Stopper3
JF-Expert Member
- Sep 1, 2019
- 625
- 1,030
Hizi ni miongoni mwa mechi zilitoa matokeo ya simanzi kwa timu pinzani.
Kila timu iliyoshinda mechi hizi ilipata mafanikio katika msimu huo, mfano Ujerumani iliitwanga Brazil na ikaenda kubeba kombe la Dunia.
Simba 5 Yanga 0
Emmanuel Okwi aliwanyanyasa sana mabeki wa Yanga hasa Nsajigwa.
Manchester United 8 Arsenal 2
Hiki kipigo mzee Wenger hatakisahau milele, Wayne Rooney katika ubora wake alifunga alivotaka.
Machester United 1 Manchester 6
Ikiwa Old Traford chini ya SAF, Man Utd ilipokea kipigo cha mbwa koko huku David Silva na Edin Dzeko waliitesa vibaya ngome ya Mashetani wekundu.
Brazil 1 Germany 7
Miroslav Klose alifunga goli 1 na kumfanya kuwa mchezaji mwenye magoli mengi zaidi kwenye michuano ya Kombe la Dunia hadi sasa. Kipigo hiki kiliacha simanzi kubwa kwa wapenda soka wa Brazil, hakika usiku ule hawatausahau kamwe.
Barcelona 5 Real Madrid 0
Huku Messi kule C.Ronaldo
Achana na hao, kuna mtu alikua anaitwa Xavi Hernandez, kiungo mahiri kuwahi kumshuhudia akisakata kabumbu, aliwatesa vibaya Madrid pale kati, yaani alichafua dimba na mwenzi Andres Iniesta
Ni Big Mechi ipi wewe unaikumbuka?
Kila timu iliyoshinda mechi hizi ilipata mafanikio katika msimu huo, mfano Ujerumani iliitwanga Brazil na ikaenda kubeba kombe la Dunia.
Simba 5 Yanga 0
Emmanuel Okwi aliwanyanyasa sana mabeki wa Yanga hasa Nsajigwa.
Manchester United 8 Arsenal 2
Hiki kipigo mzee Wenger hatakisahau milele, Wayne Rooney katika ubora wake alifunga alivotaka.
Machester United 1 Manchester 6
Ikiwa Old Traford chini ya SAF, Man Utd ilipokea kipigo cha mbwa koko huku David Silva na Edin Dzeko waliitesa vibaya ngome ya Mashetani wekundu.
Brazil 1 Germany 7
Miroslav Klose alifunga goli 1 na kumfanya kuwa mchezaji mwenye magoli mengi zaidi kwenye michuano ya Kombe la Dunia hadi sasa. Kipigo hiki kiliacha simanzi kubwa kwa wapenda soka wa Brazil, hakika usiku ule hawatausahau kamwe.
Barcelona 5 Real Madrid 0
Huku Messi kule C.Ronaldo
Achana na hao, kuna mtu alikua anaitwa Xavi Hernandez, kiungo mahiri kuwahi kumshuhudia akisakata kabumbu, aliwatesa vibaya Madrid pale kati, yaani alichafua dimba na mwenzi Andres Iniesta
Ni Big Mechi ipi wewe unaikumbuka?