Vijana waongoza maambukizi ya VVU

Vijana waongoza maambukizi ya VVU

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,618
Reaction score
9,607
Takwimu zinaonyesha kuwa vijana na watoto nchini ndiyo wanaoongoza kupata maambukizo ya Virusi vya Ukimwi (VVU) duniani.

Takwimu za hivi karibuni za Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulika na masuala ya Ukimwi (UNAIDS) zinaonyesha kuwa asilimia 40 ya maambukizi mapya ya VVU duniani yanatokana na vijana kuanzia miaka 15 hadi 24.

Meneja mawasiliano na uraghibishi kutoka taasisi ya Elizabeth Glasser inayopambana na ukimwi kwa watoto (Egpaf) Mkama Mwijarubi, alisema hayo jana akiwa katika klabu za watoto waishio na VVU Hospitali ya Kibosho na KCMC zilizopo Mkoani Kilimanjaro.

Mwijarubi alisema vijana wengi wameathirika kwa sababu ya kutokuwa na tahadhari yoyote na hivyo kuendelea kuambukizana wenyewe kwa wenyewe na kuchangia kuendelea kuwapo kwa maambukizo mapya.

Alisema idadi kubwa ya watoto wameambukizwa na wazazi wao tangu wakiwa tumboni na hivyo wanapozaliwa wanakuwa tayari wameathirika.

“Kutokana na changamoto hiyo taasisi hiyo ilifikia hatua ya kuwekeza kuwaangalia watoto na vijana kuanzia umri wa 0 hadi miaka 14 ambapo kijana akifikisha umri wa miaka 17 humwacha ajihudumie mwenyewe,” alisema.

Mkurugenzi Mkazi wa Egpaf, Jeroen Van’t Pad Bosch alisema taasisi hiyo ilianza kufanya kazi nchini tangu mwaka 2003 lengo likiwa ni kupambana na VVU kwa watoto.


Mwananchi
 
Hatari

Sent from my Iphone 7 using JamiiForums mobile app

 
Hatari iliyoko kwa vijana ni kutoka kwa hawa mabint waliozaliwa miaka ya 200 wakiwa na VVU ...na mbaya wawo hawajijui kama HIV+.

Wakitongozwa hawakatai, mnyororo ndio unaanzia hapa!
 
Hata mimi ningeshangaa kusikia Wazee ndo wanaoongoza kwa maambukizi ya VVU
 
Kundi lingine lililoko hatarini kwa maambukizi ni watu wa umri wa kati 45-65 hawa Mara wanapofiwa au kuachika huwa hawa hawakumbuki kinga na protection kwasababu wana kuwa wamekaa kwenye mahusiano na mtu mmoja kwa miaka mingi.

Kwa wanawake wengine wana fikiria tu nimeshapita minopouse condom ya nini tena kumbe kuna maambukizi ya HIV nje nje mtaani.
 
waambukizwe tu maana wengi ni sababu ya ujinga wao
 
Back
Top Bottom