Upo mchezo mchafu wa baadhi ya wanasiasa kuwadanganya watu wenye hali za chini na wanaotafuta ajira kuwa watawapatia ajira na watawaboreshea maisha yao.
Jambo baya kwenye mchezo huo ni kuwapa watu matumaini makubwa yaliyo nje ya uwezo wa nchi yetu hata kama Obama akiletwa awe Rais wetu kwa miaka kumi hawezi kutekeleza ahadi hizo
Hivi kweli mtu anayetaka Urais aseme bado siku 50 mwenye ng'ombe wawili atakua na ng'ombe wanne? ni kweli baada ya siku 50 mwenye kibajaji atakuwa na gari?
Kutokana na ugumu wa maisha na ukossefu wa ajira watu hawa wanakubali kwa shangwe na kuunga mkono bila kupima uhalisia wa mambo ulivyo.
Ni kweli kuna tatizo la ajira lakini ukweli ni kwamba hilo ni tatizo la dunia nzima, kila nchi inajitahidi kutatua tatizo hilo kadiri ya uwezo wa nchi hiyo, lakini siyo kudanganya watu kua bado siku 50 kila asiye na ajira atapata ajira.
Mtatumika kuwapigia debe wagombea hao, mtaandamana, mtavunjwa miguu lakini wakipata fursa ya kuingia ikulu watawasahau na kubadilisha kauli zao kwakua waliahidi vitu visivyowezekana.
Hivi umeshawahi kuona au kusikia nchi ambayo watu wake wote wana ajira? katika dunia hii ni rais gani aliweza kuwatoa watu wote wenye pikipiki hadi kumiliki magari tena ndani ya muda mfupi?
Umasikini wenu ni mtaji wao wa kisiasa, wanasema kwa ncha za ndimi zao lakini ndani ya nyoyo zao hawamaanishi wakinenacho. kuweni watulivu kisha mupembue sera kwa kuangalia uhalisia na utekelezaji wake. Najivunia kusema kuwa Magufuli ndiye mgombea bora mwenye sera zinazotekelezeka.
Nawatakia kila la heri kwenye safari hii ya kuelekea October 25, safari iliyobeba maisha yetu ya miaka mitano kama si kumi.
Mungu ibariki Afrika
Mungu ibariki Tanzania
Jambo baya kwenye mchezo huo ni kuwapa watu matumaini makubwa yaliyo nje ya uwezo wa nchi yetu hata kama Obama akiletwa awe Rais wetu kwa miaka kumi hawezi kutekeleza ahadi hizo
Hivi kweli mtu anayetaka Urais aseme bado siku 50 mwenye ng'ombe wawili atakua na ng'ombe wanne? ni kweli baada ya siku 50 mwenye kibajaji atakuwa na gari?
Kutokana na ugumu wa maisha na ukossefu wa ajira watu hawa wanakubali kwa shangwe na kuunga mkono bila kupima uhalisia wa mambo ulivyo.
Ni kweli kuna tatizo la ajira lakini ukweli ni kwamba hilo ni tatizo la dunia nzima, kila nchi inajitahidi kutatua tatizo hilo kadiri ya uwezo wa nchi hiyo, lakini siyo kudanganya watu kua bado siku 50 kila asiye na ajira atapata ajira.
Mtatumika kuwapigia debe wagombea hao, mtaandamana, mtavunjwa miguu lakini wakipata fursa ya kuingia ikulu watawasahau na kubadilisha kauli zao kwakua waliahidi vitu visivyowezekana.
Hivi umeshawahi kuona au kusikia nchi ambayo watu wake wote wana ajira? katika dunia hii ni rais gani aliweza kuwatoa watu wote wenye pikipiki hadi kumiliki magari tena ndani ya muda mfupi?
Umasikini wenu ni mtaji wao wa kisiasa, wanasema kwa ncha za ndimi zao lakini ndani ya nyoyo zao hawamaanishi wakinenacho. kuweni watulivu kisha mupembue sera kwa kuangalia uhalisia na utekelezaji wake. Najivunia kusema kuwa Magufuli ndiye mgombea bora mwenye sera zinazotekelezeka.
Nawatakia kila la heri kwenye safari hii ya kuelekea October 25, safari iliyobeba maisha yetu ya miaka mitano kama si kumi.
Mungu ibariki Afrika
Mungu ibariki Tanzania