black abdu
Senior Member
- Dec 2, 2022
- 157
- 214
Juzi kuna mshakaji wangu ameomba nimuazime kiasi kidogo cha fedha kwa ahadi ya kurudisha siku inayofuata...lakini hadi sasa amepiga kimya... kabla ya huyu kuna mwingine aliomba nimuazime pia, mshahara wake ukitoka angenirejeshea, nae hadi leo kimya.
Nawaza labda mambo yao hayajakaa sawa, lakini hata text tu ya kusema "samahani nitachelewa kidogo na amana yetu"?!
Haikuanzia kwa hawa wawili, huko nyuma nilimuazima mtu pesa ku-boost mtaji wake, lakini hadi leo amebaki na 5k baada ya kulipa kwa mbinde hadi ilifikia siku nilichukua bidhaa yake nikamwambia akate kwenye salio la deni. Mwengine nimemsamehe 30k, aliazima pesa ndefu kiasi kuwa anashida ya upesi lkn hadi nilitengeneza uongo kuwa pesa niliyompa niliazima kwa mtu na mwenyewe anataka kuja kuchukua vitu vya ndani, ndio akaanza kulipa kidogo kidogo na uongo mwingi.
Siku moja mshikaji kanieleza fikra yake ya biashara nikajitoa kiherehere kumkopesha pesa ya mtaji, tena niliazima kwa mtu lakini sikuona senti tano na ikabidi lile deni nilikipe mwenyewe.
Kinachofuata ni kuwa nitafunga milango ya kusaidiana, yaani mtu akija na shida zake labda nimpe kama mchango na si mkopo, na hapo itategemea niwe na pesa ambayo haitaacha "gepu" endapo nitaitoa.
Siku hizi ndio ule usemi ukimkopesha rafiki yako jiandae kupoteza pesa na kumpoteza rafiki, ila rafiki wa kweli huwezi kumpoteza kama ni mwaminifu na kama si mwaminifu hafai kuwa rafiki!
Nawaza labda mambo yao hayajakaa sawa, lakini hata text tu ya kusema "samahani nitachelewa kidogo na amana yetu"?!
Haikuanzia kwa hawa wawili, huko nyuma nilimuazima mtu pesa ku-boost mtaji wake, lakini hadi leo amebaki na 5k baada ya kulipa kwa mbinde hadi ilifikia siku nilichukua bidhaa yake nikamwambia akate kwenye salio la deni. Mwengine nimemsamehe 30k, aliazima pesa ndefu kiasi kuwa anashida ya upesi lkn hadi nilitengeneza uongo kuwa pesa niliyompa niliazima kwa mtu na mwenyewe anataka kuja kuchukua vitu vya ndani, ndio akaanza kulipa kidogo kidogo na uongo mwingi.
Siku moja mshikaji kanieleza fikra yake ya biashara nikajitoa kiherehere kumkopesha pesa ya mtaji, tena niliazima kwa mtu lakini sikuona senti tano na ikabidi lile deni nilikipe mwenyewe.
Kinachofuata ni kuwa nitafunga milango ya kusaidiana, yaani mtu akija na shida zake labda nimpe kama mchango na si mkopo, na hapo itategemea niwe na pesa ambayo haitaacha "gepu" endapo nitaitoa.
Siku hizi ndio ule usemi ukimkopesha rafiki yako jiandae kupoteza pesa na kumpoteza rafiki, ila rafiki wa kweli huwezi kumpoteza kama ni mwaminifu na kama si mwaminifu hafai kuwa rafiki!