Vipi maandamano ya Nzega?

Vipi maandamano ya Nzega?

measkron

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2011
Posts
3,782
Reaction score
2,418
Naomba kujua Yale maandamano ya amani yafanyike jana huko Nzega yaliyoandaliwa na mbunge Hamisi Kigwangalla, je yalifanyika?
 
Kwasababu kakosa uwaziri wa afya!wakiandamana cdm huyo huwa anabeza wakiandamana wao maandamno ya amani!magamba wameishiwa sasa hawana jipya.
 
unamsikiliza kingwangala anaonekana kuwa mmoja wawalopokaji ndani ya ccm
 
huyu mheshimiwa sijui tumueleweje. anadhani wapiga kura wake bado ni mbumbumbu. Kwa hivi jimbo tayari liko ndani ya gwanda.:llama:
 
Naomba kujua Yale maandamano ya amani yafanyike jana huko Nzega yaliyoandaliwa na mbunge Hamisi Kigwangalla, je yalifanyika?
via RFA nilikisikia kuwa polisi wamwambia HK aandamane na watu wake 1/2km tu hadi uwajani naye alilishukuru jeshi la polisi kwa hilo
 
Maandamano yalifanyika na yalifana sana! Anayeponda aponde, lakini ajue hayamhusu na wala hayakuandaliwa kwa ajili yake!
 
Naomba kujua Yale maandamano ya amani yafanyike jana huko Nzega yaliyoandaliwa na mbunge Hamisi Kigwangalla, je yalifanyika?

Yalifanyika na yalitisha sana! Kazi ilikuwa nzuri, wananchi walijitokeza kwa wingi na mkutano ulikuwa mkubwa japokuwa polisi walikuwa wengi sana, hali iliyotishia baadhi ya watu kujitokeza, soma kwenye youtube utaona kuna video imepostiwa kule pia kwenye Facebook page yangu utaona link ya picha na videos, usiwasikilize wapinga kila kitu cha wabunge wa CCM. Watu hupenda sisi tuwaunge mkono wabunge wa upinzani ila sisi tupingwe kila kitu....double standards!
 
Maandamano yalifanyika na yalifana sana! Anayeponda aponde, lakini ajue hayamhusu na wala hayakuandaliwa kwa ajili yake!

Tunaomba u-quantify yalivyofana Mheshimiwa kwa kuainisha malengo na mafanikio, pia unaweze ku-grade.Thanks, mpiga kura wako aliyeko DSM.
 

Hakuna picha zozote zinazoonesha maandamano hayo zaidi ya hii!! HK tuelekeze wapi tutapata??
 
Yalifanyika na yalitisha sana! Kazi ilikuwa nzuri, wananchi walijitokeza kwa wingi na mkutano ulikuwa mkubwa japokuwa polisi walikuwa wengi sana, hali iliyotishia baadhi ya watu kujitokeza, soma kwenye youtube utaona kuna video imepostiwa kule pia kwenye Facebook page yangu utaona link ya picha na videos, usiwasikilize wapinga kila kitu cha wabunge wa CCM. Watu hupenda sisi tuwaunge mkono wabunge wa upinzani ila sisi tupingwe kila kitu....double standards!
Mheshimiwa, nadhani wanaokupinga na kukwamisha jitihada zako za kuwatetea wapiga kura wako siyo wapinzani bali wabunge wa ccm na uongozi wa chama chako chenyewe.
 
nadhani watakuleteeni picha nyingine muda si mrefu...blog yangu imevamiwa na hivyo inarekebishwa kwa sasa, kule ziliwekwa picha nyingi kidogo zaidi ya hii moja tu iliyowekwa youtube
 
Yalifanyika na yalitisha sana! Kazi ilikuwa nzuri, wananchi walijitokeza kwa wingi na mkutano ulikuwa mkubwa japokuwa polisi walikuwa wengi sana, hali iliyotishia baadhi ya watu kujitokeza, soma kwenye youtube utaona kuna video imepostiwa kule pia kwenye Facebook page yangu utaona link ya picha na videos, usiwasikilize wapinga kila kitu cha wabunge wa CCM. Watu hupenda sisi tuwaunge mkono wabunge wa upinzani ila sisi tupingwe kila kitu....double standards!
Tunawapinga sababu mbunge wa ccm kuitisha maandamano dhidi ya serikali inayoundwa na chama chake does not make sense at all. Labda kama mlikuwa mnaandamana kuunga mkono kauli za nape kwamba wanaokimbia ccm ni oil chafu.

Pia, unaposema yalitisha unamanisha nini?
 
nadhani watakuleteeni picha nyingine muda si mrefu...blog yangu imevamiwa na hivyo inarekebishwa kwa sasa, kule ziliwekwa picha nyingi kidogo zaidi ya hii moja tu iliyowekwa youtube
Mh dr kigwagallah bado hujajibu hoja wewe unategemea matokeo ya maandamano yako itakuwa nini?
 
Yalidoda!
I initially thought kwamba yangedoda, kwa sababu ya short notice kwa kuzuiliwa na police na pia siku yenyewe kulikuwa na polisi (FFU) wengi sana unnecessarily, lakini on a contrary yalifana sana...watu walijitokeza kwa wingi kuliko maelezo, binafsi sikutegemea kwa kweli!
 
Back
Top Bottom