Muke Ya Muzungu
JF-Expert Member
- Jun 17, 2009
- 3,444
- 264
[MODS TAFADHALI MSIFUTE HII MADA] !
Kinachoendelea nchini Tanzania ni chimbuko la machafuko makubwa isipodhibitiwa. Haya yalitokea Libya, Tunisia na Misri. Nina maana ya kwamba kuna ubaguzi mkubwa kuanzia kwenye elimu hadi kwenye haki zetu za msingi kaka ajira. Viongozi wetu wamekuwa wakichochea machafuko kwa kutumia dhamana tuliyowapa vibaya kutunyima haki zetu za msingi.
Kinachoendelea nchini Tanzania ni chimbuko la machafuko makubwa isipodhibitiwa. Haya yalitokea Libya, Tunisia na Misri. Nina maana ya kwamba kuna ubaguzi mkubwa kuanzia kwenye elimu hadi kwenye haki zetu za msingi kaka ajira. Viongozi wetu wamekuwa wakichochea machafuko kwa kutumia dhamana tuliyowapa vibaya kutunyima haki zetu za msingi.
- Nafasi za masomo zinapotoka nje ya nchi, hawa wakubwa wanakusanya watoto wao kwa njia za panya na kuwapeleka kusoma katika vyuo vyenye hadhi kubwa
- Nafasi za kazi, kwenye ubalozi, mashirika ya umma kama TRA, NSSF, BoT nk ni watoto wao ndio wanaongizwa bila kuzingatia qualifications mbaya zaidi hawa vijana wana arrogance mbaya sana na dharau kwetu sisi watoto wa masikini. Mfano ni wale wanaofanya kazi kwenye mabalozi na BOT
- Kwenye siasa wanalazimisha na hata kufikia kupindisha taratibu ili kuwapa watoto wao madaraka.
- Watoto wa wakubwa wanafanya uonevu mkubwa mtaani, lakini ukipeleka uonevu wao kwenye vyombo vya dola na mahakama, unageuziwa wewe kesiWatoto wao wamekuwa kama viongozi, wanajilimbikizia mali, wanafanya ufisadi kila idara ya serikali. Wanadiriki kuwatishia maisha yeyote anayepinga matakwa yao