Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,286
- 10,831
Nakataa! Hawa sio wavivu, wamejituma kwenye kilimo, kiliwapora mitaji yao kwa ukosefu wa masoko na sera nzuri za kuwalinda wakulima, wafanye nini? Kwanza hata wakifanya kilimo hawafanyi kilimo kama wakulima (farmers) bali wao huwa peasnats tu, ambao hawawezi kupata faida kwenye kilimo hicho. Wakulima mnawajua kina Sumry au kina Masanja na wengine.
Hao siyo wavivu kwa kuwa wanajua wakikamatwa maisha yao yataishia jela lakini they take the risk anyway. Ndiyo wale wakiona gari ya mafuta imepinduka hawezi kuikimbia bali huikimbilia ili kupata namna ya kunusuru maisha yao. Hawa sio wavivu.
Kuna haja ya serikali kuangalia upya sera za vijana na ajira, ila kikubwa nilishawahi kusema, kwanza kuwe na marketing kubwa ya ile mikopo ya halmashauri na PTF, na masharti ya mikopo yabadilishwe ili kuleta tija kwa vijana wanaoweza kujiajiri ili wawaajiri na wengine.
Kama wimbi hili la vijana litabaki mtaani kama ilivyo hivi sasa, nadhani miaka si mingi ijayo tutaanza kuongeza majengo ya magereza kwa kuwa wafungwa watakuwa wengi.
Tuwatazame vijana.
Hao siyo wavivu kwa kuwa wanajua wakikamatwa maisha yao yataishia jela lakini they take the risk anyway. Ndiyo wale wakiona gari ya mafuta imepinduka hawezi kuikimbia bali huikimbilia ili kupata namna ya kunusuru maisha yao. Hawa sio wavivu.
Kuna haja ya serikali kuangalia upya sera za vijana na ajira, ila kikubwa nilishawahi kusema, kwanza kuwe na marketing kubwa ya ile mikopo ya halmashauri na PTF, na masharti ya mikopo yabadilishwe ili kuleta tija kwa vijana wanaoweza kujiajiri ili wawaajiri na wengine.
Kama wimbi hili la vijana litabaki mtaani kama ilivyo hivi sasa, nadhani miaka si mingi ijayo tutaanza kuongeza majengo ya magereza kwa kuwa wafungwa watakuwa wengi.
Tuwatazame vijana.