Antar bin Shaddad
JF-Expert Member
- Oct 11, 2010
- 202
- 101
kikao cha kamati ya utekelezaji ya UV-CCM mkoa wa Arusha kimevunjika leo baada ya wajumbe wawili Mrisho Gambo na mwenyekiti wa UV-CCM wilaya Karatu Bayo kutiana makonde kavukavu na baadaye mwenyekiti kutiwa mbaroni na polisi.
Wajumbe hao walizipiga kavukavu baada ya mkti huyo wa karatu kujaribu kumzuia Gambo kwa madai kuwa si mjumbe halali wa kikao hicho kilichokuwa kinaoongozwa na kaimu Mwenyekiti Esther Maleko ambaye alikaimishwa na Mwenyekiti James Ole Millya.
Baada ya vurugu hizo kikao kilivunjika na na Mwenyekit huyo alikamatwa na polisi na hadi majira ya saa mbili usiku alikuwa bado yuko mahabusu ya kituo kikuu cha polisi mjini Arusha
Awali kabla kuibuka kwa vurugu wajumbe walilazimika kupiga simu kwa Katibu Mkuu wa UV-CCM Martine Shigela kuuliza uhalali wa Gambo kushiriki kikao hicho na Shigela aliwajibu kuwa hakuna kikao chochote kilichiowahi kumsimamisha Gambo hivyo ni mjumbe halali na kutokana na majibu hayo ndipo Mwenyekiti wa Karatu alipoamua kujichukulia sheria mkononi kujaribu kumtoa Gambo kwa nguvu ndani ya kikao.
Chanzo cha kumtoa Gambo inaelezwa kuwa ni hatua ya mjumbe huyo kukataa kuungana na kundi la vijana wa arusha wakioongozwa na Millya ambao wamenunuliwa kumfanyia kammpeni Lowassa katika harakati za kuwania Urais 2015.Nawasilisha
Wajumbe hao walizipiga kavukavu baada ya mkti huyo wa karatu kujaribu kumzuia Gambo kwa madai kuwa si mjumbe halali wa kikao hicho kilichokuwa kinaoongozwa na kaimu Mwenyekiti Esther Maleko ambaye alikaimishwa na Mwenyekiti James Ole Millya.
Baada ya vurugu hizo kikao kilivunjika na na Mwenyekit huyo alikamatwa na polisi na hadi majira ya saa mbili usiku alikuwa bado yuko mahabusu ya kituo kikuu cha polisi mjini Arusha
Awali kabla kuibuka kwa vurugu wajumbe walilazimika kupiga simu kwa Katibu Mkuu wa UV-CCM Martine Shigela kuuliza uhalali wa Gambo kushiriki kikao hicho na Shigela aliwajibu kuwa hakuna kikao chochote kilichiowahi kumsimamisha Gambo hivyo ni mjumbe halali na kutokana na majibu hayo ndipo Mwenyekiti wa Karatu alipoamua kujichukulia sheria mkononi kujaribu kumtoa Gambo kwa nguvu ndani ya kikao.
Chanzo cha kumtoa Gambo inaelezwa kuwa ni hatua ya mjumbe huyo kukataa kuungana na kundi la vijana wa arusha wakioongozwa na Millya ambao wamenunuliwa kumfanyia kammpeni Lowassa katika harakati za kuwania Urais 2015.Nawasilisha