PreGE2025 Vijana watakiwa kujiepusha na vitendo vya uvunjivu wa amani

PreGE2025 Vijana watakiwa kujiepusha na vitendo vya uvunjivu wa amani

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Wont be the same

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2024
Posts
1,564
Reaction score
2,483
Vijana nchini Tanzania hususani waliopo vyuoni wametakiwa kuwa mstari wa mbele katika kudumisha utulivu, amani na kutojihusisha na vitendo vya uvunjifu wa amani.

Wito huo umetolewa na Mdau wa Maendeleo na mwanasiasa wa mkoani Iringa Shalom Robert wakati akizungumza na Umoja wa Vijana wa CCM Tawi la chuo Kikuu cha Iringa ulifanyika katika ukumbi wa CCM kata ya Kihesa.

Shalom ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mkutano huo alisema wakati tukielekea katika uchaguzi mkuu kuna kuwepo na vitendo mbalimbali viovu ikiwemo rushwa hivyo ndio wakati wa vijana kupambana navyo na kuviepuka na kudumisha utulivu na amani.

“Naombeni twendeni tukaepuke rushwa kwasababu Kuna mambo kadha wa kadha huwa yanatokea Katika kipindi hiki Vijana twendeni tukapinge hayo mambo maovu lakini twendeni tukamsikilize yule mwenye sera ambaye yupo tayari kutuongoza” alisema
 
Vijana nchini Tanzania hususani waliopo vyuoni wametakiwa kuwa mstari wa mbele katika kudumisha utulivu, amani na kutojihusisha na vitendo vya uvunjifu wa amani.

Wito huo umetolewa na Mdau wa Maendeleo na mwanasiasa wa mkoani Iringa Shalom Robert wakati akizungumza na Umoja wa Vijana wa CCM Tawi la chuo Kikuu cha Iringa ulifanyika katika ukumbi wa CCM kata ya Kihesa.

Shalom ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mkutano huo alisema wakati tukielekea katika uchaguzi mkuu kuna kuwepo na vitendo mbalimbali viovu ikiwemo rushwa hivyo ndio wakati wa vijana kupambana navyo na kuviepuka na kudumisha utulivu na amani.

“Naombeni twendeni tukaepuke rushwa kwasababu Kuna mambo kadha wa kadha huwa yanatokea Katika kipindi hiki Vijana twendeni tukapinge hayo mambo maovu lakini twendeni tukamsikilize yule mwenye sera ambaye yupo tayari kutuongoza” alisema
View attachment 3342759
kuchagiza uchaguzi huru na wa haki sio uvunjifu wa Amani

bali ni kuchagiza misingi ya Demokrasia
 
Kwa nini hawawaambii watekaji waache uvunjifu wa amani? Hakuna kijana anaevunja amani ya nchi ila ukikosoa serikali unaambiwa unavunja amani.

Amani inayolindwa ni ya viongozi kuzidi kufanya mambo bila kukosolewa.
 
Back
Top Bottom