Najaribu kutafakari mwenendo mzima wa viongozi wetu kiuongozi na kiutendaji, napata maswali kadhaa bila majibu.
Jicho langu leo linawachungulia wale wanaotokea mkoa wa Morogoro (si lazima wawe na asili ya huko kimakabila).
1. Celina Ompeshi Kombani:
Licha ya kuwa ni mbunge wa Ulanga Mashariki, pia ni Waziri wa Sheria na Katiba. Mojawapo ya mambo ambayo tunamkumbuka huyu mama ni wakati wa vuguvugu la kudai katiba mpya, ambapo bila aibu alijitokeza hadharani na kusema kuwa hatuna haja ya katiba mpya kwani iliyopo bado ni nzuri sana. Alikuja kuaibika siku chache baadaye wakati Rais alipotangaza nia ya kuanza mchakato wa katiba mpya.
Inasemekana jimboni kwake hajaonekana tangu alipopata ubunge na wananchi wake wako katika hali mbaya sana kwa kukosa huduma muhimu, ambazo yeye aliwaahidi kuwatumikia pindi wangemchagua.
Anatuhumuwa kushirikiana na Abdul Mteketa kuchakachua kura katika jimbo la Kilombero zilizomwezesha ndg. Mteketa kutangazwa mshindi wa jimbo hilo na kumpoka mgombea wa chadema ambaye ndiye alikuwa chaguo la wananchi.
2. Hadji Hussein Mponda
Huyu ni mbunge wa Ulanga Magharibi na vilevile ni Waziri wa Afya na Ustawi wa jamii.
Kama alivyo Kombani (jirani yake), naye pia ameshindwa kuongoza jimbo lake na kutatua kero/matatizo ya wapiga kura wake.
Anaonekana kuwa ni waziri asiye na "sauti" wala maamuzi hasa pale anapotakiwa kutoa maamuzi sahihi na ya haraka.
Ameshindwa kutatua mgogoro wa hivi karibuni wa madaktari ambao chanzo chake ni uozo uliopo katika wizara ambayo yeye anaiongoza, na matokeo yake kusababisha adha kubwa kwa wananchi vikiwemo vifo ambavyo vingeweza kuepukika.
Katika kipindi chote cha mgogoro wa madaktari, hakuwahi kutoa japo kauli yenye kuonesha nia yake ya kutatua mgogoro huo na badala yake alikaa kimya hadi pale walio chini yake walipotoa maamuzi yaliyochochea mgogoro huo na kufanya hali kuwa mbaya zaidi.
3. Mustafa Haidi Makunganya Mkulo:
Ni mbunge wa Kilosa na Waziri wa Fedha na Uchumi.
Licha ya kuwa na uzoefu mkubwa wa mambo ya fedha na uchumi lakini aemshindwa kabisa kutumia uzoefu wake huo katika nafasi aliyopo kulisaidia taifa.
Taifa limekumbwa na mfumuko mkubwa wa bei na hali ngumu ya maisha ambayo haijawahi kutokea kwa miaka mingi mno.
Anaonekana kupwaya sana katika nafasi hiyo na hajui nini cha kufanya ili kulikwamua taifa kutoka katika hali ngumu.
Kwa mara ya kwanza tunasikia nchi haina fedha kwenye akiba yake, yeye akiwa ndio mwenye dhamana ya hayo mambo.
Ameshindwa kusaidia wapiga kura wake hasa pale walipopata na maafa makubwa ya mafuriko. Alisubiri muda wa kupokea misaada tu ili "auze sura".
4. Lucy Sawere Nkya:
Ni mbunge wa Morogoro Kusini-Mashariki na ni Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii.
Kama mwenziye Mponda, huyu alishindwa kabisa kutatua mgogoro wa wizara ya Afya na badala yake inasemekana alichangia kwa kiasi kikubwa kukuza mgogoro huo katika hatua ambayo ulifikia akishirikiana na katibu mkuu wa wizara hiyi bi. Blandina Nyoni.
Hana uwezo wa kutafuta suluhu ya matatizo pindi anapotakiwa kufanya hivyo.
Anonekana ana element ya ubinafsi.
Ameshindwa kuwatumikia wapiga kura wa jimbo lake.
5. Abdul Rajab Mteketa:
Ni mbunge wa Kilombero.
Ana elimu ya cheti tu.
Inasemekana hajawahi kutembelea jimbo lake hadi wakati wa msiba wa marehemu Regia.
Ameshindwa kabisa kuwatumikia wananchi wake.
Alishirikiana na akina Kombani na Mponda kuchakachua kura za mgombea wa chadema katika jimbo la Kilombero.
Hatakiwi kabisa na wananchi wa Kilombero.
6. Benno Ndulu:
Ni gavana wa Benki kuu.
Ni mwenyeji wa Ulanga.
Kama Mkulo, ameshindwa kutumia nafasi yake ya ugavana na uzoefu wake wa mambo ya fedha na uchumi katika kushughulikia suala la mfumuko wa bei.
Hali ngumu waliyonayo watanzania inatokana na mfumuko wa bei ambao yeye ni mdau mkuu wa kushughulikia tatizo hilo.
Aliwahi kutuhumiwa kufanya ukarabati wa nyumba ya gavana na naibu wake kwa mabilioni ya shilingi (ufisadi?).
Ukiangalia kwa makini ni kuwa nafasi nyingi nyeti serikalini zinashikiliwa na watu ambao wengi wao ama wana asili ya mkoa wa Morogoro au ni wakazi wa muda mrefu wa maeneo ya mkoa huo.
Bado napata shida kama kuna uhusiano wowote kati ya mkoa huo na kuboronga kwa viongozi ambao wanatokea huko.
Kuna matatizo gani Morogoro?
Hapo sijawataja akina Liyumba, Ngasongwa.......na wengineo....
Nita-update kwa kadri nitakapopata muda.
Ni hayo tu kwa sasa.
Jicho langu leo linawachungulia wale wanaotokea mkoa wa Morogoro (si lazima wawe na asili ya huko kimakabila).
1. Celina Ompeshi Kombani:
Licha ya kuwa ni mbunge wa Ulanga Mashariki, pia ni Waziri wa Sheria na Katiba. Mojawapo ya mambo ambayo tunamkumbuka huyu mama ni wakati wa vuguvugu la kudai katiba mpya, ambapo bila aibu alijitokeza hadharani na kusema kuwa hatuna haja ya katiba mpya kwani iliyopo bado ni nzuri sana. Alikuja kuaibika siku chache baadaye wakati Rais alipotangaza nia ya kuanza mchakato wa katiba mpya.
Inasemekana jimboni kwake hajaonekana tangu alipopata ubunge na wananchi wake wako katika hali mbaya sana kwa kukosa huduma muhimu, ambazo yeye aliwaahidi kuwatumikia pindi wangemchagua.
Anatuhumuwa kushirikiana na Abdul Mteketa kuchakachua kura katika jimbo la Kilombero zilizomwezesha ndg. Mteketa kutangazwa mshindi wa jimbo hilo na kumpoka mgombea wa chadema ambaye ndiye alikuwa chaguo la wananchi.
2. Hadji Hussein Mponda
Huyu ni mbunge wa Ulanga Magharibi na vilevile ni Waziri wa Afya na Ustawi wa jamii.
Kama alivyo Kombani (jirani yake), naye pia ameshindwa kuongoza jimbo lake na kutatua kero/matatizo ya wapiga kura wake.
Anaonekana kuwa ni waziri asiye na "sauti" wala maamuzi hasa pale anapotakiwa kutoa maamuzi sahihi na ya haraka.
Ameshindwa kutatua mgogoro wa hivi karibuni wa madaktari ambao chanzo chake ni uozo uliopo katika wizara ambayo yeye anaiongoza, na matokeo yake kusababisha adha kubwa kwa wananchi vikiwemo vifo ambavyo vingeweza kuepukika.
Katika kipindi chote cha mgogoro wa madaktari, hakuwahi kutoa japo kauli yenye kuonesha nia yake ya kutatua mgogoro huo na badala yake alikaa kimya hadi pale walio chini yake walipotoa maamuzi yaliyochochea mgogoro huo na kufanya hali kuwa mbaya zaidi.
3. Mustafa Haidi Makunganya Mkulo:
Ni mbunge wa Kilosa na Waziri wa Fedha na Uchumi.
Licha ya kuwa na uzoefu mkubwa wa mambo ya fedha na uchumi lakini aemshindwa kabisa kutumia uzoefu wake huo katika nafasi aliyopo kulisaidia taifa.
Taifa limekumbwa na mfumuko mkubwa wa bei na hali ngumu ya maisha ambayo haijawahi kutokea kwa miaka mingi mno.
Anaonekana kupwaya sana katika nafasi hiyo na hajui nini cha kufanya ili kulikwamua taifa kutoka katika hali ngumu.
Kwa mara ya kwanza tunasikia nchi haina fedha kwenye akiba yake, yeye akiwa ndio mwenye dhamana ya hayo mambo.
Ameshindwa kusaidia wapiga kura wake hasa pale walipopata na maafa makubwa ya mafuriko. Alisubiri muda wa kupokea misaada tu ili "auze sura".
4. Lucy Sawere Nkya:
Ni mbunge wa Morogoro Kusini-Mashariki na ni Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii.
Kama mwenziye Mponda, huyu alishindwa kabisa kutatua mgogoro wa wizara ya Afya na badala yake inasemekana alichangia kwa kiasi kikubwa kukuza mgogoro huo katika hatua ambayo ulifikia akishirikiana na katibu mkuu wa wizara hiyi bi. Blandina Nyoni.
Hana uwezo wa kutafuta suluhu ya matatizo pindi anapotakiwa kufanya hivyo.
Anonekana ana element ya ubinafsi.
Ameshindwa kuwatumikia wapiga kura wa jimbo lake.
5. Abdul Rajab Mteketa:
Ni mbunge wa Kilombero.
Ana elimu ya cheti tu.
Inasemekana hajawahi kutembelea jimbo lake hadi wakati wa msiba wa marehemu Regia.
Ameshindwa kabisa kuwatumikia wananchi wake.
Alishirikiana na akina Kombani na Mponda kuchakachua kura za mgombea wa chadema katika jimbo la Kilombero.
Hatakiwi kabisa na wananchi wa Kilombero.
6. Benno Ndulu:
Ni gavana wa Benki kuu.
Ni mwenyeji wa Ulanga.
Kama Mkulo, ameshindwa kutumia nafasi yake ya ugavana na uzoefu wake wa mambo ya fedha na uchumi katika kushughulikia suala la mfumuko wa bei.
Hali ngumu waliyonayo watanzania inatokana na mfumuko wa bei ambao yeye ni mdau mkuu wa kushughulikia tatizo hilo.
Aliwahi kutuhumiwa kufanya ukarabati wa nyumba ya gavana na naibu wake kwa mabilioni ya shilingi (ufisadi?).
Ukiangalia kwa makini ni kuwa nafasi nyingi nyeti serikalini zinashikiliwa na watu ambao wengi wao ama wana asili ya mkoa wa Morogoro au ni wakazi wa muda mrefu wa maeneo ya mkoa huo.
Bado napata shida kama kuna uhusiano wowote kati ya mkoa huo na kuboronga kwa viongozi ambao wanatokea huko.
Kuna matatizo gani Morogoro?
Hapo sijawataja akina Liyumba, Ngasongwa.......na wengineo....
Nita-update kwa kadri nitakapopata muda.
Ni hayo tu kwa sasa.