Vijana wa Kitanzania na tabia za fisi

Mchimwachimego

JF-Expert Member
Jun 15, 2020
358
271
Kiumri mimi siwezi kujiita kijana ila nimepitia huko katika nchi yetu hii Tanzania nguvu kazi kubwa ni vijana wasomi na wasio wasomi hawa wote hulka zao nazifananisha na fisi msituni, maisha yake yote fisi msituni utumia nguvu nyingi katika kunyang'anya mawindo ya wanyama wengine, kuokota mizoga, kuwinda wanyama wagonjwa na ndama.

Fisi hajui mbinu za kuwinda, ratiba yake ya kesho itajulikana kesho yeye hawezi kujitafutia kwa akili zake na maarifa yake yeye utegemea wenzake wafanye kazi ili ale makombo au apole kwa nguvu.

Hivyo hivyo ndivyo vijana wengi wa Kitanzania walivyo na tabia za fisi ukiwakuta katika maongezi na mipango wanayoizungumzia unaweza kusema hapa tuna wasomi lakini vitendo ni bure kabisa, mtu amesomea teaching, mifugo, kilimo, biashara, mipango miji, fundi mitambo, ujenzi nk: lakini ukimwambia afanye alichikisomea hawezi kazi yao ni kufuga vitambi na kulalamikia mishahara.

Wapo wengine huku mitaani wanaamini kuwa ukiwa na degree basi wewe kazi yoyote ya mikono haikuhusu na si hadhi yako, nawaomba vijana mubadilike elimu ni kuongeza maarifa tu ni lazima muvifikilishe vichwa vyenu kugungundua na kubuni fulsa mpya na vitu vipya vitakavyowaongezea ubunifu zaidi, kwenye ulimwengu wa leo ukianzisha kitu kipya kitakupa faida sana kuliko kuiga cha mwingine.

Asanteni.
 
Duh vijana wanalaumiwa kila uchao...

Likija swala la mahusiano wanalaumiwa hawako romantic, caring, hawana mbinu mpyaa za kutongoza

Swala la kutunza familia wanalaumiwa

Likija swala la kisiasa wanalaumiwa hawana msimamo wala hawawezi fanya maamuzi sahihi

Maofisini kutwa kuchwa wanalaumiwa kutaka fedha za faster na kujenge/kununua magari

Kwenye maswala ya Ibada (dini zote) vijana wanalaumiwa kutopenda kushiriki shughuli za ibada hadi waanzapo ona uzee unabisha hodi ... apa anayebisha na abishee

Vijana changamkeniii amukeniii nyie ni taifa la leo na sio taifa la kesho
 
Tatizo siyo vijana jamii ielimishwe kwanza maana jamii ndiyo inawakatisha tamaa hawa wasomi ukitaka kujua Kuna changamoto ya kufanya kazi hizi ambazo hujasomea kati ya watu kumi unaokutana nao wawili tu ndiyo watakupongeza.
Hawa wengine watakukatisha tamaa na kukushangaa.
Kwa mazingira yalivyo hapa Tanzania huwezi kwenda ulikozaliwa ukaanze kufuga hata kuku maana Kijiji kitakushangaa vijana wanabidi wende sehemu za kigeni ili wakapambane.
Usilaumu vijana anza kwanza kuelimisha jamii inayowazunguka.​
 
Tatizo siyo vijana jamii ielimishwe kwanza maana jamii ndiyo inawakatisha tamaa hawa wasomi ukitaka kujua Kuna changamoto ya kufanya kazi hizi ambazo hujasomea kati ya watu kumi unaokutana nao wawili tu ndiyo watakupongeza.
Hawa wengine watakukatisha tamaa na kukushangaa.
Kwa mazingira yalivyo hapa Tanzania huwezi kwenda ulikozaliwa ukaanze kufuga hata kuku maana Kijiji kitakushangaa vijana wanabidi wende sehemu za kigeni ili wakapambane.
Usilaumu vijana anza kwanza kuelimisha jamii inayowazunguka.​
Unachoongea ni kwel kabisa , kiuhalisia mm ni msomi niliejiajiri kwa kufungua biashara , ingawa mtaji niliupata baada ya kufanya kazi ya mkataba , pindi nilipoanza biashara aisee watu walikua wananishangaa tuu, lakini sikuwajali , hawakujua mambo ya kutembea na bahasha na kuwanyeyekea watu yanavyokera , nilijipa moyo na kukomaa nikasema sitafuti kazi tena mm ilimradi nimeshapata mtaji acha nikomae na biashara yangu , namshukuru mungu mpaka sasa naendelea na biashara yangu c haba, cha msingi hapa jamii inatakiwa ibadilike na c kukariri kua ukisoma huwezi fanya kanzi nyingine ambayo hata mtu ambayo hakusoma anaweza ifanya , mashuleni tuanenda kuongeza maarifa tuu
 
Unachoongea ni kwel kabisa , kiuhalisia mm ni msomi niliejiajiri kwa kufungua biashara , ingawa mtaji niliupata baada ya kufanya kazi ya mkataba , pindi nilipoanza biashara aisee watu walikua wananishangaa tuu, lakini sikuwajali , hawakujua mambo ya kutembea na bahasha na kuwanyeyekea watu yanavyokera , nilijipa moyo na kukomaa nikasema sitafuti kazi tena mm ilimradi nimeshapata mtaji acha nikomae na biashara yangu , namshukuru mungu mpaka sasa naendelea na biashara yangu c haba, cha msingi hapa jamii inatakiwa ibadilike na c kukariri kua ukisoma huwezi fanya kanzi nyingine ambayo hata mtu ambayo hakusoma anaweza ifanya , mashuleni tuanenda kuongeza maarifa tuu
Hongera sana, vijana inatakiwa kujiongeza katika shughuli za kujiajiri tusisubiri kuajiriwa.
 
Tatizo siyo vijana bali ni mfumo mzima unaowaandaa hawa vijana, ikiwemo mfumo wa malezi, afya ya kijana kiujumla tangu akiwa mtoto ikiwemo lishe, ubora wa elimu unaomtengeneza kijana kujiamini, kuwa mbunifu na jasiri katika kufanya jambo jipya na kuleta mabadiliko chanya katika jamii....ikiwemo namna uongozi wa nchi ulivyojikita katika kusimamia haki na sheria na kukemea kwa dhati mambo yasiyo ya kimaadili ikiwemo rushwa, matumizi mabaya ya madaraka, madawa ya kulevya nk.
 
Back
Top Bottom