Vipaumbele vya Awamu ya Tano

Rufiji

Platinum Member
Jun 18, 2006
1,881
941
Nimekuwa nikifuatilia siasa zetu kwa karibu na kuna vitu vimekuwa vikinitatiza. Inawezekanaje Mbunge wa Arusha, Mheshimiwa Lema, awekwe kizuizini kwa zaidi ya miezi miwili, kwa kosa la kuota wakati huo huo kuna kiongozi alikula hela za kujenga kiwanda huko Lindi, chenye thamani za dola za Kimarekani milioni ishirini hajakamatwa? Kwa nini serikali inakuwa na upendeleo wa dhahiri?
 
Ujinga ni pale unapotumia fedha za Maendeleo ya Afya, Elimu, miundombinu, n.k kwa ajili yakununua Bajaj, halafu baadae unaenda kukopa na riba juu, kwa ajili ya maendeleo.

Ujinga ni pale unapokiuka misingi ya Demokrasia kwa mujibu wa Katiba, Kisha ukanyimwa misaada ya bure na na isiyo na Riba (free aid), Kisha kwa mbembwe ukawakejeli waliokunyima, eti hauzihitaji fedha zao na kwamba unajiweza, halafu baada ya muda ukarudi kulekule kukopa na riba juu.
 
Vipaumbele vya awamu ya tano
1,ununuzi wa ndege :tumeshanunua mbili kwa cash na tumeshaanza kulipia nyingine kubwa zaidi .japo kipaumbele hiki hakikuwepo kwenye mpango wa mwaka huu wala bajeti ya bunge.pia japo ndege halikuwa tatizo la msingi la mwananchi mnyonge
2, ujenzi wa uwanja wa ndege chato, hata kama ujenzi huo ni nje ya bajeti ya nchi.
3, kuhamia dodoma,hata kama haikuwa agenda ya uchaguzi kwa 5yrs na hata kama haikuwa kwenye bajeti
4, kudhoofisha upinzani kwa gharama yoyote,hata kama upinzani umeleta faida kubwa ya kimaendeleo kwa ukosoaji na ushauri wake kwa serikali lakini kwa awamu hii tunataka kibaki chama tawala tu
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom