Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,338
- 9,766
Ndugu zangu watanzania,
Mkoani Iringa kuna vijana takribani 37 wameandamana mpaka ofisi za CCM kuishukuru serikali ya Rais samia kupitia Mh Ridhiwani Kikwete naibu waziri ofisi ya Rais menejimenti ya utumishi wa umma na utawala bora aliyefika mkoani hapo.
Vijana hao wamekuwa wakijitolea kwa miaka mingi katika nafasi za utendaji wa mitaa,mfano kuna wengine wamefanya kazi ya kujitolea na kufanya kazi na majukumu ya utendaji wa mitaa kwa miaka takribani tisa. Lakini ilipofika wakati wa kuomba ajira serikalini vijana hao wapatao 47 ambao walikuwa katika maeneo mbalimbali ya manispaa ya Iringa walijikuta vijana 37 wanaachwa kwa kigezo kuwa hawana sifa.japo wamefanya kazi ya kujitolea na kutimiza majukumu yao vyema kabisa.
Ridhiwani Kikwete akiongea kwa uchungu mkubwa na maumivu makubwa na huruma kubwa kwa vijana hao walioonyesha uzalendo kwa Taifa lao ,alihoji mamlaka mkoani Iringa kuwa iweje kwenye kuwafanyia usaili kuingia serikalini waseme vijana hao hawana sifa wakati wamefanya kazi hiyo kwa kujitolea na kukaimishwa nafasi za utendaji wa mitaa kwa muda mrefu? Akauliza unawezaje kumkaimisha mtu ofisi unayefahamu hana uwezo wala sifa?
Kikwete kwa uchungu mkubwa alisema muogopeni Mungu ndugu zanguu.na kusema kuwa kama wizara wamepitia na kuangalia wasifu wao na kila kitu na wamebaini na kujiridhisha kuwa vijana hao wana sifa na wamekidhi vigezo .hivyo kutoa maelekezo ya kuwarudisha vijana hao wote kazini.jambo lililo leta na kuamsha tabasamu,furaha na matumaini katika mioyo ya vijana hao wanaotoka familia maskini na wenye kutegemewa na familia zao zilizowasomesha kwa kujinyima na kujibana hadi kushindwa kupata milo mitatu ya chakula kwa siku ili mradi watoto wao wasome na kutimiza ndoto zao.
Hii ndio maana ya CCM kuwa Nuru,Tumaini na kimbilio la wanyonge. Ndio maana mtu akionewa au kunyimwa haki au kudhulumiwa haki yake anakuwa na matumaini kuwa akifika katika ofisi za CCM atapata majibu, tumaini na kufutwa machozi. Ndio maana vijana hawa walikimbilia ofisi za CCM tu na kuwaona viongozi wa CCM na kuwaeleza shida yao .ambapo viongozi wa CCM wakiongozwa na mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia CCM mh Ritha kabati waliwapambania vijana hawa kwa nguvu zao zote mpaka hatimaye wamepata haki yao.
Hii ndio serikali ya Rais samia inayotoa haki kwa haki kwa watu wote.haitaki dhuluma wala uonezi wala unyanyasaji wala ukandamizaji kwa watu au mtu.ni serikali safi na yenye matendo safi.ni sauti ya watu na mtetezi wa wanyonge. Watanzania endeleeni kuiamini ccm na serikali yake kwa kuwa imedhamilia kuwainua na kumshika mkono kila mtu mwenye kuhitaji msaada au sauti ya kumtetea au kumsaidia au kumuwezesha kusonga mbele.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.
Mkoani Iringa kuna vijana takribani 37 wameandamana mpaka ofisi za CCM kuishukuru serikali ya Rais samia kupitia Mh Ridhiwani Kikwete naibu waziri ofisi ya Rais menejimenti ya utumishi wa umma na utawala bora aliyefika mkoani hapo.
Vijana hao wamekuwa wakijitolea kwa miaka mingi katika nafasi za utendaji wa mitaa,mfano kuna wengine wamefanya kazi ya kujitolea na kufanya kazi na majukumu ya utendaji wa mitaa kwa miaka takribani tisa. Lakini ilipofika wakati wa kuomba ajira serikalini vijana hao wapatao 47 ambao walikuwa katika maeneo mbalimbali ya manispaa ya Iringa walijikuta vijana 37 wanaachwa kwa kigezo kuwa hawana sifa.japo wamefanya kazi ya kujitolea na kutimiza majukumu yao vyema kabisa.
Ridhiwani Kikwete akiongea kwa uchungu mkubwa na maumivu makubwa na huruma kubwa kwa vijana hao walioonyesha uzalendo kwa Taifa lao ,alihoji mamlaka mkoani Iringa kuwa iweje kwenye kuwafanyia usaili kuingia serikalini waseme vijana hao hawana sifa wakati wamefanya kazi hiyo kwa kujitolea na kukaimishwa nafasi za utendaji wa mitaa kwa muda mrefu? Akauliza unawezaje kumkaimisha mtu ofisi unayefahamu hana uwezo wala sifa?
Kikwete kwa uchungu mkubwa alisema muogopeni Mungu ndugu zanguu.na kusema kuwa kama wizara wamepitia na kuangalia wasifu wao na kila kitu na wamebaini na kujiridhisha kuwa vijana hao wana sifa na wamekidhi vigezo .hivyo kutoa maelekezo ya kuwarudisha vijana hao wote kazini.jambo lililo leta na kuamsha tabasamu,furaha na matumaini katika mioyo ya vijana hao wanaotoka familia maskini na wenye kutegemewa na familia zao zilizowasomesha kwa kujinyima na kujibana hadi kushindwa kupata milo mitatu ya chakula kwa siku ili mradi watoto wao wasome na kutimiza ndoto zao.
Hii ndio maana ya CCM kuwa Nuru,Tumaini na kimbilio la wanyonge. Ndio maana mtu akionewa au kunyimwa haki au kudhulumiwa haki yake anakuwa na matumaini kuwa akifika katika ofisi za CCM atapata majibu, tumaini na kufutwa machozi. Ndio maana vijana hawa walikimbilia ofisi za CCM tu na kuwaona viongozi wa CCM na kuwaeleza shida yao .ambapo viongozi wa CCM wakiongozwa na mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa kupitia CCM mh Ritha kabati waliwapambania vijana hawa kwa nguvu zao zote mpaka hatimaye wamepata haki yao.
Hii ndio serikali ya Rais samia inayotoa haki kwa haki kwa watu wote.haitaki dhuluma wala uonezi wala unyanyasaji wala ukandamizaji kwa watu au mtu.ni serikali safi na yenye matendo safi.ni sauti ya watu na mtetezi wa wanyonge. Watanzania endeleeni kuiamini ccm na serikali yake kwa kuwa imedhamilia kuwainua na kumshika mkono kila mtu mwenye kuhitaji msaada au sauti ya kumtetea au kumsaidia au kumuwezesha kusonga mbele.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.