktk kuitengeneza hiyo baadaye yetu na wale watokao kwetu miilini, ni wachache wanojenga na ongezeko la watu mijini kusaka keki ya taifa, maisha ya gheto ndio yalotawala, mke watoto chumba kimoja, mpaka watu wanashindwa kununua nguo, hapa inanikumbusha enzi tulipokuwa tukisimuliwa viraka ktk nguo kuulizana!