Vipi kama ex aki ......!!

Vipi kama ex aki ......!!

Eiyer

JF-Expert Member
Joined
Apr 17, 2011
Posts
28,259
Reaction score
20,914
Ni kawaida jambo kushindikana kwa sababu mbali mbali,lakini inafikia wakati mtu unatamani iwe kama ulivyotaka lakini mazingira yanakataa

Sasa basi kwenye masuala ya mahusiano nako kuna vimbwanga vyake,inawezekana huko nyuma uliwahi kuwa na mahusiano ambayo hadi leo huwezi kuyasahau na pengine unatamani sana kama yangekuwa ndio ndoa lakini ilishindikana kwasababu mbali mbali ambazo zilikuwa nje ya uwezo wako

Hebu jaribu tu kufikiria,kwa wale ambao waliwahi kuwa na mahusiano ambayo hayakufanikiwa kwenda kwenye ndoa,je kuna mahusiano uliwahi kuwa nayo hadi leo unayakumbuka?

Je unatamani akurudie?

Vipi akikurudia,unaweza kuiweka ndoa yako hatarini kwa kuchepika nae ili ukumbushie mavituz ya kale?

Najua unaweza kuwa na kigugumizi lakini ukweli unaweza kuwa upo wazi kuwa kuna baadhi ambao walikuwa na mahusiano ambayo walitamani ndio yangekuwa njia kuu lakini yalishindikana na hadi leo wanayakumbuka na wana wish hata warudiane hata wawe mchepuko tu

Hebu jiulize hayo maswali hapo juu na uangalie kama kuna cha kujifunza kutoka kwenye hayo mahusiano yako ya kale!!
 
yani umekuja kutonesha ndugu, before huyu wa sasa, uwa namkumbuka sana na mpaka nasema sijui nivunje ila najipa jibu kuwa kila na jambo na wakati wake, wacha nimpende huyu niliye nae sasa.
Hapana mkuu sijatonesha bali najaribu kuwafanya kukumbuka na hatimae kusahau

Kumbuka huwezi kupata kila unachokitaka maishani

Hongera kwa kujua kuwa unatakiwa upende na kuheshimu ulipo sasa!
 
Sasa hebu lianzishe Eiyer
 
Last edited by a moderator:
Sina ex ambaye natamani au najutia kumpoteza. Nilijisikia vizuri kipindi hicho, tulimalizana vizuri, japo wengine ilichukua mda kumalizana, lakini sijutii..!!

...labda niseme tu kuwa haya ni madhara ya kuwa na ex wengi, huoni tofauti. Ninachojuta ni kujiingiza kwenye malove kabla ya ndoa..
 
Sina ex ambaye natamani au najutia kumpoteza. Nilijisikia vizuri kipindi hicho, tulimalizana vizuri, japo wengine ilichukua mda kumalizana, lakini sijutii..!!

...labda niseme tu kuwa haya ni madhara ya kuwa na ex wengi, huoni tofauti. Ninachojuta ni kujiingiza kwenye malove kabla ya ndoa..

Mkuu inaonekana wewe ulikuwa hatari kwenye haya mambo eehh!!
 
mi x sitaki hata kumsikia kifo kingekua kinaombewa ningemwombea afe

Pole ....

Inaonekana una hasira sana,unamjua babu ODM a.k.a Asprin ?

Ni bingwa wa kuondoa hasira,hebu mtafute halafu utaona hasira zinavyoondoka kama mshumaa kwenye moto!
 
Last edited by a moderator:
nianze kwa kujifunza,mwanamke ni mtu wa kubadilika muda wowote ule. mwaka na miezi 3 sasa tangu aliponiacha maumivu alioniachi hayaelezeki na mpaka muda huu sijaona wa kufanana nae japo alikuwa wa kawaida lakin kwa upendo niliokuwa nao kwake natamani kurudiana nae,na nileo nilikuwa nawazia hilo ila sijui nianzie wapi.lakin nimempenda sana,ushauri wangu kama uko na mpenzi wako wakati huu,usijaribu kamwe kufikiria kumuacha taabu yake hasimuliki nawaapien msijaribu.
 
Huwa sijuti wala kuangalia nyuma, the past is gone and i have to focus for the future.

i dont keep memories, because its a stupid move.
 
Pole ....

Inaonekana una hasira sana,unamjua babu ODM a.k.a Asprin ?

Ni bingwa wa kuondoa hasira,hebu mtafute halafu utaona hasira zinavyoondoka kama mshumaa kwenye moto!

du! huyu mzee namuogopa sana!!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom